Moshi: Waliotuhumiwa kuua walinzi wa Asante Tours na kupora Tsh. Milioni 65 washinda kesi

Moshi: Waliotuhumiwa kuua walinzi wa Asante Tours na kupora Tsh. Milioni 65 washinda kesi

Nani atakuwa mlinzi wa walinzi wetu!
 
Polisi wana weledi mdogo sana au hawapendi kuhangaika kupata ushahidi ndio maana wanafanya makosa ambayo wanashindwa kuwatia watu hatiani.

Wao wakikamata mtu wanataka wamtese ili asaini hayo makaratasi yao basi wawe wamemaliza kazi,sasa mtuhumiwa anaweza kukubali tu kusaini ili asiteswe Ila akifika mahakamani anakataa anasema nililazimishwa.

Kama hawa watuhumiwa ndio waliohusika kuua,kwanini ushahidi umekosekana?Je hawakukutwa na pesa zilizoibwa?bunduki ilitumika?taarifa gani iliwafanya polisi wawakamate hawa watu na si wengine?
 
Upande Jamhuri hususan wa mawakili wasomi wa serikali ofisi ya DPP / NPS wapikwe vizuri kitaaluma ili kulisaidia jeshi la Polisi ili haki iweze kupatikana inapostahiki.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania​

OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA​


Mkurugenzi wa Mashtaka​

MKURUGENZI WA MASHTAKA
Mkurugenzi wa Mashtaka ni mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka. Mkurugenzi wa Mashtaka ndiye msimamizi mkuu wa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka, Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi, Mawakili wa serikali na Waendesha Mashtaka katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
Majukumu ya Mkurugenzi wa Mashtaka yatakuwa ni:
  • (i)Kuamua kushtaki au kutoshtaki kwenye makosa ya jinai;
  • (ii)Kuanzisha, kuendesha na kusimamia mashtaka ya makosa ya jinai katika mahakama zote isipokuwa mahakama za kijeshi;
  • (iii)Kutwaa na kuendelea na mashtaka ya kesi yoyote ya jinai iliyofunguliwa na mtu au taasisi nyingine;
  • (iv)Kufuta mahakamani mashtaka yoyote ya jinai yaliyofunguliwa na mtu au taasisi nyingine katika hatua yoyote kabla hukumu kutolewa;
  • (v)Kutoa maagizo kwa jeshi la polisi au vyombo chunguzi vyoyote kuchunguza taarifa yoyote ya kijinai na kutoa taarifa kwake haraka inavyowezekana;
  • (vi)Kuchukua hatua muhimu kwa jambo lolote lenyetija katika mashtaka ya jinai;
  • (vii)Kutoa miongozo inayohusu uratibu wa upelelezi na uendeshaji mashtaka;
  • (viii)Kuteua na kutenguamamlaka ya waendesha mashtaka wa umma;
  • (ix)Kumshauri waziri mwenye dhamana katika masualaya mashtaka yanayohitaji sera au hatua za kibunge;
  • (x)Kuteuwa maafisa maalum ndani ya taasisi za serikali kusimamia mali zilizozuiliwa au kutaifishwa na mahakama katika mazingira ambayo ni vigumu kuteua wasii;
  • (xi)Kufanya kazi nyingine ambayo zinahusiana na mashtaka ya umma;
  • (xii)Kuwasimamia maafisa sheria, mawakili wa serikali na watumishi wengine walioteuliwa au kuajiriwa na ofisi ya taifa ya mashtaka;
  • (xiii)Kusimamia shughuli zote zinazofanywa na maafisa sheria, mawakili wa serikali na watumishi wengine ndani ya ofisi ya taifa ya mashtaka;
  • (xiv)Kuita afisa yoyote wa umma kutoa maelezo au taarifa kuhusiana na jambo lolote ambalo linahusu mashtaka ya umma;
  • (xv)Kuandaa na kuwasilishakwa waziri taarifa ya nusu mwaka na nakala kwa mwanasheria mkuu wa serikali kuhusu utekelezaji wa majukumu ya ofisi ya taifa ya mashtaka; na
  • (xvi)Kuteua au kuajiri na kuwajibisha maafisa sheria, mawakili wa serikali na watumishi wengine ndani ya ofisi ya taifa ya mashtaka
Source: https://www.nps.go.tz/pages/director-of-public-prosecutions
 
Walioachiwa huru ni Erick Teete, Fadhili Mohamed, John Daniel, Nassoro Nassoro, Paschal Mushi, Ibrahim Mkindi, Robert Massawe na Juma Hamis Ramadhan.

Uamuzi huo umetolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Moshi dhidi ya watuhumiwa walioshtakiwa kwa mauaji ya walinzi wa kampuni ya Utalii ya Ahsante Tours pamoja na uporaji wa Tsh. Milioni 65.5 Julai 3, 2016.

Watuhumiwa wameachiwa huru baada ya Jaji Adrian Kilimi kuukataa ushahidi wa Jamhuri wa maelezo ya Onyo na Video zilizorekodiwa na Polisi akisema Ushahidi wa Jamhuri ulitakiwa kuungwa mkono na Ushahidi Huru na hivyo Jamhuri imeacha mashaka kwa kushindwa kuthibitisha Mashtaka.

=========================

Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, imewaachia huru washitakiwa wote wanane waliokuwa wakituhumiwa kwa mauaji ya walinzi wa kampuni ya kuhudumia watalii ya Ahsante Tours, mauaji ambayo yaliambatana na uporaji wa Sh65.5 milioni.

Mauaji na uporaji huo wa fedha zikiwamo Dola 23,300 za Marekani na Sh15 milioni za Tanzania, yaliyotokea Julai 3, 2016 yaliutikisa mji wa Moshi kutokana na kampuni hiyo kuwa ya pili kwa ukubwa, ikitanguliwa na kampuni ya Zara Tours.

Walioachiwa huru na Jaji Adrian Kilimi, ni Erick Teete, Fadhili Mohamed, John Daniel, Nassoro Nassoro, Paschal Mushi, Ibrahim MkindI maarufu kwa jina la Ibra, Robert Massawe maarufu kwa jina la Kipara na Juma Hamis Ramadhan.

Upande wa mashitaka ulikuwa unadai kuwa siku ya tukio huko eneo la Shanty Town katika Manispaa ya Moshi, washitakiwa waliwaua kwa makusudi na bila uhalali, Dominic Cheddy na Omary Idd Amin waliokuwa walinzi wa Ahsante Tours.

Maelezo ya tukio hilo yaliyowasilishwa mahakamani ni kwamba siku ya tukio marehemu hao walikuwa wakitekeleza jukumu lao la ulinzi, ndipo usiku wa siku hiyo washitakiwa walidaiwa kuvamia ofisi hiyo na kupora fedha hizo.

Ni katika kipindi hicho cha uporaji, ndipo washitakiwa walidaiwa kuchukua maamuzi ya kuwaua walinzi hao baada ya kubaini kuwa mlinzi mmoja alikuwa amemtambua mmoja wao hivyo kuhofia kuwa angewataja washitakiwa.

Miili ya walinzi hao iligunduliwa asubuhi ya saa moja na katika upelelezi wa Polisi, ndipo mshitakiwa wa pili, Fadhil Mushi alikamatwa na katika mahojiano ilielezwa kuwa alikiri kushiriki mauaji hayo na kuwataja washitakiwa wenzake hao saba.

Ilielezwa na mashahidi wa upande wa mashitaka kuwa katika mahojiano polisi wakati wa kuchukua maelezo yao ya onyo, washitakiwa wote walikiri kufanya mauaji hayo na washitakiwa wanne, mbali na maelezo walichukuliwa video.

Washitakiwa hao ni mshitakiwa wa kwanza, Erick Teete, wa pili, Fadhili Mohamed au Mushi, wa tatu, John Daniel na mshitakiwa wa 7, Robert Massawe au Kipara na katika kuthibitisha shitaka, Jamhuri iliita mashahidi 13 na kuwasilisha vielelezo 15.

Vielelezo vilivyowasilishwa kortini ni pamoja na maelezo ya onyo ya washitakiwa wote wanane, ripoti za uchunguzi wa miili ya marehemu (postmortem report) na baada ya kusomewa mashitaka yao, washitakiwa wote wanane waliyakanusha.

Ushahidi wa Jamhuri ulivyokuwa

Mmoja wa mashahidi ni aliyekuwa mkuu wa Upelelezi (OC-CID) wilaya ya Moshi, Elias Haway ambaye alieleza namna alivyopata taarifa za uwepo wa tukio hilo na baadaye Agosti 28, 2016 alipata taarifa mtuhumiwa mmoja yuko Arusha.

Alituma timu ya makachero ambao walifanikiwa kukamata baadhi ya washitakiwa ambao ni mshitakiwa wa 7 (Kipara), na mshitakiwa wa kwanza (Teete) ambao katika mahojiano na polisi walikiri kushiriki tukio hilo na kutaja washirika.

Katika ushahidi wake huo, shahidi huyo alieleza kuwa mshitakiwa Robert Massawe alimtaja Erick Tetee, Nassoro Nassoro, Juma Hamis na Ibra wakati Tetee waliwataja Massawe au Kipara, Nassoro Nassoro, Big na Ibrahim Mkindi.

Mashahidi wengine wanane ambao ni maofisa wa polisi, ushahidi wao ulikuwa hautofautiani na wa bosi wao na kwa sehemu kubwa walieleza walivyokagua eneo la tukio, kukamata washitakiwa na kuandika maelezo yao ya onyo.

Raia pekee waliotoa ushahidi wao ni Dk Patrick Amsi aliyefanya uchunguzi wa miili ya marehemu, Tom Swai aliyekuwa mtunza stoo Ahsante Tours na Gilbert Shangali aliyekuwa meneja walioeleza walivyokuta ofisi zao zimevunjwa.

Utetezi wa washitakiwa

Mshitakiwa wa kwanza, Eric Teete alikanusha mashitaka hayo akisema alikamatwa Agosti 25, 2016, alikamatwa kutokana na ugomvi uliotokea siku hiyo eneo la Ilboru kati yake na askari aitwaye Hamis aliyeahidi kumlipizia kisasi.

Alishangaa siku hiyo saa 5:00 usiku mlango ukigongwa na waliingia maofisa watano wa polisi ambao walimchukua hadi kituo cha Polisi Arusha ambapo siku iliyofuata alihamishiwa kituo kikuu cha Polisi Moshi na kushitakiwa kwa mauaji.

Mshitakiwa wa pili, Fadhil Mohamed, alidai alikamatwa na Polisi Jijini Arusha Agosti 26,2016 wakati akiuza viatu ambapo polisi walimshuku labda vimeibwa mahali, ndipo akakamatwa na kufungwa kitambaa cheusi usoni.

Anadai kilipofunguliwa, alijikuta yuko kituo kikuu cha Polisi Moshi ambapo alipelekwa katika chumba cha mateso na kuteswa na kulazimishwa kusaini karatasi alizoletewa na polisi na kama asingefanya hivyo wangemuua.

Mshitakiwa wa tatu, John Daniel alisema yeye alikamatwa Septemba 2, 2016 wakati anasafiri kutoka Arusha kwenda Moshi na polisi walipompekua walimkuta na msokoto mmoja wa bangi, alipelekwa chumba cha mateso na kuteswa.

Huko kama mshitakiwa mwenzake alitakiwa kusaini karatasi zilizoandikwa na alizisaini baada ya kudai kuteswa, huku mshitakiwa wa 4, Nassoro akidai alikwenda kituo cha Polisi Moshi kumdai koplo Charles nguo zake, akashangaa amekamatwa.

Kwa upande wake, mshitakiwa wa tano, Paschal Mushi alijitetea kuwa alikamatwa Agosti 22, 2016 huko Majengo akituhumiwa kuwa na mali ya wizi na alipopelekwa kituo kikuu mjini Moshi, alidai aliteswa na kutakiwa kusaini karatasi ambazo hakuzielewa.

Mshitakiwa wa sita, Ibrahim Mkindi yeye alidai kukamatwa Agosti 28, 2016 eneo la Kaloleni Moshi na kupelekwa katika chumba cha mateso ambapo kama wenzake, alitakiwa kusaini karatasi zenye maelezo na kudai kuwa alizisaini kutokana na kipigo.

Kwa upande wake, mshitakiwa wa saba, Robert Massawe alijitetea akidai kuwa alikamatwa Agosti 24, 2016 huko Arusha na kusafirishwa hadi Moshi na kupelekwa chumba cha mateso akitakiwa kusaini karatasi fulani na kudai alilazimika kuzisaini.

Mshitakiwa wa 8, Juma Ramadhan alidai Septemba 4, 2016 usiku wa manane alikamatwa na polisi nyumbani kwake akiwa na bangi ambapo alipelekwa chumba cha mateso na kudai kuteswa ili asaini karatasi fulani, na ilimlazimu kuzisaini.

Hukumu ya Jaji Kilimi

Katika hukumu yake hiyo jaji aliukataa ushahidi huo wa maelezo ya onyo ya washitakiwa na mikanda ya video iliyorekodiwa na maofisa wa Polisi akisema ushahidi wa namna hiyo ulitakiwa uungwe mkono na ushahidi huru.

“Nakubaliana na upande wa utetezi katika majumuisho yao ya mwisho kuwa hakuna shahidi hata mmoja aliyetoa ushahidi kwamba alishuhudia mauaji haya hivyo ushahidi wote wa kesi hii ni wa kimazingira,” alisema Jaji Kilimi.

Jaji Kilimi alisema maelezo ya onyo ya ungamo ya mshitakiwa mmoja kama yanamhusisha mshitakiwa mwingine hayawezi kuchukuliwa kuwa ni ushahidi umeungwa mkono lazima upatikane ushahidi mwingine unaounga mkono.

Ni kutokana na kutopatikana ushahidi huru wa kuunga mkono maelezo ya onyo ya washitakiwa na video walizorekodiwa, Jaji alisema upande wa ushahidi wa upande wa mashitaka, umeshindwa kuthibitisha shitaka hilo na kuacha mashaka.

MWANANCHI
Kwani hapa inakuwaje? ndiyo imeisha hivo au?maana wale walinzi ilithibitika wameuawa.Au wanatakiwa warudi wakawatafute wauaji upya. Sababu kusipokuwa na action yoyote kwa uzembe kama huu. Ni rahisi sana kwa police kuchukua rushwa kutoka kwa watuhumiwa na kupindisha ushahidi.On the other hand naona mhimili wa mahakama pia ulikuwa huru kutekeleza majukumu yake.

Hapa kuna mtu anaitwa DPP,yeye anahusika wapi?
 
Yan hapo walikamatwa bila ushahid wa kutosha walifosi tu wasaini jau sana

JUMBA LINALODAIWA NI LA 'MATESO' A.K.A MBAO FC

(Page 23 - 24)
......taken to Moshi central Police. He further said on 28/8/2016 he was taken to torture room where he was tortured and returned to lock up, the following day he was taken in the same room, then upon being scared to be tortured again, he did sign the document given to him without knowing what is inside.

In regard to sixth accused one Ibrahim Athuman Mkindi (DW6) defended by saying that he was arrested by police officers on 28/8/2016, at Kaloleni, Moshi town. Next day on 29/8/2016, he was sent to torturing room known as Mbao FC, and forced to sign a paper which he did not know what was written on it.

He further explained the bad relation with Isack Chaula a police officer whom he owes money after contract of payment his money breached.

Then it was the seventh accused one Robert John Massawe (DW7) who said that on 24/8/2016 at 20:00 hours, he was arrested by 8 police officers having canibias satiya (Bang!) in his bag, after arrest they sent him to kwanguneme Police Post Arusha, at about 21:00 he was transferred to Arusha Central Police.

On 26/8/2016 at 18:00 hours, he was transported to Moshi by Police officers whom he mentioned to be Afande Pessa, Haway and Derick. Upon arrival at Moshi at about 21:30, he was then taken to Mbao FC .......

Source : Republic vs Erick Willson Teete & Others (Criminal Session Case 44 of 2019) [2022] 64 (14 December 2022); | Tanzlii
 
Bro walinzi walijiua wenyewe?,
Kama wao si wauaji sasa tuoneshwe wauaji,
la sivyo tutatoa hukumu huku mtaani!!
Unafahamu kazi ya Mahakama?
Bro walinzi walijiua wenyewe?,
Kama wao si wauaji sasa tuoneshwe wauaji,
la sivyo tutatoa hukumu huku mtaani!!
Hakuna shaka, kua walinzi waliuwawa. nani aliwauwa ? huo ndio msingi wakesi yenyewe.
Kama umesoma Uzi wenyewe , umeona jinsi watuhumiwa walivyo kamatwa na kuteswa Ili wakiri kosa wenyewe.

Jaji hawezi kumfunga mtu kifungo Cha maisha au amhukumu kunyongwa bira ushahidi usio acha shaka eti , kwasababu watu wameuliwa.
Ni jeshi la Polisi ndio lenye kukurupuka na kukamatwa watu ovyo na kuwabambika kesi badra ya kutumia weredi wakamate waharifu wenyewe .
 
Mshtakiwa wa kwanza namfahamu aisee! Mama yake kasota sana. Alikuwa Tour guide wa Ashanti Tours! Hongera kwa kushinda
 
Polisi warudi field kuwasaka wahalifu ili kutenda haki kwa hao walinzi
Mkuu kesi ni sayansi.

Hayo majamaa ndiyo mauwaji menyewe, isipokuwa ushahidi umeacha mwanya kwa makusudi!

Ni weledi mdogo wa wapelelezi wa Polisi ama rushwa"kuburuza" ushahidi kwa kukusanya vielelezo dhaifu na kuacha vya muhimu,.
 
Lakini Kuna wawili wamekili kukutwa na bangi, inakuwaje,?
 
Lakini Kuna wawili wamekili kukutwa na bangi, inakuwaje,?
kukutwa na bangi huwezi hukumiwa kwa madawa ya kulevya wakati kesi ni ya mauaji labda wafunguliwe kesi nyingne ya madawa ya kulevya
 
ASILIMIA kubwa ya mawakili wa jamuhuri Ni vilaza, matokeo Yake ndo haya

ASILIMIA kubwa wanaajiliwa kwa maelekezo ya vimemo,kadi ya chama[emoji26]
 
Back
Top Bottom