Naomba Uzi huu usiunganishwe na wowote modes.
Kimsingi akili mwili na roho yangu vinagoma kuamini Ben sanane na Azory gwanda sitawaona milele Yani siamini kabisaaaa.
Mpaka kesho nitajiuliza kwanini Mungu amewatwaa watu Hawa Kama nabii eliya?
Au hii inanivutia niamini kwamba hata bibilia iliandikwa kwa misingi hi?
Pengine nabii eliya nayeye alipotea kwenye mazingira haya ya Ben sanane na Azory gwanda ndio maana walioandika biblia waliamua kuweka shotkat?
Kitendawili hiki Cha Ben na Azory ipo siku kitateguliwa !!
Siku hazigandi!! Hata ya lisu bado yako moyoni .
Mambo yote haya yatakuja kulipuka Kama mlima Vesuvius kule pompeii Italia!!
Modes tendeni haki kwa kuacha nyuzi za watu ziishi!!
Mtu huyu mwenye rekodi ya mwanamkakati wa Pm-7 alizaliwa 13/12/1983
Mkuu Tutashinda, kauli huumba, na lisemwalo lipo kama halipo, linakuja!.
Angalia heading ya bandiko lako hili, na tarehe ya bandiko hili, halafu angalia nini kilikuja kutokea kwa Ben Saanane.
Uchaguzi wa Bavicha ndio joto linaanza kupanda.Ni jambo la hatari sana kuwa na mtu kama Ben Saanane kwenye nafasi ya juu ya BAVICHA.Tumeamua kuitendea haki BAVICHA na sasa kanuni za uchaguzi ndizo zitakazozingatiwa tu.Kiongozi ambaye kazi yake ni kufikiria namna ya kulipiza visasi hafai hata...
www.jamiiforums.com
Wana jf tuanze kujifunza kuchunga kauli zetu, kauli nyingine zinaumba, ukisema mwisho wa fulani, bila hata wewe kumaanisha ni mwisho kwa kutoweka, kwenye heading ulisema
"ben-saanane-mwisho-wake-umefika-rasmi",
Wewe bila kujua kuwa kauli hii ina powers, baada ya kutolewa bila kuwekewa any caveat ya mwisho wa nini, then powers zimeanza ku act kuutengeneza mwisho wa Ben.
Maadam kwenye bandiko hili, ulidhamiria mwisho wa Ben Saanane ni mwisho kwenye uchaguzi wa Bavicha, then the headline yako should have said so, " Ben Saanane Mwisho Wake Kugombea Bavicha Umefika Rasmi " ili zile powers za kauli yako iwe limited kwa Bavicha tuu, kitendo cha kutoa open ended statements bila kinga, ndicho kimepelekea kuchangia kufika mwisho kwa Ben Saanane.
Kwenye bandiko hili mimi pia nilichangia
Japo mimi sio Chadema na sina chama, ila tukubali tukatae, ukiondoa mapungufu yake ya kibinaadamu, (hakuna binaadamu mkamilifu), Ben Saanane, is the type of leaders BAVICHA, should have had long ago, and had it been, he had been there, BAVICHA would not have been the same again, it would have been far far ahead, by now CCM ingekuwa bize kukusanya kusanya kilicho chake kupisha njia!.
Thanks.
Pasco.
From no where, jana nimetokea tuu kumkumbuka Ben Saanane, sikujua kwanini, hivyo nilipoamka nikaanza kupitia baadhi ya mabandiko humu ndipo nikakutana na bandiko hili la 2014, nilipolisoma ndipo nikagundua kumbe jana ndio tarehe ya kuzaliwa ya Ben Saanane.
Happy Birthday Ben Saanane.
P