DOKEZO Mpangaji wangu kageuza Nyumba yangu kuwa kiwanda bubu cha kutengeneza vinywaji vikali feki kama Konyagi, K Vant nk

DOKEZO Mpangaji wangu kageuza Nyumba yangu kuwa kiwanda bubu cha kutengeneza vinywaji vikali feki kama Konyagi, K Vant nk

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Ningekuwa mimi, ningemtafuta mpangaji wangu kistaarabu nimwambie kuwa ahame kwani anachokifanya ni kinyume na makubaliano ya mkataba wetu ili sote tusije kuingia ktk matatizo, suala la kumripoti wakati polisi wanajua kinachoendelea kinaweza kkukuweka hatarini zaidi anaweza hata akaichoma moto usiku,na namwambia kuwa akiendelea kukaidi nitachukua hatua zaidi ili kujiwka salama!
 
Wapendwa habarini.Mimi ni Mtumishi wa Umma nipo Dodoma.Nina nyumba yangu nimeijenga Boko. Nilimaliza kuijenga Mei mwaka huu na Juni nikapata Mpangaji(Mme na Mkewe).

Nilishukuru maana Mpangaji huyu alijitambulisha kwamba ni Mfanyabiashara anayefuata mizigo China hivyo yupo busy sana, alinilipa Kodi ya miaka miwili(nilifurahi sana). Mwanzoni mwa mwezi huu wa Septemba jirani yangu ambaye tumetengana ukuta(fensi) alinipigia na kuniuliza kama nimeigeuza nyumba yangu kuwa godown au kiwanda cha kutengeneza vinywaji maana alidai kunakuwa na kelele za chupa kugongana usiku, nilimjibu hapana lakini nitafanya uchunguzi.

Juzi Jumapili nilikuwa Dar, hivyo mchana nilienda hapo Boko nyumbani kwangu bila kuwapa taarifa. Cha kushangaza nikakuta kafunga CCTV Camera kwenye pembe zote za fensi pamoja na kuweka Mlinzi getini. Nilivyojitambulisha getini Mlinzi hakufungua geti alinizuia kuingia(imagine nyumba yangu lakini nazuiliwa kuingia).

Nikiwa pale getini nahojiana na Mlinzi, ilikuja gari la Polisi ikasimama kwa mbali, kijana mmoja akatoka ndani ya nyumba yangu na kwenda kwenye ile gari na kuwapa naamini pesa na gari ya Polisi ikaondoka, kijana akarudi akaingia ndani, akafunga mlango, hapo mimi nimezuiwa getini. Kwa kifupi ni kwamba Mpangaji wangu huyu anazalisha bidhaa feki(vinywaji feki) na kuziingiza sokoni.

Msiri wangu ameniambia Konyagi, K-Vant, Gin na vinywaji vingine vikali vinazalishwa ndani ya nyumba yangu na kuingizaa sokoni. Naogopa asije akakamatwa mwisho wa siku Serikali ikataifisha nyumba yangu maana nimeambiwa hilo ni Kosa la Uhujumu Uchumi.

Naomba msaada taarifa hii nikaitoe wapi maana msiri wangu kaniambia Polisi wanajua na huwa wanaenda kuchukua posho kama nilivyoshuhudia mimi mwenyewe hivyo hata nikiripoti kwao itakuwa ni kazi bure.

Naomba mwenye mawasiliano na Viwanda vinavyotengeneza Konyagi, K Vant na hizi Pombe Kali za chupa anisaidie tafadhali Ili niwajulishe tushauriane cha kufanya

Nitashukuru sana wapendwa, siku njema
Mimi huwa nashangaa mtu anatafuta msadda halafu anaficha taarifa. Weka eneo ilipo nyumba mtaa na namba ya nyumba labda utuambie mmeshindwana kwenye biashara yenu ndiyo unamchoma. Kama unahitaji msaada kweli toa taarifa iliyo kamili
 
Daah baba mwenye nyumba asiione hii taarifa 🤣🤣 mimi mwenyewe nna store ya nafaka sometime huwa nashusha mzigo haitoshei maana ni ndogo kwa hiyo baadhi ya magunia huwa nayahamishia nyumbani huko huko nayapanga !! Mpaka mzigo upungue store !!
 
Kuwa makini na unachotaka kufanya,kumreport polisi utakuwa umeharibu maisha yake na kucheza na maisha ya mtu ni kujiweka katika hatari ww na family yako.Kama Kuna uwezekano mtafutemwenyewe muongee nae kwanza
 
Jamani tumieni mitandao kwa uangalifu. Umejiexpose sana mwanadada. Yaani kwa taarifa hii umejiweka hadharani. Hii nchi kwa sasa imechafuka, hao manjagu sio wa kuwaamini. Kwa hali ilivyo unaweza kujikuta ni next Kibao......

Ungeweza kuitoa taarifa hii kwa style nyingine.
 
kuwa makini unaweza kuhatarisha maisha Yako, kama hao manjagu wanaokwenda kuchukua mpunga ndio watakumaliza.
Tafuta mwanasheria akuongoze ukikurupuka umekwisha
Ni kweli. Nyumba ni yake lakini akienda kichwa kichwa hata kuuawa mana watafuta pesa kwa njia haramu kama hizo hawana cha kupoteza.

Huyo mpangaji wako hapitagi huku JamiiForum?
 
Ukikurupuka umeisha watakutaifisha uhai wako mapema sana, nenda kwa hatua soma ushauri humu utakaokufaa pita nao
 
Njia pekee ni kutoa taarifa polisi, TBS, takukuru,TRA na kwa wazalishaji wa pombe husika. Kosa ulikofanya ni kuja mtandaoni na kwa kufanya hivyo utakuwa umempa alert na ataondoa ushahidi wote. By the time vyombo husika vina act hawatapata kitu na utaonekana mzushi na kubakia na uhasama na mpangaji wako.
 
Kwa usalama subiri Kodi iishe ahame Kwa Amani hv unajua hasira za kukatiwa mrija wa pes
Acha uboya ww.

Akae miaka miwili kusubiri Kodi iishe kweli? Kwaiyo kipindi chote IKO akae Kwa mashaka?

Hiyo Ni kesi mbaya mzee, Ni lazma hatua za haraka zichukuliwe.
Iwe Kwa kuongea na mpangaji wake ili ahame, au kutoa taarifa mamlaka zinazohusika.

Ila Kwa vyovyote hapaswi kuogopa wala kusubiri chochote. Unakuta iyo nyumba amejenga Kwa tabu then Iuje itaofishwe na serikali kiboya tu Tena haina ATA mwaka.
 
Njia pekee ni kutoa taarifa polisi, TBS, takukuru,TRA na kwa wazalishaji wa pombe husika. Kosa ulikofanya ni kuja mtandaoni na kwa kufanya hivyo utakuwa umempa alert na ataondoa ushahidi wote. By the time vyombo husika vina act hawatapata kitu na utaonekana mzushi na kubakia na uhasama na mpangaji wako.
Sasa angepataje mawazo Kama haya Bila kuja mtandaoni, sababu inaonekana Ni suala linalomuumiza kichwa.
 
Acha uboya ww.

Akae miaka miwili kusubiri Kodi iishe kweli? Kwaiyo kipindi chote IKO akae Kwa mashaka?

Hiyo Ni kesi mbaya mzee, Ni lazma hatua za haraka zichukuliwe.
Iwe Kwa kuongea na mpangaji wake ili ahame, au kutoa taarifa mamlaka zinazohusika.

Ila Kwa vyovyote hapaswi kuogopa wala kusubiri chochote. Unakuta iyo nyumba amejenga Kwa tabu then Iuje itaofishwe na serikali kiboya tu Tena haina ATA mwaka.
Boya mwenyewe ulikuwa na ulazima wa kunijb kwani ww ndo mtoa mada tafuta wa kukukuna
 
Back
Top Bottom