Mradi wa Bomba la Maji la Mugango-Kiabakari-Butiama wakaguliwa na Kamati ya Bunge - Jimbo la Musoma Vijijini

Mradi wa Bomba la Maji la Mugango-Kiabakari-Butiama wakaguliwa na Kamati ya Bunge - Jimbo la Musoma Vijijini

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Jumamosi, 14.1.2023, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ilikagua Mradi wa ujenzi wa miundombinu ya Bomba la Maji la Mugango-Kiabakari- Butiama.

Gharama ya Mradi huu ni kubwa:

~ Tsh bilioni 70.5 kutoka Serikali ya Saudi Arabia (49.12%), BADEA (31.40%) na Serikali ya Tanzania (19.48%).

~ Tsh bilioni 4.775 za Serikali ya Tanzania kwa ajili kujenga miundombinu ya usambazaji wa maji kwenye Kata za Mugango na Tegeruka.

~ Choteo la maji lilojengwa Kijijini Kwibara, Kata ya Mugango, Musoma Vijijini, lina uwezo wa kuchota LITA MILIONI 35 KWA SIKU.

Kamati ya Bunge imerdhishwa na utekelezaji wa Mradi huu ambao utakamilika ifikapo tarehe 30 Juni 2023.

Matokeo ya ukaguzi wa Mradi huu yapo kwenye CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa.

images.jpg


Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
Tarehe:
Jumatatu, 16.1.2023
 
Back
Top Bottom