Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Madiliko ya katiba sio kitu ambacho hufanywa bila ma referendum and other consultative procedures. Na wazo lakusema kwamba mtu ikifika 2010 na tukabadili katiba CCM haitashinda uchaguzi, that is foolishness. I see no other party that is capable of running the country. Not for another 10-15 years. Wapinzani imewachukua election ya 95,2000,2005 (3) kurealize that they should be focusing on parliamentary elections, getting more seats and enough political experience in the eyes of the people then eventually wagombee Urais... It was obvious from the onset so the fact that they are sooo slow not to have seen it goes to show that they wont really be any better..

Mapinduzi yakimawazo nakisiasa yanachuku muda jamani, haka kanchi hakana ata 50 years. We are ayoung nation.. surely if we build on what we have taratibu, tutafikia point ambapo tutakua na vyama ambavyo vinaweza kupeana challenge. Lakini ata iweje hilo haliwezi kutokea 2010 na anaesema hivyo ni muongo.

Asante kwa majibu yako. Katiba iliyopo inaipa kipaumbele CCM kushinda katika uchaguzi. Katiba inatakiwa ibadilishwe ili kukidhi vyama vyote na iende na wakati. Kubadilisha katiba automatically hakutaifanya CCM ishindwe katika Uchaguzi lakini kutaweka demokrasia huru na pevu kwa watanzania.

Unapozungumzia experience ya kisiasa sijui una maana gani. Kwani hata viongozi wengi wa vyama vya upinzani wamekuwa katika siasa kwa muda mrefu kama hao wa CCM. Usiwe na fikra duni (Umangi meza) kwamba hakuna mtu anayeweza kutawala vyema Tanzania kutoka vyama vya upinzani ama kutoka nje ya CCM.
Kama iliwezekana Malawi na Zambia, itashindikanaje Tanzania?
 
Mabadiliko ya Katiba ni muhimu bila kujali uchaguzi ujao wa 2010. Mchakato wa kuanza kupata Katiba mpya iliyoandaliwa na wananchi waTanzania na inayotosha mahitaji ya wakati tuliopo ni vyema kuanza kufanyiwa kazi sasa.

Nia ya kuandaa Katiba mpya si kwasababu ya uchaguzi ujao tu. Ila ni kwa ajili ya kuweka sawa vipengele ambavyo havina maslahi kwa Taifa pamoja na kuweka usawa kwa watu wote. Vile vile itaondoa viraka visivyoshabihiana vilivyopo kwenye Katiba yetu pamoja na kutoa nguvu zenye uwiano kati ya Rais, Bunge, Mahakama na wananchi.

Uchaguzi ujao au mwingine wowote utafaidika na Katiba endapo itakuwa imekamilika (si lazima iwe imekamilika wakati wa uchaguzi ujao 2010). Katiba ni mwelekezo wa maisha ya Mtanzania, ni lazima iundwe na waTanzania wengi iwezekanavyo, na iundwe sasa.
 
Kumradhi wakuu, tumeunganisha mada iliyoanzishwa leo na ile ya mwaka 2006 ili kuweza kuleta mtiririko mzuri kwa wanaotaka kujua katiba yetu ilivyo na mapendekezo ya watanzania juu ya mabadiliko yepi yanahitajika.

Ni matumaini yetu mjadala utaweza kuendelea kwa uzuri zaidi
 
Kenya wamedai mabadiliko ya Katiba na matunda yameonekana ,na zaidi tunataka kubadili mtawala Sultani CCM akae pembeni akijiandaa kujibu kesi ambazo zinaweza kuchukua miaka mingi maana wapo wezi kibao wamejificha chini ya mwavuli wa Katiba iliyopo.

Sultani CCM ukimletea mambo ya katiba basi utaona wafuasi wake wanavyotetea kuwa itachukua miaka mingi na kunahitajika mambo mengi ,yaani longolongo kibao za kukatisha tamaa, lakini tunawambia kuwa upinzani utadai mabadiliko ya Katiba kwa nguvu zao zote,

Katiba na tume ya Uchaguzi ni lazima vibadilishwe ,tuseme katiba itachukua miaka hamsini ili kutimia kubadilishwa na kupatikana katiba mpya ,je hili la tume ya Uchaguzi,siku zote kunaundwa tume haifiki hata wiki na inafanya kazi na kutoa ripoto ndani ya miezi pengine isiyozidi mitatu ,sasa hapa napo mbona mnakuwa wagumu pana kitu gani ?
 
Ningependa kuuliza:

SEHEMU YA PILI
MALENGO MUHIMU NA MISINGI YA MWELEKEO
WA SHUGHULI ZA SERIKALI


6. Katika Sehemu hii ya Sura hii, isipokuwa kama maelezo
yahitaji vinginevyo, neno "Serikali" maana yake ni pamoja na
Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Serikali za mitaa na pia mtu anayetekeleza madaraka
au mamlaka yoyote kwa niaba ya Serikali yoyote.

7.-(1) Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya (2), Serikali,
vyombo vyake vyote na watu wote au mamlaka yoyote yenye
kutekeleza madaraka ya utawala, madaraka ya kutunga sheria
au madaraka ya utoaji haki, watakuwa na jukumu na wajibu wa
kuzingatia, kutia maanani na kutekeleza masharti yote ya
Sehemu hii ya Sura hii.

(2) Masharti ya Sehemu hii ya Sura hii hayatatiliwa nguvu ya
kisheria na Mahakama yoyote
. Mahakama yoyote nchini
haitakuwa na uwezo wa kuamua juu ya suala kama kutenda au
kukosa kutenda jambo kwa mtu au mahakama yoyote, au kama
sheria, au hukumu yoyote, inaambatana na masharti ya
Sehemu hii ya Sura hii.


8.-(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata
misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -

(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali
itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa
wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;

(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;

(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;

(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao
kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.

(2) Muundo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar, au wa chochote kati ya vyombo
vyake na uendeshaji wa shughuli zake, utatekelezwa kwa
kuzingatia umoja wa Jamhuri ya Muungano na haja ya kukuza
umoja wa kitaifa na kudumisha heshima ya Taifa.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

9. Lengo la Katiba hii ni kuwezesha ujenzi wa Jamhuri ya
Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au wa
chochote kati ya vyombo vyake na udugu na amani kutokana na
kufuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, amabyo inasisitiza
utekelezaji wa misingi ya kijamaa kwa kuzingatia mazingira
yaliyomo katika Jamhuri ya Muungano. Kwa hiyo, Mamlaka ya
Nchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kuelekeza sera na
shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha-

(a) kwamba utu na haki nyinginezo zote za binadamu
zinaheshimiwa na kuthaminiwa;

(b) kwamba sheria za nchi zinalindwa na kutekelezwa;

(c) kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia
ambazo zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa
unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa
manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia
mtu kumyonya mtu mwingine;

(d) kwamba maendeleo ya uchumi wa Taifa yanakuzwa
na kupangwa kwa ulinganifu na kwa pamoja;

(e) kwamba kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi
anafanya kazi, na kazi maana yake ni shughuli
yoyote ya halali inayompatia mtu riziki yake;

(f) kwamba heshima ya binadamu inahifadhiwa na
kudumishwa kwa kufuata Kanuni za Tangazo la
Dunia kuhusu Haki za Binadamu;

(g) kwamba Serikali na vyombo vyake vyote vya umma
vinatoa nafasi zilizo sawa kwa raia wote, wake kwa
waume, bila ya kujali rangi, kabila, dini au hali ya
mtu;

(h) kwamba aina zote za dhuluma, vitisho, ubaguzi,
rushwa, uonevu au upendeleo zinaondolewa nchini;

(i) kwamba matumizi ya utajiri wa Taifa yanatilia mkazo
maendeleo ya wananchi na hasa zaidi
yanaelekezwa kwenye jitihada ya kuondosha
umaskini, ujinga na maradhi;

(j) kwamba shughuli za uchumi haziendeshwi kwa njia
zinazoweza kusababisha ulimbikizaji wa mali au njia
kuu za uchumi katika mamlaka ya watu wachache
binafsi;

(k) kwamba nchi inatawaliwa kwa kufuata misingi ya
demokrasia na ujamaa.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

10. [Ibara ya 10 ya Katiba imefutwa na Sheria Na.4 ya
1992].

11.-(1) Mamlaka ya Nchi itaweka utaratibu unaofaa kwa ajili
ya kufanikisha utekelezaji wa haki ya mtu kufanya kazi, haki ya
kujipatia elimu na haki ya kupata msaada kutoka kwa jamii
wakati wa uzee, maradhi au hali ya ulemavu, na katika hali
nyinginezo za mtu kuwa hajiwezi. Na bila kuathiri haki hizo,
Mamlaka ya Nchii itaweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba
kila mtu anaishi kwa jasho lake.
(2) Kila mtu anayo haki ya kujielimisha, na kila raia
atakuwa huru kutafuta elimu katika fani anayopenda hadi kufikia
upeo wowote kulingana na stahili na uwezo wake.
(3) Serikali itafanya jitihada kuhakikisha kwamba watu
wote wanapata fursa sawa na za kutosha kuwawezesha kupata
elimu na mafunzo ya ufundi katika ngazi zote za shule na vyuo
vinginevyo vya mafunzo.
Ibara ya 7(2)...ina maana gani?
 
KATIBA ni msingi mkuu wa uendeshaji wa nchi na hii ni sheria mama katika nchi au jumuiya yoyote, kwa kawaida sheria nyingi za nchi zinatungwa kwa mujibu wa katiba. Wapo wanaoitafsiri sheria kama mkataba kati ya watawala na watawaliwa, kwa hiyo katiba ni nyaraka muhimu inayotoa dira ya nchi kwa kuamsha mamlaka ya nchi na vyombo vingine vya kuendesha nchi.

Katiba za nchi nyingi zinazoendelea zinahusiana na nchi za kikoloni kwa karibu sana, vivyo hivyo Katiba ya Tanzania. Baada ya Ujerumani kushindwa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Tanganyika kama ilivyojulikana wakati huo, iliwekwa chini ya usimamizi wa ushirika wa mataifa na baadaye kama mdhamini chini ya Umoja wa Mataifa.

Historia ya Katiba ya Tanzania
Katiba ya kwanza ya Tanzania ilijulikana kama Katiba ya Uhuru ya mwaka 1961 (Independence Constitution).
Hii ni Katiba iliyodumu kwa mwaka mmoja tu, yaani kuanzia mwaka 1961 hadi mwaka 1962, ambapo Tanzania ilipata katiba mpya, iliyojulikana kama Katiba ya Jamhuri ya mwaka 1962.

Hii ndiyo Katiba iliyotambua Tanganyika kama Jamhuri, vilevile ilipunguza kwa kiasi kikubwa madaraka ya Bunge kama yalivyotolewa na katiba ya uhuru. Mnamo mwaka 1964 Tanganyika na Zanzibar ziliungana na kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwaka mmoja baadaye, yaani mwaka 1965, nchi ilipata katiba mpya iliyotambulika kama katiba ya muda ya mwaka 1965 (Interim Constitution 1965). Lengo na dhumuni ya katiba hii ilikuwa ni kuongoza kwa muda tu na kuipisha katiba ya kudumu.

Hata hivyo, kinyume na madhumuni hayo, katiba hii ilidumu kwa muda mrefu zaidi, yaani miaka kumi na mbili, mpaka mwaka 1977.

Mwaka huo wa 1977 ndipo Tanzania ilipopata katiba ya kudumu. Hii ndiyo inayoitwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, iliyotungwa na Bunge maalumu la kutunga katiba.
Katiba hiyo ilitungwa na kamati ileile iliyotumika kuunda katiba ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kama ilivyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano Machi 16 mwaka 1977, iliyooongozwa na hayati Thabit Kombo.
Tarehe hiyo hiyo ndiyo rais aliteua Bunge la Katiba kwa madhumuni ya kujadili na kupitisha Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Kwa hakika, zoezi zima la kuijadili na kuipitisha katiba hii halikuhusisha wala hakukuwa na majadiliano na wananchi.

Haki za binadamu katika katiba hii
Haki za binadamu ni kitu muhimu sana kwa maendeleo ya wananchi na ustawi wao na taifa kwa ujumla.
Hata hivyo, kwa wananchi walio wengi wa nchi zinazoendelea Tanzania ikiwamo, suala la haki za binadamu kuwapo katika katiba si suala la msingi na halipewi uzito unaostahili.
Hivyo basi, ni muhimu sana kwa suala hili kujadiliwa kwa sababu ni vigumu kwa wananchi kudai haki zao endapo hazikuanishwa katika katiba na sheria za nchi.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano ilipitia mabadiliko mbalimbali, miongoni mwa mabadiliko hayo ni yale yaliyofanywa na sheria namba 8 ya mwaka 1975, ambayo yalikigawia chama tawala madaraka makubwa sana juu ya serikali.
Hakukuwa na mfumo wa kudhibitiana kwa dhati kati ya vyombo vikuu vya dola na hii ilileta mkanganyiko mkubwa sana, kwani watu walewale waliofanya maamuzi katika chama ndio haohao waliokuja kuhakikisha maamuzi hayo yanatekelezwa upande wa serikali.

Mkanganyiko huu na mengineyo ulisababisha mahitaji makubwa ya tamko la haki za binadamu katika katiba yetu.

Hivyo ni sahihi kusema kwamba katiba na sheria za nchi hazitoi haki hizi bali inazitambua tu.
Wakati huo, katiba wala sheria za Tanzania hazikuzitambua haki hizi, bali kilichofanyika ilikuwa ni kuziweka haki hizo katika utangulizi/ dibaji (preamble) ya katiba hiyo.

Kisheria, jambo hili lilikuwa na athari hasi, kwani kisheria sehemu hiyo si sehemu ya katiba au sheria yoyote ile.
Kwa maana hiyo, mwananchi yeyote ambaye haki yake ingekiukwa na chombo chochote cha dola, au mtu yeyote asingeweza kudai haki yake hiyo/hizo katika chombo cha kudai haki kama mahakama.
Kwa takriban miaka mingi tangu Tanganyika (Tanzania Bara) ipate uhuru mwaka 1961 sehemu inayotambua haki hizo haikuwepo.

Kupitia mabadiliko ya katiba ya mwaka 1984 yaliyofanyika chini ya sheria namba 15 ya mwaka 1985, kwa mara ya kwanza Haki za Binadamu ziliingizwa rasmi katika katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Haya yalikuwa ni matunda ya wadau wa sekta mbalimbali kama wahisani, mashirika yasiyo ya kiserikali na jumuiya ya kimataifa.

Haki hizi hata hivyo zilianza kutumika mwaka 1988 na katika katiba hii haki na wajibu wa wananchi uko katika sehemu ya tatu ya katiba.

Sehemu hii inaanzia ibara ya 12 hadi ibara ya 29. Miongoni mwa haki hizi ni pamoja na haki ya kuwa hai, haki ya uhuru wa mawazo, haki ya kufanya kazi, haki ya uhuru wa mtu kwenda atakapo na haki ya usawa.
Vilevile wajibu kwa wananchi upande mwingine umewekwa ili mwananchi aweze kupata haki yake, kwa maana hiyo ni kwamba Hakuna haki pasipo na wajibu.

Kwa mfano, katika ibara ya 25 ya katiba hii kila mwananchi amepewa wajibu wa kushiriki kwa kujituma kwa uaminifu na katika kazi halali na ya uzalishaji mali. Hata hivyo, kwa mujibu wa ibara ya 30 ya katiba hii, kuna mipaka kwa haki na uhuru ambazo katiba imezitambua, miongoni mwa mipaka hiyo ni pale haki hizi katika utekelezaji wake zitakapoingilia uhuru na haki ya mtu mwingine au kama itaingilia masilahi ya umma.

Hata hivyo, neno: Masilahi ya umma halijatafsiriwa na mara kadhaa linaweza kutumiwa kwa maana pana, ikiwa pamoja na kuhalalisha matendo ya ukiukwaji wa haki za binadamu.


News Archives - The Free Media of 𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀
 
Wakuu heshima mbele!

Kumekuwa na malalamiko ya mara kwa mara kuhusu relevance ya katiba iliyopo sasa na mahitaji ya sasa baada ya muda mrefu wa mabadiliko makubwa katika nyanja mbalimbali (New world order). Kwa upande wetu sisi wapinzani tungependa katiba mpya. Chama tawala wangependa kurekebisha katiba iliyopo. Naomba tujadili hili kwa kuwa ni la manufaa kwa taifa zima. Ningefurahi kama majadiliano yangelenga zaidi maeneo yafuatayo :

1/.Uzalendo wa waliotunga katiba iliyopo sasa na uwezekano wa katiba ile kuwa na true values za mtu wa kawaida

2/.Hali ya uzalendo kwa sasa kwa ujumla kwa watanzania wote ndani ya chama tawala, upinzani na watu wasio na itikadi za kisiasa

3/.Uwezekano wa katiba mpya kuathiriwa na hali ya uzalendo uliopo sasa positively or negatively.

4/.Tofauti kati ya mtazamo wa kitaaluma ambao hulenga zaidi katika kujenga juu ya misingi ya waliotangulia na hili suala la katiba.

Natumaini mawazo yetu sote juu ya hili yatalisaidia taifa kwa ujumla.
 
Naomba kufahamishwa katiba yetu inaongea nini ktk uteuzi wa waziri mkuu. Je anateuliwa na Rais ama ni chama ndo kinamteua baada ya kupata viti vya bunge vya kutosha. Na kama anateuliwa na Rais je ikitokea Rais katoka chama kingine na chama chenye viti vingi ni kingine je Rais ata apoint waziri mkuu wa chama kingine.?

Nauliza hivi maana sasa nimelekeza mashambulizi yangu ktk Wikipedia.Org kwa kurekebisha mambo kule, kwa maana nimechoka na wazungu kutuandikia mambo yao. Kuna sehemu nimekuta wanasema tuna university mbili ila nimesharekebisha japo si kwa usahihi sana.

Watanzania naomba tuwe wazalendo kwa kutoa taarifa muafaka hasa ktk hizi mitandao, maana wenzetu ndo source zao za habari.
 
Ipo pia kwenye jukwaa la sheria hapa hapa JF.. Wakati mwingine ni vizuri kutafuta majibu mwenyewe hasa kama ni rahisi kupatikana.
 
Naomba kufahamishwa katiba yetu inaongea nini ktk uteuzi wa waziri mkuu. Je anateuliwa na Rais ama ni chama ndo kinamteua baada ya kupata viti vya bunge vya kutosha. Na kama anateuliwa na Rais je ikitokea Rais katoka chama kingine na chama chenye viti vingi ni kingine je Rais ata apoint waziri mkuu wa chama kingine.?

Nauliza hivi maana sasa nimelekeza mashambulizi yangu ktk Wikipedia.Org kwa kurekebisha mambo kule, kwa maana nimechoka na wazungu kutuandikia mambo yao. Kuna sehemu nimekuta wanasema tuna university mbili ila nimesharekebisha japo si kwa usahihi sana.

Watanzania naomba tuwe wazalendo kwa kutoa taarifa muafaka hasa ktk hizi mitandao, maana wenzetu ndo source zao za habari.

Katiba ya Tanzania inasema wazi kuwa;

Waziri Mkuu wa Tanzania lazima awe Mbunge wa kuchaguliwa toka jimboni;kwa maana hiyo Wabunge wa viti maalum na wa kuteuliwa WAMEPOTEZA SIFA kuwa PM wa Tanzania!
 
MkamaP
Ikisemwa kuwa tunahitaji katiba mpya haieleweki kwenye masikio ya watawala wetu.
Lakini kuna mambo mengi sana yatatutatiza siku sisi m wakipoteza uhalali wa kututawala tena.
Watawala wetu wanafahamu jambo hili na wanajifanya wataendelea kututawala milele, hizi ndoto siku zikikoma tumeingia kwenye mgogoro mkubwa.

Kuna maswali kama hayo unayouliza mengi tu, na hayana majibu mbali na kuambiwa kuwa katiba yetu haina matatizo.
 
MkamaP
Ikisemwa kuwa tunahitaji katiba mpya haieleweki kwenye masikio ya watawala wetu.
Lakini kuna mambo mengi sana yatatutatiza siku sisi m wakipoteza uhalali wa kututawala tena.
Watawala wetu wanafahamu jambo hili na wanajifanya wataendelea kututawala milele, hizi ndoto siku zikikoma tumeingia kwenye mgogoro mkubwa.
Kuna maswali kama hayo unayouliza mengi tu, na hayana majibu mbali na kuambiwa kuwa katiba yetu haina matatizo.

Mkuu
Wananchi ndo wakulaumiwa, wananchi wakiipa kura upinzani 90% na ccm 10% nafikiri wataiba wee mpaka watashindwa kuiba kura na hatimaye upinzani kushika hatamu. Sijasoma katiba hasa kwenye hiyo kipengele sijui inasema je?
 
Naomba kufahamishwa katiba yetu inaongea nini ktk uteuzi wa waziri mkuu. Je anateuliwa na Rais ama ni chama ndo kinamteua baada ya kupata viti vya bunge vya kutosha. Na kama anateuliwa na Rais je ikitokea Rais katoka chama kingine na chama chenye viti vingi ni kingine je Rais ata apoint waziri mkuu wa chama kingine.?

Nauliza hivi maana sasa nimelekeza mashambulizi yangu ktk Wikipedia.Org kwa kurekebisha mambo kule, kwa maana nimechoka na wazungu kutuandikia mambo yao. Kuna sehemu nimekuta wanasema tuna university mbili ila nimesharekebisha japo si kwa usahihi sana.

Watanzania naomba tuwe wazalendo kwa kutoa taarifa muafaka hasa ktk hizi mitandao, maana wenzetu ndo source zao za habari.
Kuhusu vyuo vikuu nenda www.tcu.go.tz
 
Chama chenye wabunge wengi ndicho kitaunda serikali. Waziri mkuu atatoka kwenye chama chenye wabunge wengi. Kwetu tumezoea Rais ndiye anayeteua kwa vile kwa upande mwingine yy ni mwenyekiti wa chama twawala.
 
Back
Top Bottom