Moshi: Amuua mama yake wakigombea mali za marehemu baba yake

Moshi: Amuua mama yake wakigombea mali za marehemu baba yake

Hamna mtu mwenye akili timamu atakayeweza kufanya jambo kama Hilo. Kinachotokea hapo huyo mtoto alikuwa ni mtu wa hivyo ndio maana hata mama yake hakutaka kumpa hizo mali. Mbona ni akili kidogo Sana kumrubuni mama.
 
Ukanda huo kuna shida kubwa sana kuhusiana na suala la kugombea mali. Ni hatari Sana.
Mimi naona ni tatizo la mtu binafsi, ila kama wewe una uhakika yapo mengi ya kugombea mali za uridhi;
naomba uweke reference tatu za watu waliogombea mali ya uridhi tofauti na hiyo hapo
 
Huko moshi jamaa wa miaka 54 amemuua mama yake wa miaka 74 kwa sababu ya ugonvi wa mali alizoacha baba ama mume wa marehemu ambae ndio baba wa mtuhumiwa.

Marehemu aliacha mashamba, hayo ndio yameleta mgogoro hadi jamaa akaamua kumuua mama yake.

Matukio ya hovyo ya watu kuua wazazi wao kisa mali yanashamiri sana Kilimanjaro.
---

Adela Mushi (74), mkazi wa Okaseni, kata ya Uru kusini, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro anadaiwa kuuawa kwa kunyongwa na kisha kukatwa na shoka sehemu ya usoni na mwanaye, anayedai mali zilizoachwa na marehemu baba yake.

Inadaiwa kuwa mtoto wake huyo mwenye umri wa miaka 54, alifanya tukio hilo usiku wa Septemba 23, 2024 na kisha kutelekeza mwili wa mama yake ndani ya chumba chake alichokuwa anaishi.

Mwili wa mama huyo ulikutwa ukiwa umelazwa kifudifudi huku shingoni kukiwa kumefungwa kipande cha kanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo akieleza kuwa jeshi hilo linamshikilia mwanaume huyo kwa mahojiano zaidi.

“Septemba 23, 2024 usiku wa saa 4, maeneo ya Uru Okaseni, mwanamke ajulikanaye kwa jina la Adela Dominick Mushi, aliuawa kwa kupigwa na kitu butu kichwani kisha kunyongwa kwa kutumia kipande cha kanga na mtoto wake aitwaye Nemes Dominic,” amesema Kamanda Maigwa.

Kamanda Maigwa amesema chanzo cha mauaji hayo kinachunguzwa , lakini wawili hao walikuwa na ugomvi wa muda mrefu wakigombea mashamba na mali za marehemu.

Mwananchi
Kuna ushahidi gani? Kuwa na ugomvi sio kigezo..
 
Ndio maana wazungu ukifika 18 years you're ready to go, sasa huku kwetu wazazi wamezidi kuonea huruma watoto wao matokeo ndio haya. Kufuga fuga mwisho wanafuga majini. R.I.P ma'am 💔
 
Hamna logic unagombania mali na mama kweli!? Labda ingekuwa ndugu .
 
Dah miaka 74 mama yake si angemlea tu na sio kumuua kwa maana angemuachia tu mama ake then after a while vingerudi kwake vyote.
Kesi ya yule bint sijui unakumbuka mwaka jana ila aliachiwa huru nasikia ...Naye aliua mama yake kisa mali huko huko kilimanjaro .

Kiufupi pesa ina fitina sana , jaribu kwenda migodini uoe watu wanauawa bila ya huruma kisa pesa.
 
Mali ya baba ako aliye muoa Mama ako unaenda kugombea Kama mliolewa wote vile.
Vijana tujikaze Muda tunaopoteza ndio tunajipoteza Sisi. Muda umekubeba wewe.
 
Back
Top Bottom