Haka kaugonjwa wacha tu tukasikie kwa mwingine, wengi walioathirika wanateseka sana kisaikolojia.
Issue ya Unyanyapaa ndio unawaumiza sana waathirika. Na wengi wanaangamia kwa sababu wanajificha sana kuhusu Afya zao.
Takwimu za Tanzania zinaonyesha 3% ya watanzania wameathirika. Hiyo ni idadi kubwa sana kwa ugonjwa wa Kuambukiza, ina maana mtu yoyote anaweza akaambukizwa popote pale hapa Tanzania.
Katika kila Dakika 15 kuna mtanzania mmoja anagundulika kwa mara ya Kwanza kupata maambukizi, mbali na juhudi zote zilizofanywa kupambana na Ugonjwa huu kwa miaka zaidi ya 30.
[HASHTAG]#TUWE[/HASHTAG] WAANGALIFU.