Mradi wa Bomba la Mafuta la Tanzania na Uganda wakumbwa na changamoto za Kifedha

Mradi wa Bomba la Mafuta la Tanzania na Uganda wakumbwa na changamoto za Kifedha

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mradi wa pamoja wa mafuta kati ya Tanzania na Uganda, maarufu kama Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), umekumbwa na changamoto za kifedha. Mradi huu, unaotekelezwa kwa ushirikiano na kampuni za kimataifa TotalEnergies na China National Offshore Oil Corporation (CNOOC), umelazimika kutafuta njia mbadala za ufadhili kutokana na changamoto za mikopo.
1730101292623.png
EACOP, mradi wenye thamani ya dola bilioni 5, unalenga kusafirisha mafuta kutoka hifadhi za Ziwa Albert nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga, Tanzania. Hata hivyo, mradi huu umekumbwa na upinzani mkali kutoka kwa wanaharakati wa mazingira na baadhi ya wadau wa kimataifa, ambao wanaonya kuwa unaweza kuharibu mazingira na kusababisha athari kwa jamii zinazoishi karibu na eneo la mradi.
1730101377449.png
Kutokana na changamoto hizi, washirika wakuu wa mradi wameanza kuwekeza tena mtaji wao kwa lengo la kuendeleza utekelezaji wa mradi huo, licha ya vikwazo vilivyopo.

Pia, Soma: Ukindhani wa mitazamo mradi wa EACOP, kunani nyuma ya pazia, ukweli ni upi?
 
Mabeberu wana akili za kijinga sana! Yaani hizo athari za mazingira hazitokei kwao, isipokuwa kwetu tu!!
 
Back
Top Bottom