Mr. Blue na Baki na Mimi

Mr. Blue na Baki na Mimi

Fid anajua sana, tatizo hajui kufreestyle...ndo maana nimeamua kumkubali MBISHI badala ya fid.
mkuu hata Pac free style amna kitu....Jay Z ndio kabisa sifuri na hao pia huwakubali?!
 
blue ni mkali ila Baki na Mimi amna kitu...ni wimbo wa kawaida mno
 
Nampenda Mr. Blue,
Msanii pekee asiyechuja,
Msanii anayewika bila dili la matangazo,
Hana rafiki Paparazi ili jina lake liwe juu.

Kiufupi Blue hata aimbe Mabata madogo madogo me nitapenda na nitaimba nae.
...wapigie wazazi wako wambie uko na mimi! .....
 
blue ni habari nyengne namkubali kweli, kwa namkubali kwa ile stail ya kipekee namkubali sana
 
Blue ni kati ya wasanii tallented kupata kutokea kwenye game ya bongofleva, anauwezo mkubwa wa kurap na kuimba, huyu ni jamii za kina Ngwea. Furaha tele,....tele, wambie wakina... Leo siku ya vigelegele...
Mr umemaliza. Uko sahihi kabisa. Bongofleva wengi ni ama kuimba tu au Kuchana tu lakini Blue kama alivyokuwa Ngwea (R.I.P) anakupa vyote. Iwe ngoma za kibishoo au za kisela kama za BoB micharazo zote anaweza. Yuko vizuri.
 
Blue ni mfano wa wasanii wachache walioweza kulinda heshima yao kwenye game tangu wanatoka hadi leo, tofauti na wale waliovuma na kushindwa kurudi kushika namba.

Aina ya wasanii walioweza kukamata kitambo na mpaka leo wakishindana na watoto wa sasa ni:

Blue

Fid q

Professor j

Nyandu toz

Joh makin

Kiba

Diamond

Hao ni mfano tu ila wapo wengi waliotamba kwa nyakati zao ila mpaka leo wapo kwenye chati.

Afande Sele aliwahi kuulizwa kuwa kwa nini Blue na Diamond wanajiita simba wakati yeye ndiye anaetambulika kama simba zee, akajibu......wanastahili kujiita hivyo kwa kuwa simba ni mpambanaji na wao wamepambana na kupendwa tangu nyimbo zao za mwanzo mpaka leo wanakamata soko
 
Kijana akiwa na familia yake
9681fe5f6953cd3d676a668d8792e696.jpg
6c66198791656f2ab59ea953a4e13a41.jpg
ea0d79ad5affd464ed60ea3f63db3908.jpg
ad6601ca0294cad12c3b83196638b2c6.jpg
987041d1dcce8b1fdc5015d2007da1c1.jpg
e7af63715bdc69f4f943b8bcc09e343f.jpg
87a406b0b9f32c791bcef70e5db3da1d.jpg
 
Ni kweli matusi sikatai angeimba mwingine isingesikika sababu Blue ana swagger zake zilizopelekea nyimbo ibambe...
Ana style za kipeke yake sana. Namkumbuka huyu dogo tangu anaimba freestyle hana hata singo 1.ali washaghairi moto siku moja pale vijana club sio mango balaa. Kulikua na mashindano ya rap.
Ilikua 1999-2000 hivi
 
Inasemekana Blue alikuwa inspired kufanya mziki na kaka zake wakubwa. Cha ajabu hao wakubwa zake sijawahi kuwaona wala kuwaskia.
 
Back
Top Bottom