Mradi wa mabasi ya mwendokasi- umefeli

Mradi wa mabasi ya mwendokasi- umefeli

bopwe

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2013
Posts
1,773
Reaction score
1,460
MRADI WA MWENDOKASI: MIFANO HALISI YA WIZI WA FEDHA ZA UMMA

Mradi wa Mwendokasi (BRT) ni kielelezo cha namna miradi mikubwa inavyogeuzwa kuwa mashamba ya mafisadi badala ya kuwanufaisha wananchi wa kawaida. Tunaposema Tanzania ni nchi ya wizi na rushwa, hatusemi kwa dhana tu—tuna ushahidi wa wazi.

1. Mradi wa Trillioni za Mikopo ya Riba Kubwa

Serikali imekuwa ikichukua mikopo ya riba kubwa kwa miradi kama hii, lakini hakuna anayejali athari zake kwa wananchi wa kawaida. Hakuna uwazi kuhusu mikataba hii, gharama halisi za mradi, wala manufaa yanayopatikana kulinganisha na pesa inayotumika. Wanaofaidika ni viongozi waliopata tenda na wale wanaopitisha mikataba hiyo kwa maslahi binafsi.

2. Viongozi wa Mwendokasi Wakila Bata kwa Pesa za Umma

Wakati wananchi wakihangaika na maisha magumu, viongozi wa miradi hii wanaishi maisha ya kifahari kupita kiasi. Kuna kiongozi ndani ya mradi huu anayesomesha watoto wake wanne kwenye shule ya kimataifa IST kwa ada ya milioni 30 kwa mwaka kwa kila mtoto. Je, mshahara wake unaruhusu? Ameweza kununua nyumba Upanga kwa bilioni 2.8, pesa ambazo haziwezi kutoka kwa mshahara wa kawaida wa mtumishi wa umma. Huu ni ushahidi wa wizi wa waziwazi wa fedha za umma.

3. CCM na Serikali Yake Wamehalalisha Wizi

Rushwa na ufisadi vimekuwa sehemu ya utawala wa CCM. Miradi mikubwa kama Mwendokasi, ATCL, na SGR inatekelezwa kwa gharama kubwa kuliko inavyopaswa, huku wananchi wakilipa deni lisilo na faida kwao. Bunge, ambalo lilipaswa kuwa sauti ya wananchi, limejaa wabunge wa CCM wasiojali chochote zaidi ya kupitisha maamuzi ya chama bila kuuliza maswali.

4. Ubinafsishaji Unapigwa Vita kwa Sababu ya Wizi

Mtu yeyote akizungumzia ubinafsishaji wa miradi ili huduma ziboreke, mafisadi wanapiga kelele kwa sababu wanajua wizi wao utafunuliwa. Mfumo wa sasa wa uendeshaji wa miradi hii unawanufaisha wao, siyo wananchi.

5. Wakati wa Uchaguzi, CCM Wanatumia Miradi Hii Kama Chambo

Katika kila uchaguzi, CCM hutumia miradi kama Mwendokasi kama kigezo cha maendeleo, lakini hawatawahi kusema jinsi ilivyotokana na mikopo mikubwa ya riba au jinsi viongozi wamejitajirisha kupitia miradi hiyo. Wananchi wengi hawaelewi kuwa miradi hii si msaada—ni madeni tunayolazimika kulipa kwa kupitia kodi zetu kwa miongo kadhaa.

6. Upinzani Ulipokuwa na Ajenda ya Kupambana na Rushwa, Ulipata Nguvu

Katika miaka ya nyuma, @ChademaTz ilipojitokeza na kupambana na rushwa kwa nguvu, ilivutia wafuasi wengi. Sasa, inaonekana upinzani umelegea katika ajenda hii, na wananchi wanazidi kupoteza matumaini.
@ACTwazalendo
Huku bara mhh ukweli use usemwe ni magoigoi wanaogopa au wapo pamoja na ccm kwenye kufumbia macho majizi.
Wananchi Wataendelea Kuteseka Mpaka Lini?
Kama sio feed ya daladala Kwa kutegemea mwendokasi tu Morogoro road Wananchi wangeoata tabu sana.

Tanzania inaendelea kuzama kwenye ufisadi kwa sababu ya uongozi usiojali maslahi ya wananchi. Miradi mikubwa kama Mwendokasi inapaswa kuwa mkombozi kwa wananchi, lakini badala yake imekuwa njia ya kujitajirisha kwa wachache. Bila uwajibikaji na uwazi wa kweli, tutaendelea kuwa taifa la madeni na maisha magumu kwa wananchi wa kawaida.

Wakati umefika kwa wananchi kufumbua macho na kudai uwajibikaji wa kweli. Tusikubali kudanganywa tena!
@SuluhuSamia
Hajali wateule wake wakiiba
#Uchaguzi2025
 
Kama tu graduates ndio hawa tupo nao kitaa.. wanaishia kusema mimi nina gpa 4 and so far.. the hata wakikabidhiwa a 1 km road wanashindwa perform!!
Ni shida
 
MRADI WA MWENDOKASI: MIFANO HALISI YA WIZI WA FEDHA ZA UMMA

Mradi wa Mwendokasi (BRT) ni kielelezo cha namna miradi mikubwa inavyogeuzwa kuwa mashamba ya mafisadi badala ya kuwanufaisha wananchi wa kawaida. Tunaposema Tanzania ni nchi ya wizi na rushwa, hatusemi kwa dhana tu—tuna ushahidi wa wazi.

1. Mradi wa Trillioni za Mikopo ya Riba Kubwa

Serikali imekuwa ikichukua mikopo ya riba kubwa kwa miradi kama hii, lakini hakuna anayejali athari zake kwa wananchi wa kawaida. Hakuna uwazi kuhusu mikataba hii, gharama halisi za mradi, wala manufaa yanayopatikana kulinganisha na pesa inayotumika. Wanaofaidika ni viongozi waliopata tenda na wale wanaopitisha mikataba hiyo kwa maslahi binafsi.

2. Viongozi wa Mwendokasi Wakila Bata kwa Pesa za Umma

Wakati wananchi wakihangaika na maisha magumu, viongozi wa miradi hii wanaishi maisha ya kifahari kupita kiasi. Kuna kiongozi ndani ya mradi huu anayesomesha watoto wake wanne kwenye shule ya kimataifa IST kwa ada ya milioni 30 kwa mwaka kwa kila mtoto. Je, mshahara wake unaruhusu? Ameweza kununua nyumba Upanga kwa bilioni 2.8, pesa ambazo haziwezi kutoka kwa mshahara wa kawaida wa mtumishi wa umma. Huu ni ushahidi wa wizi wa waziwazi wa fedha za umma.

3. CCM na Serikali Yake Wamehalalisha Wizi

Rushwa na ufisadi vimekuwa sehemu ya utawala wa CCM. Miradi mikubwa kama Mwendokasi, ATCL, na SGR inatekelezwa kwa gharama kubwa kuliko inavyopaswa, huku wananchi wakilipa deni lisilo na faida kwao. Bunge, ambalo lilipaswa kuwa sauti ya wananchi, limejaa wabunge wa CCM wasiojali chochote zaidi ya kupitisha maamuzi ya chama bila kuuliza maswali.

4. Ubinafsishaji Unapigwa Vita kwa Sababu ya Wizi

Mtu yeyote akizungumzia ubinafsishaji wa miradi ili huduma ziboreke, mafisadi wanapiga kelele kwa sababu wanajua wizi wao utafunuliwa. Mfumo wa sasa wa uendeshaji wa miradi hii unawanufaisha wao, siyo wananchi.

5. Wakati wa Uchaguzi, CCM Wanatumia Miradi Hii Kama Chambo

Katika kila uchaguzi, CCM hutumia miradi kama Mwendokasi kama kigezo cha maendeleo, lakini hawatawahi kusema jinsi ilivyotokana na mikopo mikubwa ya riba au jinsi viongozi wamejitajirisha kupitia miradi hiyo. Wananchi wengi hawaelewi kuwa miradi hii si msaada—ni madeni tunayolazimika kulipa kwa kupitia kodi zetu kwa miongo kadhaa.

6. Upinzani Ulipokuwa na Ajenda ya Kupambana na Rushwa, Ulipata Nguvu

Katika miaka ya nyuma, @ChademaTz ilipojitokeza na kupambana na rushwa kwa nguvu, ilivutia wafuasi wengi. Sasa, inaonekana upinzani umelegea katika ajenda hii, na wananchi wanazidi kupoteza matumaini.
@ACTwazalendo
Huku bara mhh ukweli use usemwe ni magoigoi wanaogopa au wapo pamoja na ccm kwenye kufumbia macho majizi.
Wananchi Wataendelea Kuteseka Mpaka Lini?
Kama sio feed ya daladala Kwa kutegemea mwendokasi tu Morogoro road Wananchi wangeoata tabu sana.

Tanzania inaendelea kuzama kwenye ufisadi kwa sababu ya uongozi usiojali maslahi ya wananchi. Miradi mikubwa kama Mwendokasi inapaswa kuwa mkombozi kwa wananchi, lakini badala yake imekuwa njia ya kujitajirisha kwa wachache. Bila uwajibikaji na uwazi wa kweli, tutaendelea kuwa taifa la madeni na maisha magumu kwa wananchi wa kawaida.

Wakati umefika kwa wananchi kufumbua macho na kudai uwajibikaji wa kweli. Tusikubali kudanganywa tena!
@SuluhuSamia
Hajali wateule wake wakiiba
#Uchaguzi2025
Hivi na nyie mna Rais?
 
Nchi imejaa machawa ambayo akili na macho yao yamejaa matongorongo, hata kama mambo yanakwenda kombo, wala wao hawajali, kazi yao kutwa nzima ni kusifu na kuabudu tu.

Umeleta mada yenye mashiko sana, lakini ukweli huu wananchi wengi wala hawauoni. Wamezama katika dimbwi la umaskini wa kiakili na kimwili. Tatizo ambalo limezalisha tatizo jipya la machawa na uchawa ambalo linafahamika vyema hapa jukwaani.
 
Kwa nchi ambayo haina kiongozi kama ilivyo Tz lazima kila kitu kitakufa tuu, huyu ndio mtawala wa hovyo kabisa kuwahi kutokea Tz na waswahili wengi walivyo wapumbavu hawana akili timamu wata mchagua tena ni bora Mungu aingilie kati hii kesi afanye mambo yake tuu itakua bora sana
 
Jamaa wanaoendesha hizo nchi zilizoendelea civil servants ni watu wenye akili.

Hakuna upendeleo kwenye succession planning ya civil services kwa wazungu, utapanda kwa uwezo tu na technical knowledge ya nafasi husika.

Sisi bado sana, ukiwasikiliza civil servants wetu; failure ya miradi iliyo chini yao ni inevitable.

Hawana uwezo, ndio ukwelk.

Shida ya Tanzania ni uwezo mdogo wa uongozi.
 
Hahaha nchi haitaki uzazi wa mpango ahalafu wanaiga miradi ya Ujerumani. Ile kampuni ya Strabag walipiga zao wakaishia.

Nchi hii wange jenga barabara za kwaida tu tuka teleza na boda boda na bajaji zetu, au wairudishe UDA yetu na chai maharage zetu tupambane kivyetu.

Plani hizi za mwendo kasi ilipaswa wakomae na Treni kama ile ilikuwa inaitwa "Treni ya Mwakyembe" Zijengwe nyinge hata kwa kiwango cha reli ya kawaida siyo lazima standard Gauge.

Population inaongezeka kwa kasi, naiona Tanzania inakwenda kuwa kama Bangladesh, Sasa Mwendokasi wa nini, utakuwa Outdated muda siyo mrefu.

Kama wanatujengea sisi, walipaswa kutuuliza kwanza, lakini wanapotufanyia maamuzi kama haya wanatudanganya sana.

Wao wako kwenye Ma Land Cruiser, Haya ma Bus ya mwendo kazi yanatembea kama konokono na yanajaza kuliko chai maharage au Hiace zetu za Mbagala Gongo la Mboto, wanataka kutuua kwa magonjwa ya mlipuko sioni kama wana nia nzuri nasi.

Nchi hii Makazi ya mijini mabovu, viwanja kibao havija pimwa, majengo chini ya kiwango, na makazi holela.

Vijijini hakuna huduma, lakini wanataka kutudanganya na miradi ya mwendo kazi, hata siyo mwendo kasi, na haipounguzi foleni, sasa sijui kwanini wanaing'ang'ania.
 
Bakhresa akitoa makampuni yake yote kwa serikali baada ya muda mfupi yote ya tafirisika.
Bakhresa akipewa serikali kuindesha, wananchi wengi wanageuka kuwa matajiri
 
Back
Top Bottom