Motra the future na Diss Track dhidi ya Kikosi Kazi awaita kikosi kazi WEUPE

Ugumu uko wapi?

Au unazungumzia katika perspective ya mashabiki kwamba itaonekana kua jamaa kakamiwa kwasababu ya wingi na sio uwezo?
hivi kweli kundi zima linaweza kwenda studio kutoa diss track ya kumjibu mtu mmoja ambae ameingilia beef yao??
kuimba diss zaidi ya moja sio jambo jepesi especially opponent wako akiwa hajajibu.
 
hivi kweli kundi zima linaweza kwenda studio kutoa diss track ya kumjibu mtu mmoja ambae ameingilia beef yao??
kuimba diss zaidi ya moja sio jambo jepesi especially opponent wako akiwa hajajibu.
Ukisha zingua hupaswi kumchagulia mtu silaha

Umenipiga kofi afu unastuka kuona nanyanyuka na shoka unaanza kulalamika "eti mbona mimi nimekupiga kofi tu afu we unalipisha na shoka hiyo sio sawa"

Mimi ndo nimeona shoka ndio silaha ya kutuliza hasira zangu kwa ulichokifanya

Motra kadisi kundi, na ndio maana kuna lines nyingi akitajja straight jina la kikosi kazi. Sasa kama kaweza kuwa diss wote kwa bars zaidi ya 40 kwanini nayeye asijibiwe bars 40 hizo hizo na mahasimu wake kwa track moja?
 
Wordplay on both tracks is on another level ila Cortez katisha zaidi IMO. He went in. Kaitendea haki beat ya Renegade.

Lyrically wana kilinge/SSK ni wakali kushinda weusi no doubt ila bado wanaonekana undergrounds hadi leo, hii chuki yao towards weusi sounds more like wivu. Naona wanawaingiza na kina Lunya, Rapcha humo wakati madogo wanapambana tu na hali zao but ndo hip hop we're here for it tupate ladha tofauti.
 
Uko deep sana, ila hiyo SSK (nadhani ulikusudia kikosi kazi) ni old group iliyo consist member watatu tu (p mawenge, wakazi na zaiid)
 
Nafikiri kamgusia pia Nikki hapo upande WA one ...alipoongelea ukileta "ubishi".........lkn pia umesikia mex Cortez na yy katoa amkia
 
Hao KIKOSI kazi wanatafuta namna ya kurudi kwenye game maana bongo makundi ya hip-hop ni mawili tu.
WEUSI waliwapotezea Sasa wanatafuta namna ya kurudi. Bila WEUSI kuwadiss Hawa jamaa watapotea kwenye ramani ya mziki.
Motraa Chali wa nyumbani kabisa kawadiss ..wakijibu Kama kundi watakuwa ni WAPUMBAVU.
P mawenge anasanuka mapema anaona Hana maisha maana machizi wakina ZaiiDyao na mansuli washapotea kwenye game. Uno bado anajikongoja, Nikk mbishi hamuna anayemuelewa na mipasho yake. Stereo Yuko busy na kazi za kuajiriwa ..hivyo hili kundi halieleweki malengo yake ni yapi yani lipo lipo tu. Songa na yeye maji kupwaa maji kujaa.

Bila WEUSI kuwadiss Basi tusahau uwepo wa Hawa jamaa Kama kundi. Kila mtu ataanza kula kona yake.
 
Sasa huyo motra huoni kama diss yake dhidi ya kikosi kazi inaleta picha mpya kuonekana kama ametumwa na hao weusi?

Sasa nani kati ya hayo makundi mawili ambaye anafosi kiki kwa mwenzake?

Au hujui ile diss ya kikosi kazi kwa weusi ilikua ni reply baada ya weusi kuwachana tamaduni?

Hii sisi kwa wadau wa hip hop tunaiona kama challenge ambayo inayoleta ushindani na kuoneshana uwezo, wala sio kitu personally.

Kwanza ishu ya kikosi kazi kujibu hiyo diss sidhani hata kama ipo kwenye project yao, ila sio kwamba hawamjibu eti kwasababu ni mtu na sio kundi.
 
Wewe unawatetea tamaduni lakini ukikaa na kuangalia mziki wao una future yeyote? Miaka mingapi wako kwenye game wameishia kuwaimbia masela Kama nyie ambao mnatoa support mitandaoni kwenye real hampo.
WEUSI hawakuanza kuwadiss hao jamaa. Chokochoko zilikuwa tangu kitambo tu tamaduni walikuwa wanadai WEUSI wanabebwa na Media. Ndio WEUSI wakaamua kuwalipua bas majamaa yakapanick balaa πŸ˜‚πŸ˜‚ bila ile diss track ya WEUSI hakuna mtu mwenye attention nao ni nyie wachache tu ambao hata kazi zao hamnunui na kwenye media hamrequest ngoma zao. Ndio maana mtu Kama Nash Mc kajikataa zake, Dizasta na yeye yuko kivyake. ..kundi Lina wasanii nane siju kumi ..tangu lini kundi kubwa ivyo likadumu mda mrefu? Hawana maisha marefu Hawa jamaa watapoteana tu
 
Watu wa arusha hawajawahi mkubali nikki, ila wapo wanaojua hip hop culture wanamuelewa
Nikk ni MC mkali Nina album zake kadhaa naskizaga ni hatari tupu Ila anaharibu sana ana kipaji Ila anajiona yeye ndio Bora zaid na hiyo ndiyo ujinga wake. Amekuwa na mipasho mingi Hadi Roma kamchana afanye mziki muda unakwenda na wakati wake utapita.

NB: Ni ngumu Sana kwa watu wa A Town kuyielewa hip-hop ya Dar kwa sababu ni vitu viwili tofauti kabisa.
Hip-hop ya Dar ni soft mnoo..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…