Pole kwa mkasa huo mkuu:-
USHAURI:
1. Njia ulokuwa unatumia wewe ni njia ya amani/diplomasia, ambayo tyr imeshindwa kuleta matunda.
2. Kwa mujibu wa kifungu cha 103 (1) cha sheria ya Ardhi Na. 4/1999 utaratibu unaotakiwa kuufanya ni wa kimahakama, yaani kwa kufungua shauri la madai Mahakamani la kuiomba Mahakama itoe amri ya huyo mpangaji kuondoka (VACANT POSSESSION OF THE DEMISED PROPERTY).
3. Kifungu cha 167 cha sheria hiyo kinatamka Mahakama ni a). Baraza la Ardhi la kijiji, b). Baraza la kata, c). Baraza la Ardhi na nyumba la Wilaya, d). Mahakama kuu, na e). Mahakama ya Rufani (kwa rufaa pekee).
4. Hujatuambia kama upo mjini, ama Wilayani (vijijini) NA/AU Ardhi yako imepimwa ama laa. Mi natumai upo mjini, basi piga hesabu ya kodi yote unayodai kama haitazidi Milioni 300 (yaan 300,000,000/=) KAFUNGUE KESI YA KUMWONDOSHA katika Baraza la Ardhi na nyumba wilaya, ambalo lina mamlaka na eneo ulipo. (KUMBUKA: Mabaraza haya huwa ni ya kikanda sio kila wilaya). Kwa nini sijasema baraza la kata? Kwa sababu katika shauri la Ardhi Misc. Land Appeal No. 129 of 2009 Mahakama kuu ilitamka kuwa Mabaraza ya kata yaliyopo mijini hayana mamlaka na mashauri ya Ardhi.
HIVYO BASI KAFUNGUE KESI MAHAKAMA YA ARDHI ILI UKISHINDA UPEWE DALALI WA KUMWONDOSHA MPANGAJI KWA AMRI YA MAHAKAMA. KUNA POSITI NIMESOMA INASEMA MKAANDIKISHANE POLISI, IPO HIVI KWA MUJIBU WA SHERIA YA POLISI (SURA 322) PAMOJA NA POLICE GENERAL ORDER (PGO) POLISI HAIHUSIKI NA MASUALA YA MADAI BALI NI KWA JINAI PEKEE.
N.B Balozi wa nini karne hii ya 21?? Hata kwa sheria ya serikali za mitaa (Na. 7/1982) hayumo. ungeenda kwa M/Kitongoji ndo maana limekudharau.
Sent using
Jamii Forums mobile app