Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 9,140
- 15,963
Wanufaika wa TASAF kutoka katika baadhi ya Kata za Machame Mashariki, pia baadhi ya kata zilizopo katika Wilaya ya Moshi na Moshi Vijijini Mkoani Kilimanjaro wamekosa malipo yao tangu kuanza kwa mwaka huu Januari hadi sasa Mei 2023.
Ndani ya hiyo kata hiyo kuna Kijiji kadhaa vikiwemo Narumu, Usari, Orori, Tela na Ulali.
Baadhi ya wanufaika hao wamesema kuwa mara ya mwisho kupata pesa yao ilikuwa mwezi wa kumi na mbili 2022, lakini hadi mwezi huu wa tano hawajapata malipo yoyote na kwamba wanaishi kwa tabu.
Wanufaika hao wamekuwa wakishurutishwa kuja na majembe kuchimba /kukarabati barabara na kwamba hadi wakamalishe kukarabati wa barabara ndipo watapata malipo yao.
Baadhi ya wazee na yatima wamekuwa wakipitia katika kipindi kigumu tangu kusitishwa kwa huduma hiyo mwishoni mwa mwaka jana hadi hivi sasa.
Helena Lelo ni mama wa watoto watatu ambae ni mnufaika wa mfuko huo anasema kuwa anapitia kipindi kigumu yeye na watoto wake kwa kuwa fedha hizo zilikuwa zinamsaidia kununua vifaa vya watoto shule pamoja na matumizi ya chakula nyumbani lakini leo hii wanaambiwa wakakarabati barabara za kijiji ndipo hela zitatoka lakini hadi sasa hakuna malipo yoyote yaliyotolewa.
Pia soma Simbachawene: Tunafuatilia madai ya wanufaika wa TASAF kutolipwa
Ndani ya hiyo kata hiyo kuna Kijiji kadhaa vikiwemo Narumu, Usari, Orori, Tela na Ulali.
Baadhi ya wanufaika hao wamesema kuwa mara ya mwisho kupata pesa yao ilikuwa mwezi wa kumi na mbili 2022, lakini hadi mwezi huu wa tano hawajapata malipo yoyote na kwamba wanaishi kwa tabu.
Wanufaika hao wamekuwa wakishurutishwa kuja na majembe kuchimba /kukarabati barabara na kwamba hadi wakamalishe kukarabati wa barabara ndipo watapata malipo yao.
Baadhi ya wazee na yatima wamekuwa wakipitia katika kipindi kigumu tangu kusitishwa kwa huduma hiyo mwishoni mwa mwaka jana hadi hivi sasa.
Helena Lelo ni mama wa watoto watatu ambae ni mnufaika wa mfuko huo anasema kuwa anapitia kipindi kigumu yeye na watoto wake kwa kuwa fedha hizo zilikuwa zinamsaidia kununua vifaa vya watoto shule pamoja na matumizi ya chakula nyumbani lakini leo hii wanaambiwa wakakarabati barabara za kijiji ndipo hela zitatoka lakini hadi sasa hakuna malipo yoyote yaliyotolewa.
Pia soma Simbachawene: Tunafuatilia madai ya wanufaika wa TASAF kutolipwa