Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Mahakama iliwahi kusema katika kesi ya Director of Public Prosecutions v. Daudi Pete [1993] TLR 22 (CA) katika ukurasa wa 23 kama ifuatavyo: "As the Constitution of the United Republic of Tanzania is established in the Kiswahili language, the controlling version in interpreting the Constitution is the Kiswahili and not the English version."
Kwa hiyo kama mnatafsiri Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, msitumie version ya Kiingereza, tumieni ya Kiswahili!

Asante Buchanan. Hata kwenye rufaa ya kesi kuhusu mgombea binafsi, jaji mkuu amesisitiza hivyo hivyo.
 
Asante sana ndugu Bucha na nanihii kwa ufafafunuzi nzuri kuhusu lugha ya katiba.

hata hivyo baadaye niliamua kuwa kuwa itakuwa ni vizuri tukaziangalia zote mvbili hasa ukizingatia kuwa lugha zote ni official languages hapa kwetu. Nitakuwa naleta version zote mbili kwa kila kifungu nitakachokuwa naongelea; itasaidia pia kuona hata mapungufu katika tranalation baina ya lugha hizo.

Sawa mkuu. Pia nimependa huu mpangilio wa kuweka kifungu kimoja kimoja. Nashauri ujitahidi kuweka sehemu fupi fupi ili walio wengi tuweze kufuatilia. Wengi wetu ni wavivu wa kusoma vitu virefu virefu. Ila hii ni kitu muhimu na ingeleta tija kama tutaweza kujadili katiba yote.

Ubarikiwe na Bwana... (DC).
 
Kichunguu, nimependa wazo lako na kitu kizuri sana kujadili katiba ambayo ndiyo siyo tu sheria mama bali mwongozo wetu sote. Ila kwenye upande wa poll, maelezo yake yana utata kwani mtu anayeingia mara moja hawezi kujua kama unalenga huu mjadala wa humu jamvini bali mijadala ya kawaidia mitaani.

Kuhusu mapungufu uliyoonesha kwenye utangulizi, nakubaliana na wewe kabisa.
1. Tz siyo nchi ya kijamaa ki-uhalisia. Kilichoandikwa kwenye katiba siyo kinachoendelea. Kwa hiyo tunahitaji kubadili hiyo dhani ili tusionekane tunafanya mzaha na katiba.
2. Bunge letu lina wabunge wasiochaguliwa na wananchi. Hivyo ama katiba ibadilishwe ili tuwape nafasi au tuwaondoe.
3. Hiyo omission ya neno circular state ni hatari sana. Kwa hiyo ni muhimu ama katiba mpya itungwe kwa kiswahili ili baadaye itafsiriwe ka lugha nyingine au watu wa kutafsiri wawe makini sana. Hii dhana muhimu na kwa hiyo haikutakiwa kuachwa kwenye toleo la kiswahili!

Kwa vile dibaji hii inetangaza msingi wa Katiba yote, je itakuwa ni sahihi kuwa vifungu vyote huko mbele ambavyo vitapingana na dibaji hii viondolewe? Nitavionyesha kila tutakapovifikia. Utashangaa kuona kuwa kuna vifungu vilikuwa viantumbukizwa kwenye katiba bila mpangilio wowote.
 
Kwa vile dibaji hii inetangaza msingi wa Katiba yote, je itakuwa ni sahihi kuwa vifungu vyote huko mbele ambavyo vitapingana na dibaji hii viondolewe? Nitavionyesha kila tutakapovifikia. Utashangaa kuona kuwa kuna vifungu vilikuwa viantumbukizwa kwenye katiba bila mpangilio wowote.

Uko sahihi mkuu. Nadhani kitu chochote kinachopingana na dibaji kinakuwa kama kiko out of intention. Kama watu wako makini hiyo inatakiwa kuepukwa. Na kwa hiyo vifungu ambavyo vinapingana na dhana nzima ya katiba yenyewe (kama ilivyooneshwa kwenye dibaji) kwa maoni yangu vinajiua vyenyewe. Mimi ni mbumbu wa haya mambo na kwa hiyo haya ni maoni ya mtu ambaye yuko naive; ngoja tusubiri maoni ya wataalamu ili tujue wanasemaje!
 
Mahakama iliwahi kusema katika kesi ya Director of Public Prosecutions v. Daudi Pete [1993] TLR 22 (CA) katika ukurasa wa 23 kama ifuatavyo: "As the Constitution of the United Republic of Tanzania is established in the Kiswahili language, the controlling version in interpreting the Constitution is the Kiswahili and not the English version."
Kwa hiyo kama mnatafsiri Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, msitumie version ya Kiingereza, tumieni ya Kiswahili!
Buchanan Lakini mbona wasomi wetu majaji(Learned judges)wa mahakama zetu wanatoa hukumu zao kwa kiingereza? bila shaka watatumia version za kiingereza kama reference!
 
Kwa vile dibaji hii inetangaza msingi wa Katiba yote, je itakuwa ni sahihi kuwa vifungu vyote huko mbele ambavyo vitapingana na dibaji hii viondolewe? Nitavionyesha kila tutakapovifikia. Utashangaa kuona kuwa kuna vifungu vilikuwa viantumbukizwa kwenye katiba bila mpangilio wowote.

Nadhani swali la kujiuliza ni je dibaji/preamble ya katiba ina nguvu ya kisheria kama ibara za katiba? Ingawa dibaji inatoa mtizamo wa kijumla wa madhumuni ya watunzi wa katiba, sidhani kama ina nguvu ya kisheria kuzidi ile ya ibara za katiba!
 
Mwalimu alikazania sana maisha ya watanzania yawe juu ya misingi ya ujamaa na kujitegemea. Alipong'atuka aliondoka na wazo hilo, likaja azimio la Zanzibar ambalo lilishabikia adui wa ujamaa, ndio maana JKN alisema anaposoma azimio la Arusha la ujamaa na kujitegemea hajaona wapi alipokosea. Dhamira ni safi lakini wasaidizi wake hawakuwa naye sambamba. Alipoondoka tu wakaonyesha makucha yao na kugeuza kibao. Alikataliwa na watu wake aliowaamini na kuwapigia debe (Binadamu hana wema usimwone kucheka). Bora Kambona alimwonyesha waziwazi mkuu wake kwamba hakubaliani na sera hiyo.

Katika jitihada (kinafiki labda) za kumuenzi Mwalimu, Katiba haikarafatiwi ila inakarabatiwa kwa kupenyezwa vionjo vinavyohama kiujanjaujanza sera za ujamaa na kuingiza ubepari rasmi kwa azimio la Zanzibar. Piga ua huwezi kukubaliwa kliondoa Ujamaa kwa unafiki huohuo kwamba tunawaenzi waasisi, lakini kinawekwa kionjo kingine kinachokinzana na ujamaa lakini vinakaa kwenye katiba moja.

Kwa hali ilivyo sasa, wapinzani waliomo ndani ya CCM na walio nje ya CCM wanasema kweli kwamba katiba iandikwe upya kulingana na hali halisi ya sasa ya soko huria tulilojiamulia kwa azimio la Zanzibar. Lakini ni nani atakayesema akapewa nafasi ya kueleweka? Limeulizwa swali hilo bungeni mara kwa mara, lakini majibu yake ni fyatu tu. Hata anayejibu anajibu kijeuri akijua hutamfanya chochote maana yeye kashika mpini. Ndio maana unaambiwa piga ua CCM lazima idumu kwa gharama yoyote ili asije mwenye sera tofauti akafukua hata yale yanayosemwa ndani chumbani yakatoka nje tukatafutana ubaya bure.

Katiba ingefaa kufundishwa kama somo tangia shule za misingi ili kila mtu ajue inavyomwathiri maishani kwake kila siku. Lakini umesikia wapi hapa Bongo mtu akaambiwa haki zake? Ukichokonoa ndipo unaelezwa kwamba sawa lakini...... mambo jambo....

pengine ni wazo zuri kujadili kwa njia mbalimbali ikiwamo hii ja JF pia
 
Asante sana ndugu Bucha na nanihii kwa ufafafunuzi nzuri kuhusu lugha ya katiba.

hata hivyo baadaye niliamua kuwa kuwa itakuwa ni vizuri tukaziangalia zote mvbili hasa ukizingatia kuwa lugha zote ni official languages hapa kwetu. Nitakuwa naleta version zote mbili kwa kila kifungu nitakachokuwa naongelea; itasaidia pia kuona hata mapungufu katika tranalation baina ya lugha hizo.

Naomba ututajie hiyo Kesi ambapo Mahakama ya Rufani ilikuja kusema tena tutumie lugha zote mbili.
 
Naomba ututajie hiyo Kesi ambapo Mahakama ya Rufani ilikuja kusema tena tutumie lugha zote mbili.

Wanasheria bwana, ... wana mambo yao!! Mimi nilidhani mleta hoja alikuwa analenga kutumia lugha mbili hapa kwenye mjadala na siyo kwenye sheria katika utaratibu wa kutafsi katiba. Mimi nadhani tutumie lugha zote mbili hapa ili tueleweshane vizuri. Halafu pale panapohitaji msisitizo wa kisheria mnaweza kuingia kwenye 18 zenu! Pia ningeomba mpunguze nukuu za hukumu ili sisi wengine tusianze kupata allergy!
 
Hebu sasa tuangalie Sura ya Kwanza, Sehemu ya Kwanza, Ibara 1-3


KISWAHILI

attachment.php






KIINGEREZA
attachment.php



chap1pat1-1-3.JPG
sura1sehemu1-1-3.JPG



Maoni Yangu:

Kosa moja kubwa ninaloona hapa ni lile la kudai kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa. Kama nilivyosema huko nyuma, ningependa kuona neno hilo linaondoloewa kwenye katib


Hiyo aya ya 2 (2) ina makosa ya kimantiki. Ni kifungu kinachoonekana klilipenyezwa katika katiba bila kufikiriwa vya kutosha. Mpaka hapao, katiba haijaongelea kama Jamhuri itakuwa serikali yenye muundo upi, na mkuu wa serikali atajulikanaje, imekurupuka na kusema Serikali ya Mpinduzi ya zanzibar, ....Rais na atagawa jamhuri katika wilaya na mikoa na .... rais wa Zanzibar . Mpaka sasa hatujia katiba iapotumia maneno hayo ni makosa kwa vile haijayatafsiri. Rais anaweza kuwa rais wa kampuni au Rais wa chama au vinginevyo vyo vyote. Serikali ya mapinduzi pia haijaujulikana ni kitu gani kwa msoma katiba. Kwa hiyo kama nilivyosema ni kifungu hiki kimemwagwa hapo bila mantiki yoyote.

Tafsiri ya kiingereza imerudia tena kuonyesha kuwa Tanzania haifungamani na dini yoyote lakini tafsiri ya kiswahili iko kimya kuhusu hilo.

Mwisho, hiyo aya ya 3(2) nayo ninaona kama ni kifungu kilichopenyezwa hapo kwenye maelezo ya muundo wa nchi kabla hata hatuaelezwa muundo wa utawala; kwa mtazamo wangu nakiona pia ni kifungu kilichopenyezwa pale bila mantiki.
 
Buchanan Lakini mbona wasomi wetu majaji(Learned judges)wa mahakama zetu wanatoa hukumu zao kwa kiingereza? bila shaka watatumia version za kiingereza kama reference!

Majaji wetu wanafikiria kwa Kiswahili halafu wanaandika kwa Kiingereza, lakini wanatumia Version ya Kiswahili ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 katika tafsiri. Vile vile wanawasikiliza parties wa kesi ambao wanaongea kwa lugha ya Kiswahili halafu wao huandika kwa Kiingereza! Very interesting!
 
Wanasheria bwana, ... wana mambo yao!! Mimi nilidhani mleta hoja alikuwa analenga kutumia lugha mbili hapa kwenye mjadala na siyo kwenye sheria katika utaratibu wa kutafsi katiba. Mimi nadhani tutumie lugha zote mbili hapa ili tueleweshane vizuri. Halafu pale panapohitaji msisitizo wa kisheria mnaweza kuingia kwenye 18 zenu! Pia ningeomba mpunguze nukuu za hukumu ili sisi wengine tusianze kupata allergy!

Nilikuwa sijajua kama nukuu za hukumu zinaleta allergy!
 
Kichuguu, kwani katibu huwa haianzi na tafsiri ya maneno muhimu tunayotegemea kukutana nayo kwenye document yenyewe? Kama hiyo tafsiri ingekuwepo basi haya mapungufu mengine (aya ya 2) yesingejitokeza!
 
Nadhani swali la kujiuliza ni je dibaji/preamble ya katiba ina nguvu ya kisheria kama ibara za katiba? Ingawa dibaji inatoa mtizamo wa kijumla wa madhumuni ya watunzi wa katiba, sidhani kama ina nguvu ya kisheria kuzidi ile ya ibara za katiba!

Ninaloongelea ni consistency ya katiba; inakuwa ni vibaya kuwa na mambo yanayopingana ndani ya katiba moja. Katiba ni document ambayo inatakiwa ieleweke kwa raia wote kirahisi. Ingawa preamble haina nguvu ya kisheria, ndiyo hiyo vile vile inayotoa sababu ya kuwepo kwa katiba hiyo, na ndiyo hiyo inayosainiwa na wapitisha katiba ile.

Kwa hiyo preamble ni lazima iwe reflection kamili ya vifungu vilivyomo kwenye katiba hiyo
 
THE D.P.P VS. DAUDI PETE
CRIMINAL APPEAL NO. 28 OF 1990
IN THE COURT OF APPEAL OF TANZANIA

NYALALI, C. J.
MAKAME, J. A.
RAMADHANI, J. A

''But a word caution first. Since our Constitution is established in the Kiswahili language, we must constantly bear in mind that the controlling version is the Kiswahili one and not the English version.''
 
Asante sana ndugu Bucha na nanihii kwa ufafafunuzi nzuri kuhusu lugha ya katiba.

hata hivyo baadaye niliamua kuwa kuwa itakuwa ni vizuri tukaziangalia zote mvbili hasa ukizingatia kuwa lugha zote ni official languages hapa kwetu. Nitakuwa naleta version zote mbili kwa kila kifungu nitakachokuwa naongelea; itasaidia pia kuona hata mapungufu katika tranalation baina ya lugha hizo.
Naomba ututajie hiyo Kesi ambapo Mahakama ya Rufani ilikuja kusema tena tutumie lugha zote mbili.

Unasoma post zote vizuri kweli wewe?
 
Kichuguu, kwani katibu huwa haianzi na tafsiri ya maneno muhimu tunayotegemea kukutana nayo kwenye document yenyewe? Kama hiyo tafsi basi haya mapungufu mengine (aya ya 2) yesingejitokeza!

Katiba nyingi nilizowahi kusoma huwa hazitoi definition ye terminologies kama inavyofanyika kwenye sheria na mikataba; katiba ya Tanzania pia haina definition yoyote.
 
Katiba nyingi nilizowahi kusoma huwa hazitoi definition ye terminologies kama inavyofanyika kwenye sheria na mikataba; katiba ya Tanzania pia haina definition yoyote.

Ibara ya 151 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 ina tafsiri (definitions) mbalimbali kama ifuatavyo:

151. Ufafanuzi Sheria Na. 14 ya 1979 ib. 13; 1 ya 1980 ib. 17; 15 ya 1984 ib. 52 na 53; 4 ya 1992 ib. 38; 3 ya 2000 ib. 19; T.S. Na. 133 la 2001
(1) Katika Katiba hii, ila iwapo maelezo yahitaji vinginevyo–
"amri ya jeshi" maana yake ni sheria au amri iliyotolewa kwa mujibu wa sheria, ya kusimamia nidhamu katika jeshi;
"askari" likitumika kuhusiana na jeshi lolote maana yake ni pamoja na askari yeyote ambaye kwa mujibu wa amri ya jeshi hilo ni mtu anayewajibika kinidhamu;
"Baraza la Wawakilishi" maana yake ni Baraza la Wawakilishi la Zanzibar lililotajwa katika ibara ya 106 ya Katiba hii na linalotekeleza madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii na Katiba ya Zanzibar, 1984;
"Bunge" maana yake ni Bunge la Jamhuri ya Muungano lililotajwa katika ibara ya 62 ya Katiba hii;
"Chama cha Siasa" maana yake ni chama cha siasa kilichoandikishwa kikamilifu kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992; *

"Idara ya Mahakama" maana yake ni kama ilivyofafanuliwa katika ibara ndogo ya (1) ya ibara ya 116 ya Katiba hii;
"Idara ya Mahakama ya Zanzibar" maana yake ni Idara ya Mahakama inayojumlisha mahakama zote ambazo ziko katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
"Jaji Mkuu" maana yake ni Jaji Mkuu wa Mahakama ya Rufani aliyetajwa katika ibara ndogo ya (1) ya ibara ya 118 ya Katiba hii ambaye ameteuliwa kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2) ya ibara hiyo ya 118 au iwapo Jaji Mkuu hayupo au anashindwa kutekeleza kazi zake kwa sababu yoyote, Kaimu Jaji Mkuu aliyeteuliwa kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (4) ya ibara hiyo ya 118 ya Katiba hii, na kama Kaimu Jaji Mkuu naye hayupo au anashindwa kutekeleza kazi za Jaji Mkuu, Jaji wa Mahakama ya Rufani aliyepo kazini kwa wakati huo na ambaye yuko kwenye daraja la juu zaidi la madaraka kupita Majaji wote wa Rufani waliopo;
"Jaji Mkuu wa Zanzibar" maana yake ni Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar ambaye, kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar 1984, ndiye Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Zanzibar;

"Jeshi" maana yake ni jeshi lolote kati ya majeshi ya ulinzi na ni pamoja na jeshi lolote jingine lilioundwa na Katiba hii au kwa mujibu wa sheria na linalotawaliwa kwa amri ya jeshi;
"Jumuiya ya Madola" maana yake ni jumuiya ambayo wanachama wake ni Jamhuri ya Muungano, Uingereza na kila nchi ambayo iliwahi kutawaliwa na Uingereza;
"kiapo" maana yake itabidi ifahamike kwa maana ya kawaida ya neno hilo na ni pamoja na tamko rasmi la namna yoyote linaloruhusiwa kisheria kutumiwa badala ya kiapo;
"kiapo cha uaminifu" maana yake ni kiapo cha kuwa mwaminifu kwa Nchi na kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;

"Maadili ya Kazi ya Jaji" maana yake ni masharti ya kimaadili yanayoongoza mwenendo wa watu wafanyao kazi ya Jaji au ya Hakimu;
"madaraka ya kazi katika utumishi wa Umma Jamhuri ya Muungano" maana yake itabidi ifahamike kwa mujibu wa maana ya kawaida na maneno hayo na ni pamoja na utumishi katika Majeshi ya Ulinzi ya Jamhuri ya Muungano na katika Jeshi la Polisi au jeshi linginelo lilioundwa kwa mujibu wa Sheria;
"mahakama" maana yake ni mahakama yoyote yenye mamlaka katika Jamhuri ya Muungano isipokuwa mahakama iliyoundwa kwa amri ya jeshi; lakini kwa ajili ya ibara ya 13, ya 14 na ya 15 za Katiba hii, itakuwa ni pamoja na mahakama iliyoundwa kwa amri ya jeshi;
"Mahakama Kuu" maana yake ni Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano au Mahakama Kuu ya Zanzibar;
"Mambo ya Muungano" maana yake ni mambo yote ya umma ambayo yametajwa na ibara ya 4 ya Katiba hii kuwa ni Mambo ya Muungano;

"Mamlaka ya Nchi" ni pamoja na Serikali na Bunge la Jamhuri ya Muungano, pamoja na Serikali na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar;
"Mwanasheria Mkuu" maana yake ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano aliyetajwa katika ibara ya 59;
"Serikali" maana yake ni pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au Halmashauri ya Wilaya au ya Mji, na pia mtu yeyote anayetekeleza madaraka au mamlaka yoyote kwa niaba ya Serikali au Halmashauri;
"Serikali za Mitaa" maana yake ni vyombo vya kiserikali vilivyoundwa kwa mujibu wa ibara ya 145 ya Katiba hii kwa madhumuni ya kutekeleza madaraka ya umma;
"Tanzania Bara" maana yake ni eneo lote la Jamhuri ya Muungnao ambalo zamani lilikuwa eneo la Jamhuri ya Tanganyika;

"Tanzania Zanzibar" maana yake ni eneo lote la Jamhuri ya Muungano ambalo zamani lilikuwa eneo la Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na ambalo kabla ya Sheria hii kutungwa liliitwa Tanzania Visiwani;
"Uchaguzi Mkuu" au "uchaguzi unaofanywa na wananchi" maana yake ni uchaguzi wa Rais na uchaguzi wa Wabunge wanaowakilisha wilaya za uchaguzi unaofanywa baada ya Bunge kuvunjwa;
"Ujamaa" au "Ujamaa na Kujitegemea" maana yake ni misingi ya maisha ya jamii ya kujenga Taifa linalozingatia demokrasia, kujitegemea, uhuru, haki, usawa, udugu na umoja wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano;

"Waziri" maana yake ni Mbunge aliyekabidhiwa madaraka ya kazi ya Waziri, isipokuwa Naibu Waziri, na maana hiyo itatumika pia kwa Makamu wote wa Rais;
"Zanzibar" maana yake ni sawa na maana ya Tanzania Zanzibar.

Sijui mwenzetu ulitaka kuwe na definition zipi!
 
Ibara ya 151 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 ina tafsiri (definitions) mbalimbali kama ifuatavyo:

151. Ufafanuzi Sheria Na. 14 ya 1979 ib. 13; 1 ya 1980 ib. 17; 15 ya 1984 ib. 52 na 53; 4 ya 1992 ib. 38; 3 ya 2000 ib. 19; T.S. Na. 133 la 2001
(1) Katika Katiba hii, ila iwapo maelezo yahitaji vinginevyo–
"amri ya jeshi" maana yake ni sheria au amri iliyotolewa kwa mujibu wa sheria, ya kusimamia nidhamu katika jeshi;
"askari" likitumika kuhusiana na jeshi lolote maana yake ni pamoja na askari yeyote ambaye kwa mujibu wa amri ya jeshi hilo ni mtu anayewajibika kinidhamu;
"Baraza la Wawakilishi" maana yake ni Baraza la Wawakilishi la Zanzibar lililotajwa katika ibara ya 106 ya Katiba hii na linalotekeleza madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii na Katiba ya Zanzibar, 1984;
"Bunge" maana yake ni Bunge la Jamhuri ya Muungano lililotajwa katika ibara ya 62 ya Katiba hii;
"Chama cha Siasa" maana yake ni chama cha siasa kilichoandikishwa kikamilifu kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992; *
"Idara ya Mahakama" maana yake ni kama ilivyofafanuliwa katika ibara ndogo ya (1) ya ibara ya 116 ya Katiba hii;
"Idara ya Mahakama ya Zanzibar" maana yake ni Idara ya Mahakama inayojumlisha mahakama zote ambazo ziko katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
"Jaji Mkuu" maana yake ni Jaji Mkuu wa Mahakama ya Rufani aliyetajwa katika ibara ndogo ya (1) ya ibara ya 118 ya Katiba hii ambaye ameteuliwa kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (2) ya ibara hiyo ya 118 au iwapo Jaji Mkuu hayupo au anashindwa kutekeleza kazi zake kwa sababu yoyote, Kaimu Jaji Mkuu aliyeteuliwa kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (4) ya ibara hiyo ya 118 ya Katiba hii, na kama Kaimu Jaji Mkuu naye hayupo au anashindwa kutekeleza kazi za Jaji Mkuu, Jaji wa Mahakama ya Rufani aliyepo kazini kwa wakati huo na ambaye yuko kwenye daraja la juu zaidi la madaraka kupita Majaji wote wa Rufani waliopo;
"Jaji Mkuu wa Zanzibar" maana yake ni Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar ambaye, kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar 1984, ndiye Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Zanzibar;
"Jeshi" maana yake ni jeshi lolote kati ya majeshi ya ulinzi na ni pamoja na jeshi lolote jingine lilioundwa na Katiba hii au kwa mujibu wa sheria na linalotawaliwa kwa amri ya jeshi;
"Jumuiya ya Madola" maana yake ni jumuiya ambayo wanachama wake ni Jamhuri ya Muungano, Uingereza na kila nchi ambayo iliwahi kutawaliwa na Uingereza;
"kiapo" maana yake itabidi ifahamike kwa maana ya kawaida ya neno hilo na ni pamoja na tamko rasmi la namna yoyote linaloruhusiwa kisheria kutumiwa badala ya kiapo;
"kiapo cha uaminifu" maana yake ni kiapo cha kuwa mwaminifu kwa Nchi na kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
"Maadili ya Kazi ya Jaji" maana yake ni masharti ya kimaadili yanayoongoza mwenendo wa watu wafanyao kazi ya Jaji au ya Hakimu;
"madaraka ya kazi katika utumishi wa Umma Jamhuri ya Muungano" maana yake itabidi ifahamike kwa mujibu wa maana ya kawaida na maneno hayo na ni pamoja na utumishi katika Majeshi ya Ulinzi ya Jamhuri ya Muungano na katika Jeshi la Polisi au jeshi linginelo lilioundwa kwa mujibu wa Sheria;
"mahakama" maana yake ni mahakama yoyote yenye mamlaka katika Jamhuri ya Muungano isipokuwa mahakama iliyoundwa kwa amri ya jeshi; lakini kwa ajili ya ibara ya 13, ya 14 na ya 15 za Katiba hii, itakuwa ni pamoja na mahakama iliyoundwa kwa amri ya jeshi;
"Mahakama Kuu" maana yake ni Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano au Mahakama Kuu ya Zanzibar;
"Mambo ya Muungano" maana yake ni mambo yote ya umma ambayo yametajwa na ibara ya 4 ya Katiba hii kuwa ni Mambo ya Muungano;
"Mamlaka ya Nchi" ni pamoja na Serikali na Bunge la Jamhuri ya Muungano, pamoja na Serikali na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar;
"Mwanasheria Mkuu" maana yake ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano aliyetajwa katika ibara ya 59;
"Serikali" maana yake ni pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au Halmashauri ya Wilaya au ya Mji, na pia mtu yeyote anayetekeleza madaraka au mamlaka yoyote kwa niaba ya Serikali au Halmashauri;
"Serikali za Mitaa" maana yake ni vyombo vya kiserikali vilivyoundwa kwa mujibu wa ibara ya 145 ya Katiba hii kwa madhumuni ya kutekeleza madaraka ya umma;
"Tanzania Bara" maana yake ni eneo lote la Jamhuri ya Muungnao ambalo zamani lilikuwa eneo la Jamhuri ya Tanganyika;
"Tanzania Zanzibar" maana yake ni eneo lote la Jamhuri ya Muungano ambalo zamani lilikuwa eneo la Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na ambalo kabla ya Sheria hii kutungwa liliitwa Tanzania Visiwani;
"Uchaguzi Mkuu" au "uchaguzi unaofanywa na wananchi" maana yake ni uchaguzi wa Rais na uchaguzi wa Wabunge wanaowakilisha wilaya za uchaguzi unaofanywa baada ya Bunge kuvunjwa;
"Ujamaa" au "Ujamaa na Kujitegemea" maana yake ni misingi ya maisha ya jamii ya kujenga Taifa linalozingatia demokrasia, kujitegemea, uhuru, haki, usawa, udugu na umoja wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano;
"Waziri" maana yake ni Mbunge aliyekabidhiwa madaraka ya kazi ya Waziri, isipokuwa Naibu Waziri, na maana hiyo itatumika pia kwa Makamu wote wa Rais;
"Zanzibar" maana yake ni sawa na maana ya Tanzania Zanzibar.


Sijui mwenzetu ulitaka kuwe na definition zipi!

Asante, kumbe definition ziko kwenye ibara ya mwishio kabisa ambayo kwa bahati mbaya sikuwa kusoma. Ni kawaida ya definition zote kuorodheshwa kabla hazijaanza kutumika. Huku kutokuwa systematic kwenye katiba yetu ni mojawapo ya mambo ambayo ningependa yarekebishwa ikiwezekana.

Zaidi ya hizi definitions, bado naamini kuwa kifungu kile nilichoongelea 2-(2) kimekaa mahala pasipohusika kabisa ingawa haki-affect lengo la katiba. Hakina ulazima kabisa kuwepo pale, ni kifungu ambacho kingewekwa chini ya powers za President.
 
Ndugu Mzizi Mkavu

Siyo kwamba nachukia ujamaa, lengo langu wakati naannzisha tthread hii ni kuangalia upungufu wa katiba yetu ili tupate mawazo ya kuinyoosha. Kuweka ndani ya Katiba kuwa tunajenga taifa la kijamaa ilhali tunajua kuwa hatufanyi hivyo, ni ama tudharau na kukiuka katiba yetu makusudi, au katiba hiyo siyo ni kitu serious. Ningependa kila kilichoko ndani ya katiba kiwe ni kitu sahihi; kwa hiyo neno ujamaa liondoplewe tu. Katiba imeshasema tunajenga taifa lenye misingi ya haki kwa watu wote; hilo ni lengo linalotosha kabisa kuliko kuongeza ujamaa ambao siyo kweli.

Kwa tafsiri hii ya ujamaa katika katiba yetu, sioni kama ina tatizo kwa neno ujamaa kuendelea kuwapo kwenye katiba:

"Ujamaa" au "Ujamaa na Kujitegemea" maana yake ni misingi ya maisha ya jamii ya kujenga Taifa linalozingatia demokrasia, kujitegemea, uhuru, haki, usawa, udugu na
umoja wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano;
 
Back
Top Bottom