Moto wateketeza ghala lenye mizigo ya magendo na waliokwepa ushuru Tanga

Moto wateketeza ghala lenye mizigo ya magendo na waliokwepa ushuru Tanga

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa Omary Mgumba, ghala lilikuwa na mizigo ya Mamlaka ya Mapato (TRA) ikiwemo Vitenge vilivyokamatwa kwa Magendo baro 370 pamoja na Sukari, Mafuta ya Kula, Baiskeli na Pikipiki

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa, Fatuma Ngenya amesema wamefanikiwa kuudhibiti Moto ulianza saa 8 usiku eneo hilo na uchunguzi wa chanzo chake umeanza.

==================

Moto ambao chanzo chake bado hakijafahamika umezuka usiku wa kuamkia leo kwenye ghala la Bandari ya Tanga ambalo lilikuwa limehifadhi mizigo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga vikiwemo vitenge vya magendo baro 370, sukari, mafuta ya kupikia, pikipiki na baiskeli ambavyo ni mali ya Wafanyabiashara ambao wameshindwa kulipia ushuru na vyote vimeteketea kwa moto.

Mkuu wa wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amezungumza leo asubuhi wakati moto ukiendelea kuzimwa ambapo amesema tukio hilo limetokea majira ya saa nane usiku ambapo ghala hilo lilikuwa linahifadhi vitu mbalimbali vya magendo ikiwemo mizigo ya walioshindwa kulipa ushuru.

Mgumba amesema, hadi sasa mkazo wao mkubwa ni kuhakikisha moto unazimwa kabla ya uchunguzi kuanza ili kubaini chanzo cha moto huo.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Tanga, Fatuma Ngenya amesema hadi sasa wamefanikiwa kuudhibiti moto huo.
 
Taarifa kutoka Tanga inaonyesha kwamba , ghala la kuhifadhia mizigo ya Wafanyabiashara iliyokamatwa kwa makosa mbalimbali limeteketea kwa moto , huku kukiwa na mali kadhaa ndani yake , yakiwemo marobota 370 ya vitenge , mafuta ya kula na vitu vingine .

Natoa wito kwa Wahusika kuchunguza chanzo cha moto huo na wachunguze pia kama mizigo tajwa ilikuwemo ndani ya ghala hilo wakati wa moto huo au ilifaulishwa .
 
Moja kwa Moja kwenye mada..

Naona Sarakasi za Viongozi kudaidia wafanyabiashara kukwepa Kodi zimeanza..

Kuna Taarifa kutoka Tanga kwamba Ghala lililokuwa na bidhaa zilizokamatwa kwa kukwepa Kodi kimeungua moto..

Kwa haraka haraka hii ni Hujuma kwa Nchi, sio sawa Viongozi wa Serikali wakikaa kimya na kufumbia macho mambo haya.

Hii italeta picha mbaya kwamba kumbe ufisadi umerudi. Serikali chukueni hatua kali kwa viongozi wa Bandari Tanga na viongozi wa TRA Tanga na wengine wote waliohusika..

Hii sio sawa 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20221023-133009.png
    Screenshot_20221023-133009.png
    131.8 KB · Views: 8
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa Omary Mgumba, ghala lilikuwa na mizigo ya Mamlaka ya Mapato (TRA) ikiwemo Vitenge vilivyokamatwa kwa Magendo baro 370 pamoja na Sukari, Mafuta ya Kula, Baiskeli na Pikipiki

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa, Fatuma Ngenya amesema wamefanikiwa kuudhibiti Moto ulianza saa 8 usiku eneo hilo na uchunguzi wa chanzo chake umeanza.

==================

Moto ambao chanzo chake bado hakijafahamika umezuka usiku wa kuamkia leo kwenye ghala la Bandari ya Tanga ambalo lilikuwa limehifadhi mizigo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga vikiwemo vitenge vya magendo baro 370, sukari, mafuta ya kupikia, pikipiki na baiskeli ambavyo ni mali ya Wafanyabiashara ambao wameshindwa kulipia ushuru na vyote vimeteketea kwa moto.

Mkuu wa wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amezungumza leo asubuhi wakati moto ukiendelea kuzimwa ambapo amesema tukio hilo limetokea majira ya saa nane usiku ambapo ghala hilo lilikuwa linahifadhi vitu mbalimbali vya magendo ikiwemo mizigo ya walioshindwa kulipa ushuru.

Mgumba amesema, hadi sasa mkazo wao mkubwa ni kuhakikisha moto unazimwa kabla ya uchunguzi kuanza ili kubaini chanzo cha moto huo.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Tanga, Fatuma Ngenya amesema hadi sasa wamefanikiwa kuudhibiti moto huo.
Huu ni uhujumu uchumi na viongozi wa TRA na Bandari wakamatwe..

Hapo Takukuru hakuna kitu watafanya ila watasubiria maelekezo ya Waziri Mkuu,bure kabisa.
 
Moja kwa Moja kwenye mada..

Naona Sarakasi za Viongozi kudaidia wafanyabiashara kukwepa Kodi zimeanza..

Kuna Taarifa kutoka Tanga kwamba Ghala lililokuwa na bidhaa zilizokamatwa kwa kukwepa Kodi kimeungua moto..

Kwa haraka haraka hii ni Hujuma kwa Nchi,sio sawa Viongozi wa Serikali wakikaa kimya na kufumbia macho mambo haya..

Hii italeta picha mbaya kwamba kumbe ufisadi umerudi.. Serikali chukueni hatua kali kwa viongozi wa Bandari Tanga na viongozi wa TRA Tanga na wengine wote waliohusika..

Hii sio sawa 👇
eti kumbe ufisadi umeanza kurudi!!kwani toka uhuru ni kipindi kipi huo ufisadi ulishawahi kuisha??
 
Back
Top Bottom