Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,487
- 13,611
Niliusoma ule ujumbe wa waziri wa mambo ya nje wa Marekani kumhusu mkuu wa mkoa wa Dar juu ya watu kudhulumiwa haki ya kuishi, kichwani mwangu zikaja kila aina ya fikra. Zilikuwa ni tuhuma nzito zilihitimishwa kwa RC wa Dar kunyimwa haki ya kuingia Marekani.
Lakini kesho hakuna binadamu aijuaye namna inavyofanana. mapolisi wa Minneapolis wamemnyanyasa na kumnyima haki ya kuendelea kuishi George Floyd akiwa ni kijana wa miaka 46. Dunia nzima imeona tukio lote lililovyokuwa kwanza likirekodiwa na kamera za CCTV za jengo moja na pili kwa video fupi jongevu iliyochukuliwa na mpita njia.
Maandamano yanaendelea ulimwengu mzima, hasira zimewawaka watu wa kila rangi, watu weusi wakiwa ndio viongozi wa maandamano. Kule Uingereza wananchi wanaiangusha minara yenye kusimama kama kielelezo cha biashara za kitumwa.
Wamarekani wanabeba mabango yenye maandishi yasemayo DEFUND POLICE yaani bajeti zinazotengwa kwa ajiii ya polisi na zipitiwa upya, wengine wanashauri mifumo ya utendaji kazi ya polisi na yenyewe ipitiwe upya.
Siku zote kauli huwa zinaumba, Donald Trump na msaidizi wake Pompeo hawajifunzi lolote kuhusiana na hekima hii ya miaka na miaka, kwao kuongea mambo bila kuangalia madhara yake sio kitu muhimu.
Wenye kudhulumu haki ya kuishi ni polisi wa Marekani, kwani dhuluma yao inasababisha ulimwengu mzima kuandamana. Dhuluma ya Marekani ni mbaya sana kwani ni ya miaka na miaka, kule kwenye majimbo ya kusini yenye weusi wengi kumekuwa na sehemu ambazo mtu mweusi haruhusiwi kuvuka. Akithubutu basi haki yake ya kuishi inakuwa imechukuliwa bila ya ridhaa yake.
Yale maandishi ya Pompeo yenye kumuongelea RC wa Dar namna anavyodhulumu haki ya kuishi yamemgeuka yeye na bosi wake. Wao ndio wenye kudhuluma haki za watu za kuishi tena ni utamaduni wao kwa miaka zaidi ya mia nne.
Lakini kesho hakuna binadamu aijuaye namna inavyofanana. mapolisi wa Minneapolis wamemnyanyasa na kumnyima haki ya kuendelea kuishi George Floyd akiwa ni kijana wa miaka 46. Dunia nzima imeona tukio lote lililovyokuwa kwanza likirekodiwa na kamera za CCTV za jengo moja na pili kwa video fupi jongevu iliyochukuliwa na mpita njia.
Maandamano yanaendelea ulimwengu mzima, hasira zimewawaka watu wa kila rangi, watu weusi wakiwa ndio viongozi wa maandamano. Kule Uingereza wananchi wanaiangusha minara yenye kusimama kama kielelezo cha biashara za kitumwa.
Wamarekani wanabeba mabango yenye maandishi yasemayo DEFUND POLICE yaani bajeti zinazotengwa kwa ajiii ya polisi na zipitiwa upya, wengine wanashauri mifumo ya utendaji kazi ya polisi na yenyewe ipitiwe upya.
Siku zote kauli huwa zinaumba, Donald Trump na msaidizi wake Pompeo hawajifunzi lolote kuhusiana na hekima hii ya miaka na miaka, kwao kuongea mambo bila kuangalia madhara yake sio kitu muhimu.
Wenye kudhulumu haki ya kuishi ni polisi wa Marekani, kwani dhuluma yao inasababisha ulimwengu mzima kuandamana. Dhuluma ya Marekani ni mbaya sana kwani ni ya miaka na miaka, kule kwenye majimbo ya kusini yenye weusi wengi kumekuwa na sehemu ambazo mtu mweusi haruhusiwi kuvuka. Akithubutu basi haki yake ya kuishi inakuwa imechukuliwa bila ya ridhaa yake.
Yale maandishi ya Pompeo yenye kumuongelea RC wa Dar namna anavyodhulumu haki ya kuishi yamemgeuka yeye na bosi wake. Wao ndio wenye kudhuluma haki za watu za kuishi tena ni utamaduni wao kwa miaka zaidi ya mia nne.