Morogoro: Treni ya SGR (Dar-Dodoma) yakwama Kidete Kilosa kwa zaidi ya saa 4, sababu Hitilafu ya Umeme

Morogoro: Treni ya SGR (Dar-Dodoma) yakwama Kidete Kilosa kwa zaidi ya saa 4, sababu Hitilafu ya Umeme

Changamoto ni jambo la kawaida, iwe umeme au changamoto za train yenyewe.

Tusiwe wepesi kuponda au kuzodoa, hakuna kitu kimefanikiwa undwa kwa ufanisi wa 100%

Pole kwa abiria wote waliokwama.
 
Ni muhimu TRC wakatoa taarifa nini kilitokea kusababisha train ya jana usiku kutoka Dar to Dom kukwama zaidi ya masaa manne Kidete na kufika Dodoma karibia saa 8 na nusu usiku badala ya saa 4 usiku.

Shida yangu sio kwamba matatizo hayawezi kutokea ila shida ni customer care katika utoaji wa taarifa. Hii train ndio kwanza tumeanza na kesho ndio inazinduliwa rasmi ila hii limetia doa sherehe yote ya kesho.

Je, pre-commissioning haikufuatwa kama inavyotakiwa, tumekimbiza tu haraka kufanikisha malengo ya kisiasa?

TRC mambo kama haya wanatakiwa kuyatolea maelekezo ya kina. Jana train imechelewa display yao still inaonesha train arrival saa 4 na nusu hakuna kuonesha delays na kutoa matangazo taarifa kwanini kuna delays.

TRC toeni maelezo ya kina au ndio sabotage zimeanza.
 
Au umeme uliisha?
Jamani tusicheke 😉 ndio maana tunataka waeleze nini kimetokea, kutoa taarifa sahihi ndio rahisi kupata dawa. Nakumbuka toka siku ya kwanza nilitoa ombi kazi ya operation watafute mbia aendeshe kama private kujitegemea ili kulete ufanisi. Na serikali kuchukua % kubwa ya mapato ili gharama zirudi lakini kuwapa TRC kama wafanyakazi wa serikali tutasubiri siku ya kuzika tu kama Reli ya kati na Tazara.
 
Mlikuwa mnalazimisha ianze fasta mkishadidia eti angekuwepo Magufuli ingeshaanza Toka 2021 🤣🤣🤣🤣

Kwanza sidhani hata kama testing ya kutosha imefanyika kati ya Moro-Dodoma
 
Mtaambiwa tu kuna hujuma ilikuwa imefanyika mahali nyaya zilikatwa.

Ndicho mkitarajie hicho.
 
Back
Top Bottom