Mpinga Hayati Magufuli aangua kilio ndani ya treni ya SGR

Mpinga Hayati Magufuli aangua kilio ndani ya treni ya SGR

Etwege

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2018
Posts
7,207
Reaction score
17,674
Tarehe 4, july, 2024 nikiwa kwenye treni ya umeme (SGR)ya Dar - Morogoro ambapo abiria wanatumia saa moja na dakika 49 tu kufika, hivyo kuokoa muda mwingi wa uzalishaji uliokuwa unapotea barabarani kwenye foleni, kwenye siti pembeni yangu alikaa kijana ambaye kwa muonekano yupo umri wa above 25 ambaye muda wote alionekana mwenye huzuni sana na majuto mengi.

Baada ya kufika kituo cha Soga mkoani Pwani nikamuona kijana ameanza kuangua kilio na ndipo ilibidi nimuhoji na abiria wenzangu wakataka kujua ni nini kinamsibu kijana huyu, kijana alieleza kuwa nafsi inamsuta kupanda hii SGR kwani alipinga ujenzi wake akiongozwa na Tundu Lisu na Chadema kwa ujumla alishiriki kumtukana hayati Rais Magufuli na kumkejeli pale alipoanzisha ujenzi wa reli ya umeme wakati huo ikiwa awamu ya tano!

Kijana anasema sasa analia na kusaga meno kwani Magufuli hayupo tena duniani na hajui atamuombea wapi msamaha ili nafsi yake iwe huru kwani mradi wa sgr Dar - Moro umekamilika na kuwa wenye manufaa makubwa kwa watanzania masikini na matajiri bila kujali vipato vyao.

My take

Kwa maoni yangu vijana wa namna hii wako wengi wanapanda ndege, treni, flyover na kuwasha umeme wa bwawa huku nafsi zao zinawasuta sana maana walidanganywa na wanasiasa matapeli wasio na maono wala uzalendo wowote kwa taifa la Tanzania wakaishia kumtukana hayati Magufuli kwamba ni mshamba badala ya kutumia nguvu zao kuungana na Magufuli kujenga nchi wao wakatumia nguvu zao kumtukana na sasa wanajuta.
 
Mbona Lissu aliziita ndege panga boy na anazipanda?

Hawa wanasiasa wakati mwingine wakikuambia jambo,

Changanya na akili zako!!
Nyumbu huwa hawachanganyi na zao kabisa, wanafuata mkumbo tu. Umewahi kuwaona wanavyovuka mto Mara? Mmoja akishatumbukia kwenye maji, na wengine wote wanafuata, bila kujali hata kama kiongozi wao ataliwa na mamba!
 
Nyumbu huwa hawachanganyi na zao kabisa, wanafuata mkumbo tu. Umewahi kuwaona wanavyovuka mto Mara? Mmoja akishatumbukia kwenye maji, na wengine wote wanafuata, bila kujali hata kama kiongozi wao ataliwa na mamba!
Mimi nilikataa mwanasiasa kunishikia akili zangu.

Penye Kweli nitasema, na penye hadaa nitapinga macho wazi!!
 
..mimi nilimpinga Magufuli kununua midege.

..midege inatuletea hasara ambayo hatukupaswa kuibeba.

..pamoja na hayo nitapanda Atcl ilimradi inanifikisha ninapotaka kwenda.

..pia nilipinga ujenzi wa mji Mkuu Dodoma. Fedha na rasilimali zilizotumia Dodoma zingeweza kufanya mambo mengi yenye tija.

..mtizamo wangu haunizuii kutembelea Dodoma.
 
Kumetokea niji treni ya sgr inaingia muda huu Morogoro
 
Mimi Jiwe nilimpenda kwa YOTE isipokuwa nilimchukia kwa jinsi alivyokuwa akionea wafuasi wa vyama vya upinzani na kuwafunga magerezani kwa kesi za kutengenezwa!
Watu waliuawa,waliopona walikuwa wamefanywa vilema!
Aloo! Yule jamaa hapana aise kama ni kuinyosha nchi aliinyosha kikweli kikweli.
Hata hivyo Rest in Peace Magu kwa sababu ya Uchapakazi (Hapa Kazi tu) uliouonyesha.
 
Back
Top Bottom