Mradi gani wa kiuchumi unaweza kuanzisha kwa kutumia fedha za mafao kiasi cha Tshs 90,000,000/-?

Mradi gani wa kiuchumi unaweza kuanzisha kwa kutumia fedha za mafao kiasi cha Tshs 90,000,000/-?

Wana JF habari zenu,

Mama yangu baada ya kunusurika na kikotoo ameniomba nimshauri kumpendekezea mradi ambao anaweza akaanzisha na kuusimamia yeye mwenyewe, pesa anazotegemea kupata ni Tshs. 94,000,000.

Fedha anayotegemea kuanzishia mradi ni tshs 90,000,000.

Nimeona ni vyema kuwashirikisha kupata mawazo mbadala, pkwa kuwa ninaamini baadhi yetu wazazi wetu walistaafu na kuanzisha miradi ambayo imekuwa imara na endelevu mpaka sasa.
Mkuuu miradi inayohusu Ujenzi wa Majengo haijawahi kumliza mtu kama umenunua kiwanja sahihi.
JENGA GUEST HOUSE DODOMA.
Kamnunulie Kiwanja eneo la Mjini pale Dodoma Mil 25. Anza ujenzi wa Gesti ya vyumba 10 ambayo utatumia takribani Milioni 60. Baada ya happo ni kukusanya noti kwa kwenda mbele kwa Wabunge na Serikali kwa ujumla baada ya wimbi la kuhamia Dodoma kushika kasi. Nakuhakikishia Guest Dodoma hailali tupu hata iwejeeee! Ukitaka uzoefu zaidi usissite kuniPm ni bure kabisaaaa mkuu. Hongereni
 
Kama hajawahi kufanya boashara yeyote ile, risk ya kuanza na 90m ni kubwa mno. Ni vizuri aanza na mradi utakaotumia mpaka mil 45.
Hakika kama hajawahi kufanya biashara, ni vyema kajenga jengo la bishara, weka fremu kadhaa, anahakika kila mwezi atapata chochote kitu

Au ajenge nyumba simple ya kupangisha maeneo ya mji kidogo, Hakika hatokosa fedha ya kula
 
Wana JF habari zenu,

Mama yangu baada ya kunusurika na kikotoo ameniomba nimshauri kumpendekezea mradi ambao anaweza akaanzisha na kuusimamia yeye mwenyewe, pesa anazotegemea kupata ni Tshs. 94,000,000.

Fedha anayotegemea kuanzishia mradi ni tshs 90,000,000.

Nimeona ni vyema kuwashirikisha kupata mawazo mbadala, pkwa kuwa ninaamini baadhi yetu wazazi wetu walistaafu na kuanzisha miradi ambayo imekuwa imara na endelevu mpaka sasa.
Hakuna mstaaf aliyewahi kutajirika kwa pension.
Mwambie ale kidogo kidogo. Nyingine awagawie.
 
Wana JF habari zenu,

Mama yangu baada ya kunusurika na kikotoo ameniomba nimshauri kumpendekezea mradi ambao anaweza akaanzisha na kuusimamia yeye mwenyewe, pesa anazotegemea kupata ni Tshs. 94,000,000.

Fedha anayotegemea kuanzishia mradi ni tshs 90,000,000.

Nimeona ni vyema kuwashirikisha kupata mawazo mbadala, pkwa kuwa ninaamini baadhi yetu wazazi wetu walistaafu na kuanzisha miradi ambayo imekuwa imara na endelevu mpaka sasa.
Mwambie aweke hio hela NMB awe anapokea laki 7.5 kila mwezi. Its a risk free business kuliko ku risk kama hajawahi fanya kabisa biashara yeyote!
 
Kama mtu afahamu maana ya kuwekeza pesa na kupata pesa kwa muda msimpe ushauri huyu ndugu, maana fursa hazina formula zinataka kupambana.... Sasa nasikia mtu anamwambia eti ajenge guest house mjini kwa milioni 60
 
Kama mtu afahamu maana ya kuwekeza pesa na kupata pesa kwa muda msimpe ushauri huyu ndugu, maana fursa hazina formula zinataka kupambana.... Sasa nasikia mtu anamwambia eti ajenge guest house mjini kwa milioni 60
Tena ya vyumba kumi mjini.
 
Mkuuu miradi inayohusu Ujenzi wa Majengo haijawahi kumliza mtu kama umenunua kiwanja sahihi.
JENGA GUEST HOUSE DODOMA.
Kamnunulie Kiwanja eneo la Mjini pale Dodoma Mil 25. Anza ujenzi wa Gesti ya vyumba 10 ambayo utatumia takribani Milioni 60. Baada ya happo ni kukusanya noti kwa kwenda mbele kwa Wabunge na Serikali kwa ujumla baada ya wimbi la kuhamia Dodoma kushika kasi. Nakuhakikishia Guest Dodoma hailali tupu hata iwejeeee! Ukitaka uzoefu zaidi usissite kuniPm ni bure kabisaaaa mkuu. Hongereni
Mkuu mbona mahesabu yanagoma kichwani mwangu,Dodoma mjini unaweza ukajenga gesti ya vyumba kumi yenye hadhi ya kulala waheshimiwa uchwara wetu kwa milioni sitini.
 
Najua mnaishi mjini sana..mwambie atafute eneo kubwa ajenge nyumba nyingine pembezeni kidogo ya mji ambayo mtahamia kuishi huko..iyo nyumba ya mjini aikarabati katika mfumo iwe nyumba ya kupangisha ikiwezekana ajenge na nyumba nyingine hapohapo mjini palipochangamka iwe ya kupangisha so jumla ya nyumba zenye wapangaji mtakuwa nazo mbili hapo kila mwezi atakuwa anapata kodi..huko mtakapohamia etenge eneo kubwa kwa ajili ya ufugaji ng'ombe na kuku ikiwezekana na mifugo mingine alafu atafute kijana kutoka kijijini kwa ajili ya kuhudumia iyo mifugo na ambae atakuwa anamsaidia kuuza hizo bidhaa zitokanazo na mifugo kama maziwa..mayai..etc...kwa kuwa mama umri umeenda kama kuna visenti kidogo vitabaki hapohapo nyumbani mtakapohamia aweke duka la bidhaa za nyumbani so hapo ndo itakuwa sehemu yake ya kupiga Story na kupata hela ndogondogo...ukifuata huu ushauri najua kuna siku utanitafuta unishukuru
Respect

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hilo nalo neno japo watoto nao wafaidi matunda ya mama kidogo

Namshukuru mama yetu

Alitugawia 5M each tupo 3

Na 1M each ya kwenda kula Bata Ngorongoro.


Yeye hajataka kupata tabu na Biashara kajiwekea fixed akaunti crdb wakati huo ilikuwa Ni asilimia 13 kwa mwezi

So anajipatia laki tano 30 kwa mwezi bila kukimbizana na mtu. Mkataba wake Ni wa miaka 3.

Ila anasema wameshusha riba Ni 9 Sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama anasimamia mwenyewe basi asifanye miradi inayohitaji sana uangalizi, kwa mtu aliyestaafu na hakuzoea changamoto za biashara au kilimo si vema kuanza kipindi kama hiki...
Kwa maoni yangu naona atafute eneo zuri kwa ajili ya kujenga real estate ndogo ndogo, mfano vyumba viwili viwili unaweza kupata kuanzia 150k-200k per month si haba na haina longolongo,
Pia angepata stationary, kwa hapa apate dada mmoja tuu na yeye mwenyewe, hivyo atakua anaamka kila siku asubuhi kama kipindi yupo kazini, kwa mtu ambaye alizoea kuamka kila asbh kuwahi kazini si vema kukaa tuu,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Atafute mazingira mazuri atenge fedha kiasi ajikite kwenye ufugaji!
Anaweza kufuga ng'ombe wa maziwa kwa Iringa Lita 1000 Na unakuta asas anafuata mpaka njombe ko demand bado ni kubwa!
Halafu ni mradi ambao hauleti stress sana!
Akipata mbegu nzuri angalau ya kutoa Lita 10+ inalipa sana!

Lakini kama anaweza anaweza akajikita kwenye ufugaji wa kuku Mfano chotara mahitaji ya mayai bado ni makubwa halafu haihitaji kutumia nguvu sana kuhudumia kama ng'ombe wa maziwa, Kwahiyo hii ata hawa wastaafu wanaweza kufanya!

Ingawa sijui kama atakuelewa Maana wastaafu na kununua nyumba mjini ni kama paka Na maziwa!

NB; Hiyo miradi inahitaji usimamizi wa karibu sana wa mwenye mali mwenyewe asije akajiroga kufuga kwa remote (yupo dar mradi upo njombe) atalia
Mshauri afuge nguruwe wa biashara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ungesoma comments zangu zote, najua unachofikiri kuwa ni kila mwezi SI KWELI pesa inaingia katikati ya mwezi wa pili au hata inamaliza miezi miwili ndio iingie na kiwango cha kila mwezi ni hafifu mno kuliko cha miezi mitatu.
.
Mimi nina kaelimu kadogo cha uhasibu (sijabobea) na wafanyakazi wanaostaafu kwenye taasisi yetu (kwa eneo nililopo) cheque zao na hata taratibu za kuwalipa nusu mishahara ya waliokuwa wakilipwa nashughulikia mimi
Mkuu niwie radhi kwa kuendeleza 'debate' kibishani.

Nilichokueleza nina uhakika nacho.

Ninachokuomba 'update' kumbukumbu yako kwa mstaafu mwaminifu juu ya kupata ukweli namna ambavyo wastaafu wanalipwa sasa hivi.

Tena muulize hivi...'eti pensheni za wastaafu zinaingia tarehe ngapi kila mwezi?'...

Hapa naongelea wastaafu wanaolipwa na hazina.

Ni kila tarehe 28 ya kila mwezi na haijawahi kupitiliza katika kipindi cha awamu ya utawala huu na kwenye sikukuu kubwa za kitaifa wanawahishiwa sana.

Na huyo mama anayeelezwa kwenye mada hii, kama alilipwa mkupuo 90m, uhakika wa kulipwa lk5 kila mwezi ni sahihi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani hapati penshion ya kila mwezi??,mfano mama yeye kila mwezi anapewa tshs 500,000
Laki Tano kwa mwezi,Mbona ni nyingi sana,iyo hela aiweke fixed deposit imzalishie aiache kama mwaka mwaka mmoja bila kuigusa ili akili iweze kutulia
 
Back
Top Bottom