Mrejesho biashara ya madini ya dhahabu second season

Mrejesho biashara ya madini ya dhahabu second season

mcrounmj

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2016
Posts
380
Reaction score
889
Panapo majaaliwa ya mwenyezi Mungu tumekutana tena kwenye kikao cha wapambanaji. Wakuu wa jukwaa hili hususani vijana nawasalimu kwa Salam adhimu ya mama yetu Samia Suluhu Hassan......

Bila kuwachosha ni kuwa tangu nimeianza safari yangu ya kibiashara nimekuwa nikiwashirikisha hatua ninazopitia, ups and downs na Mambo lukuki. Nikiri tu kuwa kufanya biashara na ikakua siyo kitu kidogo. Inahitaji uvumilivu, umakini na bidii.

Mwaka Jana 2020 June nilikuja kwenye jukwaa hili kuomba ushauri juu ya kuanzisha biashara ya madini ya dhahabu. Watu wengi walinishauri, walinitia moyo na kunikatisha tamaa pia. Nilifanikiwa kukata leseni na vibali vingine na kuanza biashara kama blocker. Pamoja kuwa na mtaji mdogo yaani mpaka napata vibali ilikuwa imebaki milioni nne tu na changamoto nyingine lakini kutokea June nianze biashara hadi December nilikuwa nimefikisha milioni kumi na upuuzi (ndani ya miezi sita).

Nimeianza January ya mwaka huu na moto zaidi, kwanza nikiwa na uzoefu wa kutosha na pili nikiwa nimeshapata connection na watu tofautitofauti.

Malengo yangu ilikuwa mpaka kufika June ya mwaka huu kuanzia January niwe na zaidi ya milioni ishirini na hapo ninunue karasha nianze kukuza mlima na biashara ya dhahabu nikiendelea nayo.

To be honest guys, malengo yamefika kabla ya muda. Ninachokisubiri ni kwenda kuchonga karasha tu niwe na mwalo wangu. Tangu nimeianza biashara hii Sasa naenda kukamilisha mwaka mmoja this June. Vivyo kwa ukuaji wa kiwango hicho naona kama ushindi mkubwa mno kwangu.

Nimeandika na nimekuwa nikiandika my ways to success ili ku share na vijana wenzangu kwa sababu naamini njia niliyopita kufika hapa lipo kundi kubwa la vijana wanapita na pengine wanahisi wamepotea. Mimi ni mhanga wa wahitimu wa chuo kikuuu waliokosa ajira. Niliamua kupambana na umasikini nikifanya vibarua vyote vya halali nikikusanya vipande vya sarafu ili nipate mtaji.

Changamoto ni nyingi mno. Ni lazima ujifunze kuzipunguza zenye kupunguzika, ubalansi matumizi yako na biashara. Katika kipindi cha mwaka mzima kuna muda nimeanguka, nimetapeliwa zaidi ya milioni mbili kwa siku moja, zipo siku nimenunua mzigo kwenye kuuza ulikata zaidi ya milioni mbili, n.k n.k...

Cha mwisho ni kwamba vijana tusibaki kulalamika kwa kuilaumu serikali kushindwa kutuajiri, bali tuziibue fursa na kisha tuidai serikali ijenge mazingira rafiki katika kukuza biashara zetu. Wanajukwaa hususani vijana, giza ni nene safari ni ndefu lakini tutatoboa.

#kikaochawapambanaji

1620712743416.png

 
Hongera boss.

Ila sisi vijana huwez kutuona kwenye thread kama hizi, ila za mateso mtu anayopitia ndipo utakukuta huko, au tuliyempekua tukakuta sintofahamu( utapeli) ndio utatukuta huko, pengine hapa tumekupekua thread zote na comment zako zote humu tukakuta hauna chembe ya utapeli, kwahio huwez kutuona wengi ndio mana unaona ndani ya masaa 17 kuna comment 5 tu.

Ila naamini ume inspire wale wenye mlengo wa kuingia huko kwenye dhahabu.

Wangari Maathai umeona hii?
Sikuona ngoja nisome boss
 
Hongera boss.

Ila sisi vijana huwez kutuona kwenye thread kama hizi, ila za mateso mtu anayopitia ndipo utakukuta huko, au tuliyempekua tukakuta sintofahamu( utapeli) ndio utatukuta huko, pengine hapa tumekupekua thread zote na comment zako zote humu tukakuta hauna chembe ya utapeli, kwahio huwez kutuona wengi ndio mana unaona ndani ya masaa 17 kuna comment 5 tu.

Ila naamini ume inspire wale wenye mlengo wa kuingia huko kwenye dhahabu.

Wangari Maathai umeona hii?
😀😀😀...sasa hivi wimbi limeangukia ulichoandika...huku kwenye mafaniko full korosho..
Lol
 
Hongera boss.

Ila sisi vijana huwez kutuona kwenye thread kama hizi, ila za mateso mtu anayopitia ndipo utakukuta huko, au tuliyempekua tukakuta sintofahamu( utapeli) ndio utatukuta huko, pengine hapa tumekupekua thread zote na comment zako zote humu tukakuta hauna chembe ya utapeli, kwahio huwez kutuona wengi ndio mana unaona ndani ya masaa 17 kuna comment 5 tu.

Ila naamini ume inspire wale wenye mlengo wa kuingia huko kwenye dhahabu.

Wangari Maathai umeona hii?
Hakika, something is wrong somewhere.

Kwa hivi vilio vya ajira kila siku humu jukwaani na kwingineko katika hali ya kawaida ungetarajia uzi huu uwe umefurika watu wakitoa pongezi, kujifunza na kuuliza ni jinsi gani na wao wanaweza pita njia hii ama fursa nyingine zinazo ambatana na njia hii.
 
Panapo majaaliwa ya mwenyezi Mungu tumekutana tena kwenye kikao cha wapambanaji. Wakuu wa jukwaa hili hususani vijana nawasalimu kwa Salam adhimu ya mama yetu Samia Suluhu Hassan........
Mkuu, hongera kwa kupambana na kushare experience ili wenye nia nao wapate kujifunza pa kuanzia atleast.

Hope utajibu swali la unapofanyia shughuli zako kama lilivyo ulizwa na watu kadhaa.
 
Hakika, something is wrong somewhere.

Kwa hivi vilio vya ajira kila siku humu jukwaani na kwingineko katika hali ya kawaida ungetarajia uzi huu uwe umefurika watu wakitoa pongezi, kujifunza na kuuliza ni jinsi gani na wao wanaweza pita njia hii ama fursa nyingine zinazo ambatana na njia hii.
Hatuthubutu....hapa kuna watu wako busy kufukua mafaili ya mtoa mada😀! Wamuumbue roho zitulie
 
Hatuthubutu....hapa kuna watu wako busy kufukua mafaili ya mtoa mada[emoji3]! Wamuumbue roho zitulie
[emoji23][emoji23][emoji23]
Basi kama tumekosa pa kumuumbua, tuokote hata mawili matatu ya kujifunza.

Kiukweli hii ni moja ya business ambayo inaweza kukubadilisha jina ndani ya muda mfupi ukiwa na jitihada, uvumilivu na right attitude.
 
Hongera mkuu ninatamani sn kuingia hyo inamaana biashara hila changamoto hayo mavibari nnaona mtaji wenyewe utaishia humo kabla ya biashara.
 
[emoji23][emoji23][emoji23]
Basi kama tumekosa pa kumuumbua, tuokote hata mawili matatu ya kujifunza.

Kiukweli hii ni moja ya business ambayo inaweza kukubadilisha jina ndani ya muda mfupi ukiwa na jitihada, uvumilivu na right attitude.
Hakika mkuu
 
Back
Top Bottom