Moyo wangu 'umemdondokea' huyu dreva wa Bodaboda

NAKWEDE

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2007
Posts
27,970
Reaction score
35,168
Moyo jamani moyo!!!

Mwenzenu nimetokea kumpenda Dreva wa Bodaboda hadi najisikia akili inadundadunda.
N mwanamme mpole, ana kamzuzu kwa mbali, mweusi, mnene kiasi, mrefu, akicheka ana kamwanya fulani hivi, jaman jamani mie yaani natamani kila mara nimuone tu japo kwa mbali.

Nimefanya upelelezi wangu, ni miongoni mwa wale watumishi waliopata dhahama ya vyeti feki.

Na yeye ananipenda ila hajawa direct. Jamani moyo huuu.

Nimewaza zawadi ya kumpa ili kuonesha nampenda ila bado sijafikia maamuzi sahihi. Nawaza nikamnunulie yale makoti yao mazito kama manne hivi, au nimnunulie boxer, au nimnunulie kadi.

Hebu nishaurini nimnunulie nini mimi huyu ndugu anayeutesa moyo wangu kama ishara ya kumuonesha kuwa nimekufa na kuoza hadi kunuka juu yake.

MBITIYAZA msaada mwenzio niko hoi kwa bodaboda
 
Mpe papa maana inawezekana anapendaga samaki kama sisi waathu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…