Mpaka wa Namanga wafungwa kwa muda baada ya Kenya kuwazuia madereva malori kutoka Tanzania kwa kutokuamini vipimo vyao vya #Corona

Mpaka wa Namanga wafungwa kwa muda baada ya Kenya kuwazuia madereva malori kutoka Tanzania kwa kutokuamini vipimo vyao vya #Corona

Hii imani ndiyo Ina tufanye tusitangaze idadi ya maambukizi?
Wewe mwenyewe na ukoo wenu hakuna hata mmoja mwenye Dalili za zozote za Covd na tangu ugonjwa huu kuingia umekuwa ripota wa mitandaoni kila siku, hujawahi kuugua na hata kufa, ili Hali wewe unatangaza eti Corona inamaliza watu, Kwa nini Wao na sio wewe, hapo ndipo napoona uwongo wenu

Wakati huohuo unataka watu waendelee kupima, na Wakati Hakuna hata mwenye Dalili hizo Hadi kwenu, mkuu, mbona mnatuombea mabaya tu mkuu
 
kama umepata dawa ya kutibu nitaenda, ila kama hakuna na sijasikia dalili yoyote siwezi kwenda, maana hiyo 120000 inatosha kununua tangawizi na vitunguu pamoja na limao, pia nitaingia sauna kwa muda mrefu sana.
Kumbuka kupima corona sio kama kupima mkojo, kuna maumivu watu wanapata, sasa usifikili kuchokonolewa watu wansikia raha.
Unaona basi? Sasa ungekuwa dereva ungepima kweli ikiwa unaambia kwa 25,000 unapewa cheti bila kupimwa?
 
MPAKA wa Namanga upande wa Tanzania umesitisha shughuli zote za kibiashara na nchi jirani ya Kenya kwa muda kutokana na nchi hiyo kutoamini vyeti vya ugonjwa wa Covid -19 unaosababishwa na virusi vya corona vya madereva wa malori wa Tanzania vinavyoonyesha kuwa hawajaambukizwa.

boda.jpg

Mkuu wa Wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe, ameiambia Nipashe jana kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya upande wa Kenya kukiuka makubaliano ya pande hizo mbili, waliyotiliana saini Mei, mwaka huu kwa kuzuia madereva wa Tanzania, kukataa vyeti ili wawaruhusu kuingia Kenya.

“Nadhani wenzetu wana ajenda ya siri kutuhujumu kiuchumi, tumeshakubaliana dereva anapopimwa upande wa Tanzania aruhusiwe upande wa Kenya kwa cheti, sasa wamekiuka makubaliano, wakifika upande ule wanataka wawapime tena sijui wana maana ipi nashindwa kuwaelewa kabisa, tumeamua kuchukua hatua na haturudi nyuma,” alisema.

Katika makubaliano hayo waliamua katika lori itaruhusiwa dereva na wasaidizi wawili kuingia katika nchi husika wote wakiwa wamepimwa kama wana maambukizo ya corona.
Hata hivyo, alisema upande wa Kenya wamebadilika juzi (Jumatatu) kwa kuzuia na kutaka kuwapima tena.

“Pamoja na juhudi za mimi na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, kuwasiliana na viongozi wenzetu wa Kenya, lakini zimegonga mwamba na ndipo tukaamua kuzuia vyeti vyote na magari ya mizigo kutoka Kenya pamoja bidhaa zote zinazoingia kutoka nchini humo hadi hapo tutakapokaa tena na kufikia muafaka maana sote tunategemeana, Kenya wanatuhitaji kama soko na sisi wanatuhitaji pia ili kuuza bidhaa,” alisema Mwaisumbe.

Alisema mwezi Mei makubaliano ya kuruhusu kuaminiana pande mbili yalikaliwa kikao na mawaziri wa mambo ya nje za nchi, makatibu wakuu, wataalamu na viongozi wengine wa mikoa na wilaya wa kutoka nchi mbili katika mpaka wa Namanga, kufuatia mazungumzo ya Rais John Magufuli na Rais Uhuru Kenyata ambao waliwaagiza viongozi wanaohusika kukaa na kufanya vikao na makubaliano, huku wakichukua tahadhari za ugonjwa huo na kuona namna ya kuendelea na biashara kwa nchi hizo.

Alisema kama hali ya kutoaminiana itaendelea, itawalazimu kutoa uamuzi wa kuigeuza Namanga kuwa bandari kavu na majirani Wakenya watashusha mizigo au bidhaa upande wake na Tanzania kuichukua na pia hata Tanzania itapeleka wa Tanzania ili Kenya waifuate.

“Nchi yetu ni huru inayojitegemea haihitaji kubembeleza nchi nyingine kufanya biashara kwa sababu sisi tunategemeana, haiwezekani mambo ambayo yameagizwa na marais viongozi wa chini hawatekelezi…linaashiria dharau na ajenda ambayo wanadhani ni siri iliyofichika kumbe sisi tunaifahamu, hatutaweza kuivumilia hata kidogo,” alisema.

Alisema, nia ya Rais Magufuli ni kuwasaidia watu wa hali ya chini kwa kuwa uamuzi huo unapofanyika wanao umia ni watu wa chini.

“Nataka nikuhakikishie ndugu kupima kipimo cha Covid-19 sio lelemama kinaumiza sana, sasa haiwezekani siku mbili mtu amechokonolewa pua, halafu anatoka upande wa Tanzania anaenda upande wa Kenya anafanyiwa kitu kile kile, sasa hali hii kwa kweli sio sahihi, tunataka hiyo agenda yao ya siri ijitokeze hadharani tushughulike nayo kuliko kutumia ugonjwa wa Covid-19, sisi hatutakuwa tayari,” alisema Mwaisumbe.
Kenya wako sahihi,
Tanzania wana pima wapi wagonjwa
 
Hahahaha! You are not serious my brother. Serikali hii inayosema corona imeisha ndio nikaiambie kuna watu wenye corona wanapewa vyeti bila kupima?

Hapo mie ndio nitawekwa ndani.


Labda kama hao wanaotoa vibali ni wajomba zako, taarifa zinatolewa kwa njia nyingi, hata hapa jukwaani unaweza kutoa hiyo taarifa na watu waliopewa ikafanyika msako kwa hao maderva kazi itakuwa imeisha.
 
Wewe mwenyewe na ukoo wenu hakuna hata mmoja mwenye Dalili za zozote za Covd na tangu ugonjwa huu kuingia umekuwa ripota wa mitandaoni kila siku, hujawahi kuugua na hata kufa, ili Hali wewe unatangaza eti Corona inamaliza watu, Kwa nini Wao na sio wewe, hapo ndipo napoona uwongo wenu

Wakati huohuo unataka watu waendelee kupima, na Wakati Hakuna hata mwenye Dalili hizo Hadi kwenu, mkuu, mbona mnatuombea mabaya tu mkuu
Kama hakuna anaekufa kwanini watu walizikwa usiku kule Unonio na wazikaji wakiwa wamevaa mavazi mwalimu?
 
Tatizo lipo Tanzania! Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu. Ukute madereva wote kutoka Tanzania wanapewa tu vyeti hata Corona hawapimwi tena kwa sababu Tanzania inaamini kuwa Corona ilishaisha!

Kama tatizo ni hilo jibu lake ni rahisi sana. Wafanyakazi wa Kenya Madaktari, Wafanyakazi wa mahabara, na manesi wakishirikiana na wafanyakazi wa Tanzania katika mahabara za upimaji covid- 19.

Katika cheti kuwe na sahihi ya daktari wa Tanzania na Kenya. Mchezo umekwisha, tatizo liko wapi.
 
Kama una akiri jiulize, walizuia magari nasi tukazuia kama wao, kila mtu ana haki.ya.kujilinda na nchi yake,
Sasa Uhuru alipiga simu ya kumaliza tatizo ili iweje?
Kama anaona Tanzania kuna corona alipiga simu ya nini, atangaze tu kuwa hakuna kuruhusu m tz kuingia basi nasi tutafanya hivyo na maisha yataendelea.
Hawa wakenya wana dharau sana.
Sioni logic kwenye andiko lako.Huwez kujua mtu ana corona bila kupimwa.
Si watanzania wote wana corona. Wapo wanaopita mipakani fresh tu tena wako cleared na vipimo.

Siwez jua uhuru aliongea nn na jpm. Wakaja na resolution kila mtu apimwe kwake apewe cheti.
Kama wanamashaka na vipimo vya tz. Wanaweza alert mamlaka za tz wakaja na mbinu ingine.
Uswahili hapa hautotusaidia..
Sisi tupeleke madkatari wetu mpakani. Ili na wao wakiingia kwetu haijalishi vyeti vyao. Sisi tunapima tu.
Kuwe na check and re-check.. hapa tutaenda sawa.
 
Mkuu naomba unijibu maswali machache haya, Ni kiongozi gani mwenye mamlaka ya kutangaza kuhusu corona aliyesema corona imeisha Tanzania? Toka itangazwe kuhusu kuruhusu maisha kuendelea lakini kwa tahadhari ni ndugu au majirani zako wangapi wamekufa na corona?
Kwa kusema wagonjwa wamebaki wanne tu Tanzania na sasa tunafungulia kila kitu ni sawa na kusema Corona imeisha. Taarifa hizo zilitolewa na Waziri Mkuu na kuthibitishwa na Waziri wa Afya.

Hatuwezi kujua idadi ya wagonjwa au wanaokufa kwa kuwa Tanzania ilsema haitatangaza kwa kuwa inapanikisha watu. Na pia hatuwezi kujua kwa kuwa Tanzania haipimi watu.

Inawezekana kabisa kwamba karibu 50% ya Watanzania wana virusi vya Corona, pamoja na mimi na wewe
 
Tanzania tunafanya mambo kiajabu sana, na hii yote inasababishwa na kufuata mawazo ya mtu mmoja, haiwezekani mseme vipimo vyenu vilikuwa vibovu baada ya kuvichunguza, halafu baada ya muda mnaanza kulazimisha idadi ya wagonjwa wa Corona imepungua, mtu mwenye akili atajiuliza imepungua kwa vipimo gani mlivyowapimia?

Hao wakenya ni haki yao kugoma, kwasababu kwanza tulishajifunga wenyewe kwa kukiri vipimo vyetu vilikuwa vibovu, sasa kwanini waamini hivyo vyeti vinavyopelekwa na madereva wetu? waacheni watumie vipimo vyao kuwapima wajiridhishe.

Halafu kwa akili za viongozi wetu watakurupuka nao kuwazuia wakenya, sijui watawazuia kwasababu gani wakati wakenya hawakuwahi kukiri kama vipimo vyao ni vibovu hivyo tusiwaamini madereva wao.

Yaani maji yametufika shingoni.
 
Kama tatizo ni hilo jibu lake ni rahisi sana. Wafanyakazi wa Kenya Madaktari, Wafanyakazi wa mahabara, na manesi wakishirikiana na wafanyakazi wa Tanzania katika mahabara za upimaji covid- 19.

Katika cheti kuwe na sahihi ya daktari wa Tanzania na Kenya. Mchezo umekwisha, tatizo liko wapi.
Hapo umeongea point ndugu yangu!
 
Hawa Wakenya wanaimani zaidi na ubalozi wa Marekani TZ kuliko taarifa kutoka kwa maabara zetu! Huwezi kumlazimisha mtu kuamini wakati general infos ni shida kutolewa
Na sisi hatuwezi walazimisha waige style yetu. Na sidhan kama wanaiman na ubalozi wa marekani. Wana iman na vipimo vyao... ndio maana wana namba kubwa. Imewapa hofu sana na wako kwenye high alert.
 
Kama ndo hivyo nitapimwa naumwa
 

Attachments

  • VID-20200527-WA0000.mp4
    4 MB
Kama hakuna anaekufa kwanini watu walizikwa usiku kule Unonio na wazikaji wakiwa wamevaa mavazi mwalimu?
Ahaaah, kumbe unaongelea yaliyopita? Ijapokuwa sina uthibitisho wa Hilo mkuu, Basi nimekuelewa mkuu,
 
Sasa hao wanaochukulia serious kupambana na corona wapi wamefika na kupambana kwao, vip USA? Etc na Nchi zingine, hofu inaua kuliko corona, sisi tunajielewe sana kam Tz mpya tunalindwa na Mungu na sio mwandamu au maneno ya jirani,

Huwezi kujenga nyumba kwa kusikiliza meneno ya jirani lazima sisi Tz tujiamrie kama Nchi inayojitawala,

Mh. Dr JPM mbele kwa mbele 2020🔥🔥🔥🔥
 
Labda kama hao wanaotoa vibali ni wajomba zako, taarifa zinatolewa kwa njia nyingi, hata hapa jukwaani unaweza kutoa hiyo taarifa na watu waliopewa ikafanyika msako kwa hao maderva kazi itakuwa imeisha.
Mkuu, kama Tanzania haikushughulika na taarifa za waliohusika na kutekwa na kuua watu tulizowapa, unafikiri kwa nini watachukulia taarifa za vyeti kwa uzito? Yaani forgery za vyeti vya Corona ni jambo la muhimu kuliko taarifa juu ya wauaji?
 
Back
Top Bottom