Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,843
- 31,057
Kwa namna huyu "Jasusi mbobezi" Bernard Kamilius Membe, anavyoendelea kushika "chart" humu kwenye mitandao ya kijamii, ni dhahiri kuwa huko kwenye hicho chama, wanachodai wenyewe kuwa ni chama kikubwa, hivi sasa kunatokota na sisi wananchi tusubiri, kwa kuwa yajayo yanafurahisha au kukarahaisha...
Membe ametoa madai mazito sana kuwa Katiba ya CCM haikufuatwa katika kufukuzwa kwake ndani ya Chama
Kwani amedai kuwa ni takwa la kikatiba, anapofukuzwa kiongozi yeyote wa ngazi za juu katika chama hicho ni LAZIMA jambo lake lingejadiliwa ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM, ndipo uamuzi ufikiwe.
Jambo ambalo halikufanyika katika kufikia uamuzi wa kufukuzwa kwake. Kwani mwenyewe anadai kuwa "process" ilikuwa haijakamilika, kwa kuwa kikao kilichomjadili kilikuwa ni kikao cha Kamati Kuu pekee, wakati mchakato ulikuwa haujakamilika, kwa kuwa kikao chenye uamuzi wa mwisho, ambacho ni kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM, kilikuwa hakijakaa.
Jambo linaloshangaza ni kuwa tokea madai hayo yatolewe na Membe, hakuna kiongozi yeyote wa ngazi ya juu wa CCM, aliyejitokeza kujibu tuhuma hizo
Kwa madai mazito kama hayo, ni kwanini hadi sasa chama cha CCM, kimeamua kukaa kimya, kisitoe majibu yoyote, kwa madai hayo ya Membe?
Inaelekea kuna mfukuto mkubwa sana huko kwa majirani zetu wa CCM
Ni dhahiri sasa kama alichoongea mwenyewe Membe, kuwa tufanye subira kati ya mwezi huu wa June hadi October ya mwaka huu, lolote lisilotegemewa na wananchi wengi litatokea katika nchi hii na litaleta kishindo kikubwa sana!
Subira yavuta kheri, ngoja tusubiri ili tuyashuhudie yatakayojiri
Membe ametoa madai mazito sana kuwa Katiba ya CCM haikufuatwa katika kufukuzwa kwake ndani ya Chama
Kwani amedai kuwa ni takwa la kikatiba, anapofukuzwa kiongozi yeyote wa ngazi za juu katika chama hicho ni LAZIMA jambo lake lingejadiliwa ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM, ndipo uamuzi ufikiwe.
Jambo ambalo halikufanyika katika kufikia uamuzi wa kufukuzwa kwake. Kwani mwenyewe anadai kuwa "process" ilikuwa haijakamilika, kwa kuwa kikao kilichomjadili kilikuwa ni kikao cha Kamati Kuu pekee, wakati mchakato ulikuwa haujakamilika, kwa kuwa kikao chenye uamuzi wa mwisho, ambacho ni kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM, kilikuwa hakijakaa.
Jambo linaloshangaza ni kuwa tokea madai hayo yatolewe na Membe, hakuna kiongozi yeyote wa ngazi ya juu wa CCM, aliyejitokeza kujibu tuhuma hizo
Kwa madai mazito kama hayo, ni kwanini hadi sasa chama cha CCM, kimeamua kukaa kimya, kisitoe majibu yoyote, kwa madai hayo ya Membe?
Inaelekea kuna mfukuto mkubwa sana huko kwa majirani zetu wa CCM
Ni dhahiri sasa kama alichoongea mwenyewe Membe, kuwa tufanye subira kati ya mwezi huu wa June hadi October ya mwaka huu, lolote lisilotegemewa na wananchi wengi litatokea katika nchi hii na litaleta kishindo kikubwa sana!
Subira yavuta kheri, ngoja tusubiri ili tuyashuhudie yatakayojiri