Mradi gani wa kiuchumi unaweza kuanzisha kwa kutumia fedha za mafao kiasi cha Tshs 90,000,000/-?

Mradi gani wa kiuchumi unaweza kuanzisha kwa kutumia fedha za mafao kiasi cha Tshs 90,000,000/-?

Mkuu niwie radhi kwa kuendeleza 'debate' kibishani.

Nilichokueleza nina uhakika nacho.

Ninachokuomba 'update' kumbukumbu yako kwa mstaafu mwaminifu juu ya kupata ukweli namna ambavyo wastaafu wanalipwa sasa hivi.

Tena muulize hivi...'eti pensheni za wastaafu zinaingia tarehe ngapi kila mwezi?'...

Hapa naongelea wastaafu wanaolipwa na hazina.

Ni kila tarehe 28 ya kila mwezi na haijawahi kupitiliza katika kipindi cha awamu ya utawala huu na kwenye sikukuu kubwa za kitaifa wanawahishiwa sana.

Na huyo mama anayeelezwa kwenye mada hii, kama alilipwa mkupuo 90m, uhakika wa kulipwa lk5 kila mwezi ni sahihi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nina mzee wangu ambae kalitumikia jeshj la magereza kwa miaka 34 kastaafu 2015 akiwa na cheo kikubwa tu, huu utaratibu mpya uliokuja wakuwalipa kila mwezi sio wakweli na tarehe uliyoitaja si ya kweli anapokeaga huo mshahara Bank ya posta nasema hivi nikiwa na ushahidi.
.
Na kuna baadhi ya waliokuwa wafanyakazi wenzangu waliostaafu hawalipwi hivo
 
Namshukuru mama yetu

Alitugawia 5M each tupo 3

Na 1M each ya kwenda kula Bata Ngorongoro.


Yeye hajataka kupata tabu na Biashara kajiwekea fixed akaunti crdb wakati huo ilikuwa Ni asilimia 13 kwa mwezi

So anajipatia laki tano 30 kwa mwezi bila kukimbizana na mtu. Mkataba wake Ni wa miaka 3.

Ila anasema wameshusha riba Ni 9 Sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani wakishusha na yeye faida yake ya 13% kwa mwaka itashuka wakati kulingana na mkataba wake yeye alioingia na benki ni kuweka fedha kwa miaka mitatu na faida ikiwa ni 13% kwa mwaka? Hapo sasa si itakuwa kwenda kinyume na mkataba?
 
Nina mzee wangu ambae kalitumikia jeshj la magereza kwa miaka 34 kastaafu 2015 akiwa na cheo kikubwa tu, huu utaratibu mpya uliokuja wakuwalipa kila mwezi sio wakweli na tarehe uliyoitaja si ya kweli anapokeaga huo mshahara Bank ya posta nasema hivi nikiwa na ushahidi.
.
Na kuna baadhi ya waliokuwa wafanyakazi wenzangu waliostaafu hawalipwi hivo
Wanalipwa kila mwezi ni shahidi wa hilo kwa bibi yangu
 
Atafute mazingira mazuri atenge fedha kiasi ajikite kwenye ufugaji!
Anaweza kufuga ng'ombe wa maziwa kwa Iringa Lita 1000 Na unakuta asas anafuata mpaka njombe ko demand bado ni kubwa!
Halafu ni mradi ambao hauleti stress sana!
Akipata mbegu nzuri angalau ya kutoa Lita 10+ inalipa sana!

Lakini kama anaweza anaweza akajikita kwenye ufugaji wa kuku Mfano chotara mahitaji ya mayai bado ni makubwa halafu haihitaji kutumia nguvu sana kuhudumia kama ng'ombe wa maziwa, Kwahiyo hii ata hawa wastaafu wanaweza kufanya!

Ingawa sijui kama atakuelewa Maana wastaafu na kununua nyumba mjini ni kama paka Na maziwa!

NB; Hiyo miradi inahitaji usimamizi wa karibu sana wa mwenye mali mwenyewe asije akajiroga kufuga kwa remote (yupo dar mradi upo njombe) atalia
Maziwa yanalipa hapa nilipo ninakwenda kununua maziwa kwa mfugaji anauza 2400 uko vyema
 
There something wrong with lump sum money(wengi huita pensheni) haiwezekani kila mstaafu lazima afeli
 
Nina mzee wangu ambae kalitumikia jeshj la magereza kwa miaka 34 kastaafu 2015 akiwa na cheo kikubwa tu, huu utaratibu mpya uliokuja wakuwalipa kila mwezi sio wakweli na tarehe uliyoitaja si ya kweli anapokeaga huo mshahara Bank ya posta nasema hivi nikiwa na ushahidi.
.
Na kuna baadhi ya waliokuwa wafanyakazi wenzangu waliostaafu hawalipwi hivo
Ulipotaja "bank ya posta" tu ndiyo hapo umenifungua!
Mwanzo nilijiuliza sana, mara unataja "check za wastaafu"
Sasa hivi mkuu utaratibu wa check haupo na hao posta ni mumiani wakubwa.

Wanawatongoza wastaafu na kuwapatia mikopo yenye masharti ya kinyonyaji.

Na masharti ya kupatiwa hiyo mikopo, mstaafu ni lazima mwenyewe akiri kwa maandishi kuwa pensheni yake kupitia huko.

Wastaafu wengi si wakweli hasa wakiona "wamepigwa", mfuatilie huyo mzee wako utaupata ukweli wa ninayokueleza.

Kawaida askari magereza mishahara yao huchukulia Nmb ama Crdb.

Anapostaafu hakuna tena mambo ya check, utaratibu huo sikatai ulikuwepo zamani na uliwasumbua sana wastaafu na umekwisha kufutwa.

Sasa hivi pensheni kuanzia hicho kiinua mgongo cha mkupuo na vikokotoo vya kila mwezi, hulipwa 'direct' kupitia kwenye account zao za mishahara na ni kila mwezi.

Ukizidi kubisha mkuu itafikia hatua tuwekeane 'dau' la kutafuta mshindi ili mwisho wa siku ubishi huu tuumalize kwa pesa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulipotaja "bank ya posta" tu ndiyo hapo umenifungua!
Mwanzo nilijiuliza sana, mara unataja "check za wastaafu"
Sasa hivi mkuu utaratibu wa check haupo na hao posta ni mumiani wakubwa.

Wanawatongoza wastaafu na kuwapatia mikopo yenye masharti ya kinyonyaji.

Na masharti ya kupatiwa hiyo mikopo, mstaafu ni lazima mwenyewe akiri kwa maandishi kuwa pensheni yake kupitia huko.

Wastaafu wengi si wakweli hasa wakiona "wamepigwa", mfuatilie huyo mzee wako utaupata ukweli wa ninayokueleza.

Kawaida askari magereza mishahara yao huchukulia Nmb ama Crdb.

Anapostaafu hakuna tena mambo ya check, utaratibu huo sikatai ulikuwepo zamani na uliwasumbua sana wastaafu na umekwisha kufutwa.

Sasa hivi pensheni kuanzia hicho kiinua mgongo cha mkupuo na vikokotoo vya kila mwezi, hulipwa 'direct' kupitia kwenye account zao za mishahara na ni kila mwezi.

Ukizidi kubisha mkuu itafikia hatua tuwekeane 'dau' la kutafuta mshindi ili mwisho wa siku ubishi huu tuumalize kwa pesa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni vyema tukawekeana dau mkuu, ili tuumalize mjadala mimi napatikana kwa makonda
 
Kwa umri wake atafute kiwanja ajenge nyumba za kupanga kwa mfano chumba na sebure na choo ndani anaweza jenga hata kumi biashara hiyo haina stress kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mama yangu alistaafu, kiinua mgongo akatumia kujenga nyumba za kupangisha 3. Nyumba ni 2 bedrooms kitchen na sebule. Bahati kiwanja alkuwa nacho tayari na eneo ni zuri karibu na barabara. Hela iliyobaki akanunua gari ya kutembelea, nyingine akaanzisha mradi was kuku wa mayai (alikuwa na uzoefu) nyumba anapangishsha 300,000 kwa mwezi, na zinagombaniwa hakosi wapangaji.
 
Kuna kitu cha kujifunza hapa,wekeza na fanya biashara ukiwa na nguvu zako;fedha za kiinua mgongo ni kwa ajili ya kuukarabati mwili kutokana na magonjwa ya uzeeni.
 
Wana JF habari zenu,

Mama yangu baada ya kunusurika na kikotoo ameniomba nimshauri kumpendekezea mradi ambao anaweza akaanzisha na kuusimamia yeye mwenyewe, pesa anazotegemea kupata ni Tshs. 94,000,000.

Fedha anayotegemea kuanzishia mradi ni tshs 90,000,000.

Nimeona ni vyema kuwashirikisha kupata mawazo mbadala, pkwa kuwa ninaamini baadhi yetu wazazi wetu walistaafu na kuanzisha miradi ambayo imekuwa imara na endelevu mpaka sasa.
Mkuu natumaini mama yetu alishapata mafao husika pia alishawekeza sehemu ya pesa ya mafao katika miradi ya kuingiza pesa, ingependeza ukarudisha mrejesho namna mradi alioufungua ulivyo hivi sasa ili wengine tupate funzo kupitia uzoefu wenu.
 
Back
Top Bottom