Mpinzani halisi wa Alikiba ni MarLaw, sio Diamond...

Diamond hakuna wakushindana nae Tanzania na hatatokea kamwe ko wewe alikiba kaa na hiyo miaka 40+ ukauze nguo kariakooo ebooooooh.
 
I am afraid you misinterpreted the message here. Please take your time up, and read again.
 
Umeona Uzi wako utachacha Bila kumtaja diamond platnumz si ungezungumzia huyo marlaw na alikiba Bila kumuhusisha msanii wa kimataifa diamond watu wangekuelewa
Ali Kiba na Diamond ndio big names kwenye industry hivi sasa. Hata nisingemtaja Diamond, kuna watu wangekuja kumtaja tu humu. Hakwepeki!
 
Write your reply...ni kweli Daimond sio wakufananisha au kumlinganisha na na mwanamuziki yeyote ndani ya Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla,,,
Mwache alikiba ashindanishwe na Marlow
Hoja sio Ali Kiba au Marlaw ni bora kuliko Diamond..

Hoja ni Marlaw ndiye mshindani halisi wa Alikiba. Sio Diamond.

Sababu nimezieleza vizuri tu!
 
Kumshindanisha Diamond na mwanamziki yoyote Tanzania ni ujinga, si kwa waliopo au waliokuwepo. Bahati nzuri mi ni mtu wa zamani, najua wale wa zamani na wa sasa.
Ukiweka ushabiki pembeni, kuna wale wasiojua biashara ya muziki(showbiz) wanabaki kusema Diamond alikuwa zamani enzi za "nenda kamwambie" and the likes lakini hawajui dogo amebadilika kulingana na soko, internationally na local(kwa wale wa amsha amsha), muziki wa kuchezeka na ambao unaweza kumfurahisha hata asuyejua Kiswahili.
Kwa sisi tunaoishi na watu wasiojua Kiswahili hauwezi kumshawishi mtu asikilize nyimbo za kina Kiba/Marlaw ambazo wanaimba visauti kama wanaimba taarabu, hakuna mwenye uelewa wa kinachoimbwa na haiwezekani ukamshawishi apende nyimbo za aina hiyo.
Kuwashindasha Kiba na Marlaw inaweza kuwa sawa lakini kumtaja, I mean hata kumtaja tu Diamond katika wanamuziki wa level hizo ni makosa na ni kama kunakuwa na makusudi flani kwani ndiye mtu anayepaisha jina la Tz internationally katika sekta ya burudani.
Angalia fans hata maoni tu popote kwenye social media, angalia impact ya shows zake, angalia endorsements na matangazo na vyote hivi havikuja kwenye silver plate bali ni matunda ya mafanikio katika biashara ya burudani(kuimba vizuri, kujibranda vizuri, kumantain kwenye level ya juu kwa muda mrefu, kufanya kazi kwa bidii, kushikamana na timu yake bila ya majivuno kujiona yeye ndiyo kila kitu).
Hawa nyota wengine wa muziki(Bongo flavour) wangekuwa kiwango cha Diamond hata kufanya nao interview ingekuwa ni shida, kuwa humble pia kunambeba sana, kuushikilia ule Utandale kunamsaidia pia ndiyo diehard fans wake asilimia kubwa ni wale wa uswazi.
Wa kushindanishwa locally waendelee, nyota wanaopaisha jina la nchi kimataifa washindanishwe/walinganishwe na international artists.
 
Ali Kiba na Diamond ndio big names kwenye industry hivi sasa. Hata nisingemtaja Diamond, kuna watu wangekuja kumtaja tu humu. Hakwepeki!
Usingemtaja ili watakaomtaja uwakosoe uwaambie uzi ni wa Ali Kiba na Marlaw, nadhani waliosema umemtaja Diamond ili uzi upate mvuto wana point hapo.
 
Una mawazo mazuri lakini umeteleza kudhani muziki mzuri unatokana na lugha.

Wahindi wana nyimbo nzuri na zinatamba almost dunia nzima na watu hawaelewi hata wanachoimba. Wakongo na wale kina Despacito vile vile.

Hayo mengine ya kusema Diamond ni mkali kuliko wasanii wengine sio lengo la uzi huu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…