Ukisha gundulika kuwa uko positive unaanza initial assessment, ambayo sasa wanachukua damu kuangalia kiwango cha CD4 kwenye mwili wako, dawa gani itareact na damu yako, uzito, urefu, blood pressure, hivi vinafanywa na nesi. Baada ya hapo unapewa appointment ya kuonana na daktari baada ya wiki mbili, wakati huo majibu ya damu yanakuwa yamerudi na daktari atajua dawa gani inaendana na tiba yako. Kwa siku za kwanza utapewa appointment nyingi, inawezekana urudi tena baada ya wiki 6-8 hii ni kuangalia kama huna reaction na dawa, kama kuna reaction unaweza kubadilishiwa dawa.
Hali ikistablelize na wakiona una comply na treatment, basi utakuwa unaonwa mara moja baada ya miezi sita au mwaka, lakini unaambiwa kabisa ukiwa na tatizo unaweza kwenda saa yeyote. Tatizo ni wale wa methadone na walevi kupitiliza pia wale wanaokunywa dawa kwa wasiwasi watu wasijue, wanakosa privacy au wanasahau kunywa dawa consistently na hivyo ni vigumu kumaintain viral suppression level.