#COVID19 Most Mutated COVID-19 Variant yet found in Tanzania travelers

#COVID19 Most Mutated COVID-19 Variant yet found in Tanzania travelers

Ingekua ni hivo mlivokaririshwa kuwa korona inaua sana watu,hospitali za dar es salaam zingekua zimezidiwa maana kila siku maelfu wapo uwanja wa mkapa bila barakoa wanaangalia mpira.
Yanayoandikwa mitandaoni ukija mtaani hayapo kabisa

Kumbe kina Nkapa, Maalim, Kijazi, jiwe, Dr. Mpango ni wa mitandaoni?
 
Hawa wapumbuva washaanza kuleta ujinga wao
Hakuna lockdown hapa tz peleken ujinga wenu huko
Kama ni kufa acha tufe
Matapeli wamkubwa nyie waongo wazandiki
Tz hakuna korona kwanza

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
🤣🤣🤣🤣yaani hapo ungekuta upinzani ndio unaongoza nchi ungekuta tupo ndani lockdown toka mwaka Jana korona ilipoanza mpk leo yaani hali ingekua ngumu kupita maelezo.
 
Kuwa na aina mpya ya mlolongo wa virus wa Corona sio issue...

Issue ni je kirusi hicho kipya ni hatari kiasi gani?
Jambo ambalo bado hao wanaosema wameking'amua hawajawa na majawabu...

Si ajabu ni variant mpya ambayo ukiipata inasaidia mwili kutengeneza kinga na usiweze pata Covid tena...
 
Una uthibitisho kua ni korona?au na wewe umesikia taarifa za vijiweni?acha kufuata wajinga wajinga huko Twitter

Za kuambiwa changanya na za kwako:

IMG_20210318_132000_124.jpg


Hiyo miamba ilikuwa buheri wa afya.

Mmoja wao push-up sana majukwaani achilia mbali nyakua nyakua.

Unaambiwa alikuwa na afya hati hati leo?

Hao mtu wote wenye afya na nafasi zao ni deportivo la coruna peke yake mwenye ujasiri wa kuangusha miamba kama hiyo kwenye span ya mwaka mmoja robo tatu yao ndani ya mwezi mmoja!

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Wiki iliyopita mwanangu karudi toka shule anachemka nikampa panadol akapoa usiku alirudia tena kuchemka nikampa tena panadol. Asubuhi imefika nikampeleka hosptal wakakuta hana ugonjwa ila wanasema dam imechafuka wakanipa dawa. Narudi nyumbani nakuta na dada yake nae anachemka kumpeleka nae wanasema mkojo ni mchafu wakanipa dawa.....

Nimewapa dawa hakuna iliyosaidia wakaanza mafua na kukohoa na mm nikaanza kusikia viungo vyote vya mwili vinauma. Sasa familia nzima ikawa inaumwa ebwana usiku kucha watu ni kukohoa nikaona subiri niache hizi dawa nipige nyungu kidogo ikasaidia nikaanza kutumia pia chumvi ya magadi na ndimu mpaka leo wamebaki na kubanja tu ila km ndo Corona jamani tuambiane tu ukweli km kinga zetu ni ndogo si ndo ilikuwa bye bye.
 
Kuna jamaa mmoja hapa JF nilimwambia Tanzania inaweza kutoa mutation mpya ya kirusi, akawa anabisha saaana kwa ubishi wa kibongo wa ilimradi kubisha tu

Natamani niuone ule uzi nimuoneshe hii habari.
Kwani mkuu ni conditions zipi ambazo zinaweza sababisha strain ya kirusi ika'undergo mutation hasa zinazohusiana na mazingira ya hapa kwetu Tanzania yalivyo?
 
Za kuambiwa changanya na za kwako:

View attachment 1735257

Hiyo miamba ilikuwa buheri wa afya.

Mmoja wao push-up sana majukwaani achilia mbali nyakua nyakua.

Unaambiwa alikuwa na afya hati hati leo?

Hao mtu wote wenye afya na nafasi zao ni deportivo la coruna peke yake mwenye ujasiri wa kuangusha miamba kama hiyo kwenye span ya mwaka mmoja robot tatu yao ndani ya mwezi mmoja!

Au nasema uongo ndugu zangu?
Sio korona ni magonjwa mengine ya kibinadamu tu,hata wewe unaweza ukaumwa kichwa tu ukafa mtaani kwako wakaanza kudai korona imekuua
 
Uzuri ni kua, hiki kirusi kikikupata kama upo healthy kinakutingisha kidogo tu kama wiki mbili kisha unakaa sawa,

Kwa Tanzania corona ni old school song.
Kweli kabisa hata haiongelewi watu wanaendela na life,watz tumeshindikana .Leo mzee anazikwa nimekuta sehemu watu wanaendelea kugonga vyombo na mbuzi kwa sana
 
Kwani mkuu ni conditions zipi ambazo zinaweza sababisha strain ya kirusi ika'undergo mutation hasa zinazohusiana na mazingira ya hapa kwetu Tanzania yalivyo?
1.No testing.
2.No isolation
3. No vaccine

Hizi mutations zinatokea popote, lakini, kwenye testing, isolation and vaccination, zinakuwa contained.

Kwetu hatuna testing, hatuna isolation, hatuna vaccination.

Tunatengeneza mutations ambazo zinaachwa ku evolve rampantly.
 
Mama Samia atakataa vipi wakati mumewe anafanya kazi na mabeberu
 
Back
Top Bottom