Mpaka sasa sijaona mchezaji Kama Ronaldinho (GAUCHO)

Mpaka sasa sijaona mchezaji Kama Ronaldinho (GAUCHO)

"Mpaka sasa sijaona mchezaji kama Ronaldinho"

Tuanzie kwanza kwenye kichwa chako cha habari.. Umeanza kuona/kuangalia mpira lini kwanza?

Siongelei clips za youtube nataka kufahamu ni mwaka gani hasa umeanza kufuatilia mpira live?
 
Mkuu hivi Leo FIFA iweke majina kumi ya wachezaji bora kuwahi kutokea duniani huwezi kuamini Ronaldinho anachukua nafasi ya Kwanza.

Hakuna ambaye hajui kiwango cha jamaa.

We angalia hata hapa JF uone jamaa uwezo wake unavyokubalika. Pia wachezaji wengine hufanya mambo ya kawaida ambayo hata mtanzania wa Timu ya Libolo huweza kufanya. Tofauti na Gaucho ambaye hufanya vitu ambavyo wengi sio rahisi kufanya.

Unafurahisha
 
LIONEL MESSIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII.

Fatilieni records na stats afu mrudi hapa. Tuweke hisia pembeni
Messi ni chalii kwa GAUCHO mkuu.
Tunapozungumzia mpira tunazingatia.
1.ball control
2. Dribbling/vyenga
3. Energy/pumzi
4. Nguvu.
5. Ufungaji wa magoli.
6. Ugawaji pasi.

Sasa utaniambia mwenyewe Messi amepunguka wapi.

Gaucho alikuwa ananguvu na kontrol ya mpira ndio maana alikuwa anapenda Sana mipira ya juu. Iwe kupiga mtu kanzu, kuweka kwa Kifua n.k.
Wakati Messi hutumia zaidi mipira ya chini zaidi kuliko ya juu kumaanisha anajua hana nguvu/msuli wa kuzuia adui asichukue mipira yake ya juu na uhafifu wa kontrol wa mipira ya juu.

Aidha Messi anatumia zaidi mguu mmoja wa kushoto wakati Gaucho anatumia yote.

Messi anachoweza kumzidi Gaucho pengine ni ufungaji wa Magoli unaosababishwa na ushindani wake na Ronaldo lakini Kama Gaucho angekuwa na mpira wa ushindani basi historia ingekuwa nyingine kwani jamaa angekuwa mfungaji ambaye hakuna ambaye angemfikia
 
Habari Wakuu!

Tokea ninakua mpaka sasa bado sijawahi ona ona mchezaji Mpira anayemfikia GAUCHO kwa ubora.

kwa wanaomjua Gaucho wataungana na Mimi na hawatanishangaa nikimkubali huyu mchezaji ambaye wataalamu tunamuita Mchawi wa Soccer.

Gaucho alikuwa mahiri kwa kuukontroli Mpira. Alikuwa anauwezo wa kuuweka mpira sehemu yoyote ya mwili.

Aidha Mbrazili huyu kwenye swala za dribbling bado hakuna anayemkamata.

Hutotamani mpira uondoke mguuni mwake pindi afanyapo mambo yake.

Gaucho ni miongoni mwa Wachezaji wakali kuwahi kutokea duniani.


Je wewe unadhani ni nani anayemkaribia huyu Mchawi wa Soccer kwa maana kwa wakumzidi bado hayupo.
Mkuu, zidane alikuwa mchezaji mzuri sana walikuwa wanaweza kwenda sawa tu na gaucho. okocha pia alikuwa mzuri. hao kina Mesi na Ronaldo wa ureno ni bidii na bahati tu ila sio kipaji cha kuzaliwa nacho.
 
"Mpaka sasa sijaona mchezaji kama Ronaldinho"

Tuanzie kwanza kwenye kichwa chako cha habari.. Umeanza kuona/kuangalia mpira lini kwanza?

Siongelei clips za youtube nataka kufahamu ni mwaka gani hasa umeanza kufuatilia mpira live?
2004.

We unadhani kwa nini hata hapa JF Watu wengi hufikiri kuwa Gaucho ni mchezaji bora ambaye hana Spare yake.
 
Mkuu, zidane alikuwa mchezaji mzuri sana walikuwa wanaweza kwenda sawa tu na gaucho. okocha pia alikuwa mzuri. hao kina Mesi na Ronaldo wa ureno ni bidii na bahati tu ila sio kipaji cha kuzaliwa nacho.
We unajua mpira Mkuu.
Safi Sana.
 
Mkuu hivi Leo FIFA iweke majina kumi ya wachezaji bora kuwahi kutokea duniani huwezi kuamini Ronaldinho anachukua nafasi ya Kwanza.

Hakuna ambaye hajui kiwango cha jamaa.

We angalia hata hapa JF uone jamaa uwezo wake unavyokubalika. Pia wachezaji wengine hufanya mambo ya kawaida ambayo hata mtanzania wa Timu ya Libolo huweza kufanya. Tofauti na Gaucho ambaye hufanya vitu ambavyo wengi sio rahisi kufanya.
Hapa JF akichukua sitashangaa wengi ni mashabiki hawajui mpira.
Huko ulaya kwenye 10 bora utakutana na majina haya huku 1-3 wakibadilishana Messi, Maradona na Pele.
Huku nafasi zilizo baki utakutana na haya majina.
Best
Platin
Gerd Muller
Eusebio
Lothar Matthaurs
Puskas
Garrincha
Cruyff
Beckenbauer
Di Stefano
Zidane

Huyo Ronaldinho huko Brazil kwenyewe top 3 hayupo kuna akina De lima, Pele, Garrincha.
Ataingia Top ten ya Dunia kweli.!?!?
Labda top 10 ya shafii dauda.
 
wengi humu wamezaliwa juzi.

nataka waliowaona hawa wachezaji waje tuzungumze...zidane..stephen efernberg...dinho..
figo ...luis enrique...raul...rivaldo...nedved..batistuta....

P 5
 
hapo sasa unafosi nipende unachotaka wewe
pia hizo videos ziko kwa ajili ya biashara kule youtube ubora wa mchezaji unapimwa kwa mechi sio clips
sijakataa kuwa Ronaldinho si mchezaji mzuri don't quote me wrong braza
We unadhani ni vigezo gani vinamfanya mchezaji awe bora kuliko wengine?

Umesahau na suala la Promo, wachezaji wengi hufanyiwa promo na kusapotiwa akiwemo Ronaldo, messi.
Hawa hutumia bidii zao na wala si kipaji cha kuzaliwa
 
Hapa JF akichukua sitashangaa wengi ni mashabiki hawajui mpira.
Huko ulaya kwenye 10 bora utakutana na majina haya huku 1-3 wakibadilishana Messi, Maradona na Pele.
Huku nafasi zilizo baki utakutana na haya majina.
Best
Platin
Gerd Muller
Eusebio
Lothar Matthaurs
Puskas
Garrincha
Cruyff
Beckenbauer
Di Stefano
Zidane

Huyo Ronaldinho huko Brazil kwenyewe top 3 hayupo kuna akina De lima, Pele, Garrincha.
Ataingia Top ten ya Dunia kweli.!?!?
Labda top 10 ya shafii dauda.

Sina cha kuongeza hapo
 
Ronaldinho hakuna anayemfikia, ile computer.
Ni kweli mkuu.
Jamaa hafanyi bidii lakini yupo vizuri.
Unaambiwa jamaa anasifa ya uzembe na kudoji mazoezi lakini mambo ndio yale tuyaonayo.
Jamaa anakipaji cha kuzaliwa
 
Kwa kizazi cha karibuni cha wachezaji wenye vionjo uwanjani gaucho ndo kaondoka navyo maana wachezaji wa zama hizi wao nikukimbiza tu.ila hapo nyuma gaucho alitanguliwa na mafundi kama kina maradona,okocha,zidane,rivaldo nedved nawakali wengine we sema miaka iyo mafundi walikua wengi na hakukuwa na mbwembwe nyingi za kupambana kama miaka ya hivi karibuni ndo maana huwez kuwasikia sana au hata taarifa zao zinaonekana za kawaida.Hata hapa bongo miaka ya nyuma ndo kulikua na soka safi,kulikua na kina thomas kipese,madaraka suleiman,zamoyon mogela,edward chumila,nteze john,edibil lunyamila,geo masatu namafundi wengine ila ndo ivyo pamoja na soka lao kubwa bado historia yao inaonekana ya kawaida kwasababu ya zama.Kwaiyo naunga mkono hoja nikizingatia na wakati.
Upo vizuri mkuu.
Sasa hivi unaweza kuangalia mpira ukapatwa na usingizi lakini si zamani
 
wengi humu wamezaliwa juzi.

nataka waliowaona hawa wachezaji waje tuzungumze...zidane..stephen efernberg...dinho..
figo ...luis enrique...raul...rivaldo...nedved..batistuta....
Wewe mwenyewe umezaliwa Jana halafu unasema wenzio... Angalau ungetutajia akina maradona baggio klinsmaan... Tumekuona kidogo na wewe u mtu mzima.
 
Back
Top Bottom