Mradi wa BBT Usipofanya Vizuri Tutawalaumu Wizara ya Kilimo

Mradi wa BBT Usipofanya Vizuri Tutawalaumu Wizara ya Kilimo

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

KOMREDI KAWAIDA - MRADI WA B.B.T USIPOFANYA VIZURI TUTAWALAUMU WIZARA YA KILIMO

Kilombero. Wakati Wizara ya Kilimo ikitekeleza mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT), Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM), Mohammed Kawaida amesema chochote kitakachokwama lawama ataitupia wizara hiyo.

Kauli yake hiyo, inatokana na kile alichoeleza kuwa, Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kugharimia sekta ya kilimo na jukumu la wizara hiyo ni kutekeleza.

Kawaida ametoa kauli hiyo leo, Jumatano ya Aprili 19, 2023 akihotubia vijana baada ya kutembelea mradi wa BBT Kituo cha Chuo cha Taifa cha Sukari wilayani Kilombero Mkoa wa Morogoro.

"Wizara ya Kilimo imepewa imani kubwa kwa ajenda ya 2030, mradi wa BBT na mambo mengine lukuki," amesema.

Kwa sababu ya imani iliyopewa wizara hiyo, amesema chochote kikikwama UVCCM na vijana wengine watailaumu Wizara ya Kilimo kwa kushindwa kutekeleza.

"Chochote kikikwama UVCCM na vijana wengine Tanzania tutakayemlaumu ni Wizara ya Kilimo na sio Rais Samia, kwa sababu yeye ametoa fedha nyingi katika Wizara hiyo," ameeleza.

Kauli hiyo ya Kawaida ni kama inapigia msumari wa kile kilichowahi kuelezwa na Rais Samia kuhusu mradi wa BBT, kwamba hata kusikia umekwama.

"Sitaki kusikia tumeshindwa, hakuna kushindwa lazima twende na lazima tufanikiwe,” alisema Rais Samia Machi 20, 2023 wakati wa uzinduzi wa mradi huo.

Onyo lake hilo liliambatana na onyo kwa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe alipomwambia: “Nataka kuwaambia nimekusudia kwenye hili na sitavumilia Bashe na wenzio pale nitakapotoa fedha za wavuja jasho wa Tanzania ziende kwenye matumizi ya kilimo zikazalishe na fedha ile ikachezewe, sitavumilia,” alisema.
 

Attachments

  • FuGJ6-cWYAM65fE.jpg
    FuGJ6-cWYAM65fE.jpg
    139.8 KB · Views: 10
  • FuGJ8mVX0AAp1gc.jpg
    FuGJ8mVX0AAp1gc.jpg
    153.2 KB · Views: 13
  • WhatsApp Image 2023-04-19 at 17.18.00(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-19 at 17.18.00(1).jpeg
    95.7 KB · Views: 13
Kisiasa utaonekana uko vizuri ila kwa uhalisia ule mradi CAG akipiga tutajua ukweli
 
Back
Top Bottom