Mpenzi wangu anapenda kutumia lugha ngumu

Ndugu ,mapenzi Yana nguvu sana kikubwa yawe mapenzi ya kweli sio ulaghai ,kwa hapo yote yanawezekana .
Uliwahi safiri umbali gani kumfuata binti ? Je ilikuwa ni nguvu ya Nini kaa ?
EHehehehw..nishawahi kwenda tabora mimi toka Dar kwaajili ya Manzi. πŸ˜‚πŸ˜‚.
 
Simaanishi alegeze ulimi ila nkimuita romantic names bas naye arespond vizuri sio kuniita mwamba!
Tehee hee hee sure nakuelewa mkuu kukuita "mwamba" inaukakasi jamaa yaonekana amezoea lugha ngumu, unaweza kumshawishi kupunguza ukali au usela japo KUA MAKINI SANA kwani anaweza kuitafsiri hatua hiyo ya kushauri kama umemuona mhuni.

Meanwhile mvumilie na ukimshawishi taratiiiiiiiiiiiiiiiiibu sana waweza kumwambia " natamini uniite 1,2,3" na siku akikuita hiyo onyesha kufurahi hii itamfanya abadilike. (Wanaume tunapenda kuwafurahisha wale tuwapendao)
 
EHehehehw..nishawahi kwenda tabora mimi toka Dar kwaajili ya Manzi. πŸ˜‚πŸ˜‚.
Basi rafiki ,kwa lugha za kiume tutasema ulienda kupata tendo lakini uhalisia haikuwa kufuata penzi Ila ni mapenzi yalikujaa ndiyo ikawa safari maana hauwezi mfuata mtu ikiwa haujampenda .
Ndivyo nisemavyo ni rahisi sana kumbadili mtu anayekupenda na vise versa is true
 
Sawa shukrani
 
Wala hata sikufuata tendo. Nilikua nampenda tu. Yan imagine, mimi nasoma Dar yeye yuko Tabora na makaz ni Dar, ila akifunga chuo mimi ndio natika Dar kwenda Tabora nimsindike kurud Dar.. πŸ˜‚πŸ˜‚.
Mapenzi ni ya kifala sanaaa.
Nilikuaga sina akil sijui.??!!!

Maana nikikumbuka niliokua nayafanya those 10 yrs ago, kwakwel nabak najicheka sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…