BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa Omary Mgumba, ghala lilikuwa na mizigo ya Mamlaka ya Mapato (TRA) ikiwemo Vitenge vilivyokamatwa kwa Magendo baro 370 pamoja na Sukari, Mafuta ya Kula, Baiskeli na Pikipiki
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa, Fatuma Ngenya amesema wamefanikiwa kuudhibiti Moto ulianza saa 8 usiku eneo hilo na uchunguzi wa chanzo chake umeanza.
==================
Moto ambao chanzo chake bado hakijafahamika umezuka usiku wa kuamkia leo kwenye ghala la Bandari ya Tanga ambalo lilikuwa limehifadhi mizigo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga vikiwemo vitenge vya magendo baro 370, sukari, mafuta ya kupikia, pikipiki na baiskeli ambavyo ni mali ya Wafanyabiashara ambao wameshindwa kulipia ushuru na vyote vimeteketea kwa moto.
Mkuu wa wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amezungumza leo asubuhi wakati moto ukiendelea kuzimwa ambapo amesema tukio hilo limetokea majira ya saa nane usiku ambapo ghala hilo lilikuwa linahifadhi vitu mbalimbali vya magendo ikiwemo mizigo ya walioshindwa kulipa ushuru.
Mgumba amesema, hadi sasa mkazo wao mkubwa ni kuhakikisha moto unazimwa kabla ya uchunguzi kuanza ili kubaini chanzo cha moto huo.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Tanga, Fatuma Ngenya amesema hadi sasa wamefanikiwa kuudhibiti moto huo.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa, Fatuma Ngenya amesema wamefanikiwa kuudhibiti Moto ulianza saa 8 usiku eneo hilo na uchunguzi wa chanzo chake umeanza.
==================
Moto ambao chanzo chake bado hakijafahamika umezuka usiku wa kuamkia leo kwenye ghala la Bandari ya Tanga ambalo lilikuwa limehifadhi mizigo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga vikiwemo vitenge vya magendo baro 370, sukari, mafuta ya kupikia, pikipiki na baiskeli ambavyo ni mali ya Wafanyabiashara ambao wameshindwa kulipia ushuru na vyote vimeteketea kwa moto.
Mkuu wa wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amezungumza leo asubuhi wakati moto ukiendelea kuzimwa ambapo amesema tukio hilo limetokea majira ya saa nane usiku ambapo ghala hilo lilikuwa linahifadhi vitu mbalimbali vya magendo ikiwemo mizigo ya walioshindwa kulipa ushuru.
Mgumba amesema, hadi sasa mkazo wao mkubwa ni kuhakikisha moto unazimwa kabla ya uchunguzi kuanza ili kubaini chanzo cha moto huo.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Tanga, Fatuma Ngenya amesema hadi sasa wamefanikiwa kuudhibiti moto huo.