Pacbig
JF-Expert Member
- Oct 15, 2017
- 1,095
- 2,087
Nilianza mahusiano na huyu binti mwaka juzi mwezi wa kumi na mbili. Mwaka 2019 Nikiwa semester ya mwisho kabla ya kumaliza chuo nilipata supplementary ambayo mwalimu alichelewa kutoa matokeo, akaja kutoa siku moja kabla ya graduation hivyo jina langu halikuwepo kwenye list ya graduates iliyopitishwa na senate. Nikaambiwa niandike barua then nitaingizwa kwenye list mwaka unaofuata.
Ulipita mwaka mzima, siku chache kabla ya graduation ya mwaka uliofuata ambao ndio nilipaswa sasa nigraduate ilitoka list ya mwaka huo lakini jina langu halikuwepo. Ikanibidi niende chuoni kufuatilia.
Nilipofika chuoni na kuanza kufuatilia ndipo nilipokutana na binti huyu. Kiufupi yeye na mimi tulikuwa kwenye the same scenario na yeye hakuwemo kwenye list pia. Tulikutana kama bahati tu nikiwa kwenye kundi la watu nje ya ofisi ya head of department ambaye hakuwemo ofisini, nilishangaa binti mmoja mchangamfu ananifata moja kwa moja akiwa amenyoosha simu yake akanipatia na kuniambia
"Ongea na head of department mwambie tunamsubiri huku ofisini mimi naogopa"
Niliipokea ile simu na huo ndio ukawa mwanzo wa kujuana. Tulibadilishana mawasiliano na baadaye mahusiano yakazaliwa. Nilimpenda sana yule binti ukizingatia sikuwahi pata binti mzuri na smart kama yule maishani mwangu. Kwa bahati nzuri alipata kazi mkoa wa nyumbani kwetu ambako mimi pia ndio ninaishi. Ila yeye akawa anakaa wilayani mimi nakaa mjini. Kuna siku nikiwa kaka yangu yangu ambaye yuko likizo home huyu binti alinipigia na katika maongezi akaniuliza uko na nani nikamjibu niko na kaka yangu akasema hebu mpe simu nimsalimie sikuona shida nikampa wakaongea ila maongezi yalikuwa ya kawaida tu. Niwe muwazi hapa huyu kaka yangu huwa simpendi kihivyo kwa sababu ana tabia ya kuniongelea vibaya hivyo namheshimu tu kwa sababu ni ndugu.
Sasa juzi kuna shosti yake na huyu binti wanafanya kazi sehemu moja alinitumia picha whatsapp ambayo ni ya kaka yangu na kuniuliza kama ninamfahamu, nikamwambia huyo ni kaka yangu je picha yake umeitoa wapi? akajibu amenionyesha Frida (sio jina halisi) ambaye ndio huyo mpenzi wangu. Nilipata mashaka yeye na kaka yangu wamefahamiana vipi wakati wameongea kwa simu tu. Kiukweli mimi huwa sina tabia ya kumuamini mtu yeyote mpaka hapo nikahisi kuchapiwa. Nikawa namfatilia bro kimachale. Kuna siku bro alikuwa anaongea nje ya nyumba na simu nikamfatilia lakini katika maongezi nikabaini anaongea na huyu huyu binti. Usiku wa jana mida ya saa mbili ndio nimeona txt kwenye simu ya bro simu ikiwa lock ila ikaingia txt ya namba ya huyu binti. Txt inasema nanukuu
" Kweli bora niachane nae tu"
Nimemuuliza rafiki yake aliyenitumia picha hajafunguka ila kaniambia tu
" hayo ndio maisha Pacbig"
Nimeumia sana sijajua hata cha kufanya ila I think this is going to be the end of our brotherhood between me and my brother, I hate him more than I hate a devil.
Ulipita mwaka mzima, siku chache kabla ya graduation ya mwaka uliofuata ambao ndio nilipaswa sasa nigraduate ilitoka list ya mwaka huo lakini jina langu halikuwepo. Ikanibidi niende chuoni kufuatilia.
Nilipofika chuoni na kuanza kufuatilia ndipo nilipokutana na binti huyu. Kiufupi yeye na mimi tulikuwa kwenye the same scenario na yeye hakuwemo kwenye list pia. Tulikutana kama bahati tu nikiwa kwenye kundi la watu nje ya ofisi ya head of department ambaye hakuwemo ofisini, nilishangaa binti mmoja mchangamfu ananifata moja kwa moja akiwa amenyoosha simu yake akanipatia na kuniambia
"Ongea na head of department mwambie tunamsubiri huku ofisini mimi naogopa"
Niliipokea ile simu na huo ndio ukawa mwanzo wa kujuana. Tulibadilishana mawasiliano na baadaye mahusiano yakazaliwa. Nilimpenda sana yule binti ukizingatia sikuwahi pata binti mzuri na smart kama yule maishani mwangu. Kwa bahati nzuri alipata kazi mkoa wa nyumbani kwetu ambako mimi pia ndio ninaishi. Ila yeye akawa anakaa wilayani mimi nakaa mjini. Kuna siku nikiwa kaka yangu yangu ambaye yuko likizo home huyu binti alinipigia na katika maongezi akaniuliza uko na nani nikamjibu niko na kaka yangu akasema hebu mpe simu nimsalimie sikuona shida nikampa wakaongea ila maongezi yalikuwa ya kawaida tu. Niwe muwazi hapa huyu kaka yangu huwa simpendi kihivyo kwa sababu ana tabia ya kuniongelea vibaya hivyo namheshimu tu kwa sababu ni ndugu.
Sasa juzi kuna shosti yake na huyu binti wanafanya kazi sehemu moja alinitumia picha whatsapp ambayo ni ya kaka yangu na kuniuliza kama ninamfahamu, nikamwambia huyo ni kaka yangu je picha yake umeitoa wapi? akajibu amenionyesha Frida (sio jina halisi) ambaye ndio huyo mpenzi wangu. Nilipata mashaka yeye na kaka yangu wamefahamiana vipi wakati wameongea kwa simu tu. Kiukweli mimi huwa sina tabia ya kumuamini mtu yeyote mpaka hapo nikahisi kuchapiwa. Nikawa namfatilia bro kimachale. Kuna siku bro alikuwa anaongea nje ya nyumba na simu nikamfatilia lakini katika maongezi nikabaini anaongea na huyu huyu binti. Usiku wa jana mida ya saa mbili ndio nimeona txt kwenye simu ya bro simu ikiwa lock ila ikaingia txt ya namba ya huyu binti. Txt inasema nanukuu
" Kweli bora niachane nae tu"
Nimemuuliza rafiki yake aliyenitumia picha hajafunguka ila kaniambia tu
" hayo ndio maisha Pacbig"
Nimeumia sana sijajua hata cha kufanya ila I think this is going to be the end of our brotherhood between me and my brother, I hate him more than I hate a devil.