Libya
JF-Expert Member
- Nov 11, 2016
- 790
- 1,968
Wagombea wa CHADEMA Moshi wakataliwa kupokelewa fomu zao na Mkurugenzi.
======
Mkurugenzi amegoma kupokea fomu baada ya tuhuma za awali kwamba sio halisi na kutaka kabla wahusika hawajazirudisha wakathibitishe polisi kama ni halisi ama La.
Baada ya katibu wa CHADEMA kuhoji iwapo vyama vyote vinaenda polisi kuthibitisha, amejibu yeye aliemtuhumu na wote waliomtuhumu ndio wanatakiwa kwenda polisi kuzithibitisha kabla hawajazileta kwake.
Pia katibu wa CHADEMA alilalamikia kuwa na risiti za aina mbili kwa wagombea wa CCM na CHADEMA ambapo risiti za CHADEMA zimekuwa printed kwenye computer ilhali za CCM ni stakabadhi ya halmashauri.
Kuhusu hilo mkurugenzi, amemtaka kuwasilisha kwa maandishi malalamiko yao na yeye atakaa na wataalam kuangalia kipi ni kipi lakini amesema uko utata, zipo ambazo ni stakabadhi kama za mahakama, nyingine za mfumo na nzuri ni ya stakabadhi lakini wakitaka majibu wawasilishe malalamiko yao.
Pia mwenyekiti amelalamika suala la risiti ya mgombea ubunge kuandikwa ni ya mgombea udiwani, mkurugenzi ametaka wayawasilishe wamalizane.
=====
Kwa upande wake mkurugenzi amesema ametoa fomu halali na CHADEMA wakaandika barua na kumpelekea wakimtuhumu amewapa fomu zisizo halisi na baadae kwenda polisi. Ikabidi awaandikie kwamba hilo suala halina shida lakini kwa kuwa wameenda polisi, yeye hana uweza wa kutambua kitu 'fake' hivyo watafute mamlaka yenye weledi wa kutambua hivyo asingeweza kuzipokea.
======
Mkurugenzi amegoma kupokea fomu baada ya tuhuma za awali kwamba sio halisi na kutaka kabla wahusika hawajazirudisha wakathibitishe polisi kama ni halisi ama La.
Baada ya katibu wa CHADEMA kuhoji iwapo vyama vyote vinaenda polisi kuthibitisha, amejibu yeye aliemtuhumu na wote waliomtuhumu ndio wanatakiwa kwenda polisi kuzithibitisha kabla hawajazileta kwake.
Pia katibu wa CHADEMA alilalamikia kuwa na risiti za aina mbili kwa wagombea wa CCM na CHADEMA ambapo risiti za CHADEMA zimekuwa printed kwenye computer ilhali za CCM ni stakabadhi ya halmashauri.
Kuhusu hilo mkurugenzi, amemtaka kuwasilisha kwa maandishi malalamiko yao na yeye atakaa na wataalam kuangalia kipi ni kipi lakini amesema uko utata, zipo ambazo ni stakabadhi kama za mahakama, nyingine za mfumo na nzuri ni ya stakabadhi lakini wakitaka majibu wawasilishe malalamiko yao.
Pia mwenyekiti amelalamika suala la risiti ya mgombea ubunge kuandikwa ni ya mgombea udiwani, mkurugenzi ametaka wayawasilishe wamalizane.
=====
Kwa upande wake mkurugenzi amesema ametoa fomu halali na CHADEMA wakaandika barua na kumpelekea wakimtuhumu amewapa fomu zisizo halisi na baadae kwenda polisi. Ikabidi awaandikie kwamba hilo suala halina shida lakini kwa kuwa wameenda polisi, yeye hana uweza wa kutambua kitu 'fake' hivyo watafute mamlaka yenye weledi wa kutambua hivyo asingeweza kuzipokea.