[emoji23][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]Sasa hivi Mwamposa ametulia hotelini na mchepuko wake wanahesabu hela huku wachagga wanakodi mahema ya misiba. Kamatahii mutu. Fungia ndani. Ndalichako njoo kuna nwingine huku anahitaji ung'eng'e wako akalale ndani.
Kwanza wachaga hawakai mjini mpaka usiku. Wakishafunga maduka yao saa 12 jioni wanapanda zao milimani.Nahisi hao waliokufa ni raia wahamiaji kutoka mikoa mingine, mi siamini kama wachaga nao ni wajinga hivyo. ,😂😂😂😂
Poleni sana! Mungu awatie nguvuWapumzike kwa amani, niko njiani kuelekea msibani kuna mwenzetu kakanyagiwa huko!
Asante kwa marekebisho.Kwa kukosa maarifa
Sio kusoma maarifa.
Anyway huyo mwamposa ni kijana wa mzee wa upako ila sasa naona kamzidi kete hadi aliye muonyesha janja janja
Ila umaskini ni mbaaaya sana Hawa watu ni matapeli tu sema Imani nayo ngumu hadi mtu akuelewe kuhusu utapeli wao
Nyongeza_Wewe ni mkumbaff!! Mwamposa ni mungu? Eti wanamkosea mungu!!mtu anasemwa ili aache tabia mbaya ya wizi na ushirikina wewe unasema wanamkosea mungu? Haya sasa tamaa zake zimeshasababisha vifo,ila nasikia amelala sero,angebaki huko hadi angalau keshokutwa apandishwe kizimbani na kuhukumiwa nyundo kadhaa ingependeza zaidi.Aisee inakuwaje unanitukana, nimekukosea nini, na kama huamini si wewe, inakuwaje unanitukana? Bro tuheshimiane,
HAYO MAFUTA WANAYOGOMBANIA ETI YANA UPONYAJI WA MARADHI!! SASA CHA AJABU BADALA YA KUONDOA MARADHI YENYEWE YAMELETA UMAUTI.Waumini 18 wa Dini ya Kikristo wamefariki dunia usiku huu mjini Moshi, wakati wakikanyagana kugombea kukanyaga mafuta ya upako katika kongamano la kidini la Mtume Boniface Mwamposa, DC wa Moshi Kippi Warioba amethibitisha
Updates: 00:45
Idadi ya watu waliopoteza maisha kwa kukanyagana imefikia 20 na uenda idadi hiyo ikaongezeka Mkuu wilaya amethibitisha.
UPDATES:
Watu 20 wamefariki dunia leo jioni Jumamosi Februari 1,2020 katika ibada ya mahuburi wakati wa harakati za kukanyaga mafuta ya upako kwenye kongamano la Mtume Boniface Mwamposa 'Buldoza' katika Viwanja vya Majengo Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.
Inadaiwa kuwa waumini hao walikumbwa na maafa hayo wakati wakikanyagana kwa ajili ya kugombania kukanyaga mafuta yaliyomwagwa na mhubiri huyo yakidaiwa kuwa na upako.
Inaelezwa kuwa watu zaidi ya 40 walikanyagana katika harakati za kugombania mafuta ya upako na kukimbizwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi.
Idadi ya waliokufa huenda ikaongezeka kwa kuwa hakuna taarifa ya ujumla ya majeruhi waliopelekwa katika vituo vya afya vya jirani pamoja na Hospitali ya Rufaa ya KCMC.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba amelithibitisha leo saa 5:00 usiku kuwa taarifa za awali waumini 20 wamekufa lakini akasisitiza hizo ni taarifa za awali.
“Taarifa za awali tulizonazo ni kuwa ni waumini 20 wamepoteza maisha lakini tunaendelea kufuatilia maeneo mengine ya zahanati, vituo vya afya na hospitali kama kuna watu walipelekwa huko,” amesema Kippi.
Taarifa zinaeleza kuwa baada ya tukio hilo Mhubiri huyo alielekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akitaka kuondoka, lakini ndege aliyokuwa amepangwa kuondoka nayo ilichelewa (delayed) na ndipo Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro lilipomtia mbaroni uwanjani hapo.
Apostle Boniface Mwamposa a.k.a Bulldozer
Chanzo: Mwananchi
Kwanza wachaga hawakai mjini mpaka usiku. Wakishafunga maduka yao saa 12 jioni wanapanda zao milimani.
P1Hahahahha.Wanataka baraka za miteremko. Baraka hazikuji bila kufanya kazi na katika mazingira yanayofavor Baraka.
Juzi mkurugenzi wa babati mji alianza kufunga makanisa yasiyosajiliwa watanzania hawakumuelewa.sasa huko Moshi watu20 wamekufa kwa uzembe na ujinga wa mtu moja.Waumini 18 wa Dini ya Kikristo wamefariki dunia usiku huu mjini Moshi, wakati wakikanyagana kugombea kukanyaga mafuta ya upako katika kongamano la kidini la Mtume Boniface Mwamposa, DC wa Moshi Kippi Warioba amethibitisha
Updates: 00:45
Idadi ya watu waliopoteza maisha kwa kukanyagana imefikia 20 na uenda idadi hiyo ikaongezeka Mkuu wilaya amethibitisha.
UPDATES:
Watu 20 wamefariki dunia leo jioni Jumamosi Februari 1,2020 katika ibada ya mahuburi wakati wa harakati za kukanyaga mafuta ya upako kwenye kongamano la Mtume Boniface Mwamposa 'Buldoza' katika Viwanja vya Majengo Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.
Inadaiwa kuwa waumini hao walikumbwa na maafa hayo wakati wakikanyagana kwa ajili ya kugombania kukanyaga mafuta yaliyomwagwa na mhubiri huyo yakidaiwa kuwa na upako.
Inaelezwa kuwa watu zaidi ya 40 walikanyagana katika harakati za kugombania mafuta ya upako na kukimbizwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi.
Idadi ya waliokufa huenda ikaongezeka kwa kuwa hakuna taarifa ya ujumla ya majeruhi waliopelekwa katika vituo vya afya vya jirani pamoja na Hospitali ya Rufaa ya KCMC.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba amelithibitisha leo saa 5:00 usiku kuwa taarifa za awali waumini 20 wamekufa lakini akasisitiza hizo ni taarifa za awali.
“Taarifa za awali tulizonazo ni kuwa ni waumini 20 wamepoteza maisha lakini tunaendelea kufuatilia maeneo mengine ya zahanati, vituo vya afya na hospitali kama kuna watu walipelekwa huko,” amesema Kippi.
Taarifa zinaeleza kuwa baada ya tukio hilo Mhubiri huyo alielekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akitaka kuondoka, lakini ndege aliyokuwa amepangwa kuondoka nayo ilichelewa (delayed) na ndipo Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro lilipomtia mbaroni uwanjani hapo.
Apostle Boniface Mwamposa a.k.a Bulldozer
Chanzo: Mwananchi
Hii ni hatari kwa vizazi vijavyoWatu wetu wamegeuzwa kuwa waabudu viumbe badala ya muumba .Hii ni aina ya shirikina kuamini kitu kitakupa baraka au utukufu fulani alionao mtu utakusaidia wewe, Na hawa wachungaji wapotezaji huwaaminisha watu mambo ili kujikweza wenyewe au kujipatia manufaa ya kipato.
Dini zimegeuzwa DILI.
Sent using Jamii Forums mobile app
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Umaskini ni mbaya sana. Huyo mchungaji akamatwe haraka sana.
Damu ya Yesu, jina la Yesu na neno lake Mungu pekee ndizo silaha tosha kupitia maombi ya kufunga, usiku wa manane na kusali mara kwa mara kwa imani lakini mengineyo yote ni utapeli mtupu.wale wakristo mnisaidiye kuna mahala kwenye biblia yesu aliwapaka mafuta watu,kuuza vitambaa,maji,chumvi na kupokea bahasha zenye pesa?je pia alipofanya miujiza alijitangaza?
Umesoma mpaka mwisho au umekoment tu mkuuHuyo mchungaji hata hakamatwi? Kama hayupo kizuizini mpaka sasa basi serikali imeoza, ikafukiwe tu tuendelee na maisha yetu.
Kweli!hali ngumu ya maisha jamani duuuuh
Duh Mwamposa kawapelekea jam Moshi huko
Any way lbda atawafufua
Ova
Sent using Jamii Forums mobile app