Mrejesho: Faida nilizopata baada ya kuwatoa watoto wangu shule ya English Medium na kuwarejesha kayumba

Daddy & Mummy maana yake ni baba na mama. Sasa shida ipo wapi? Hivi unajua ya kuwa asilimia kubwa ya tabia za hovyo mtoto anajifunza katika hizi shule za Swahili medium? Mimi ninashauri kila mmoja afanye jambo kulingana na hali yake ya uchumi.
Sio kweli mkuu asilimia kubwa ya tulio zaliwa miaka ya themanini na tisini na kaka zetu wa miaka.ya sabini tumesoma shule hizi ambazo mnaziita shule za kayumba na hakuna kitu kama.hicho unacho kisema wewe
 
Sio kweli mkuu asilimia kubwa ya tulio zaliwa miaka ya themanini na tisini na kaka zetu wa miaka.ya sabini tumesoma shule hizi ambazo mnaziita shule za kayumba na hakuna kitu kama.hicho unacho kisema wewe
Unaikumbuka vita baina ya Secondary ya Tambaza na Azania? Vijana well-mannered wanaweza kufanya vita kama ile?
 
Huo ndo ukweli watu wengi wanaanza familia pasipo kuwa na mpango mkakati wa kiuchumi wa miaka isiyopungua 30

Shule ya za serekali kidogo zaman sasa hivi zinahali mbaya sana
We acha tu ukiwasoma wengi hapo wapo umri wa 30-45 kipindi ambacho kuna matumzi mengi kwa baba wa familia ikiwemo ujenzi/kodi ya nyumba, uwekezaji, kutegemewa na ndugu/wazazi/jamii/serikali ada za watoto, kujiendeleza kielimu kama hakujiendeleza kwenye 20s, chakula na malazi kwa familia, kuhudumia mke, n.k sasa kwa wingi wa matumiz kama haya na mengine lazma kama mtu kipato si kikubwa ataishia kuwachomoa watoto private na kuwapeleka za serikali. Kwa mtu ambaye yupo Dar na yupo karibia mjini afadhali hata hizo za serikali basi umpeleke shule nzuri mfano bunge/olympio na zingine zile nzuri nzuri. na si kumdump mtoto apambane na hali yake. Kingine mzazi lazima ufuatilie kwa ukaribu mno maendeleo ya mtoto na isiwe tena ndo jukumu la waalimu
 
Ndugu ile sentensi ya kiingereza ilikuwa ina makosa au haina makosa? Unazunguka sana. Hapa mtandaoni huwa hakuna huruma jomba.
 
Sasa imekuwaje leo ukaandika sentensi kama ya mtu wa form one B huko Oljoro Secondary School?
 
Moderator hii comment naomba mu ipin. Komenti iliyo kwenda shule.

Mkuu , You are the true son of your father.

Baba ako hakusingiziwa. Wewe ni mtoto wake kabisa.
kama unaweza mpeeleke mtoto shule nzuri za awali. Akipata msingi mzuri sekondari atatoboa bila shida. Kijijinii kwangu kuna shule ndogo ya englsh medium. hii shule hutoa wanafunzi zaidi ya 20 kwenda sekondari yetu ya kata. Katika matokeo ya form four asili mia tisini ya wale wanaotoka english medium hupata daraja la kwanza na la pili. Walobaki hupata daraja la tatu, Haya matokeo husababishwa na msingi mzuri wa shule ya msingi. kama unao uwezo mpeleke mtoto english medium, lakini sekondari mpeleke zaserekali.
 
Sio kweli mkuu asilimia kubwa ya tulio zaliwa miaka ya themanini na tisini na kaka zetu wa miaka.ya sabini tumesoma shule hizi ambazo mnaziita shule za kayumba na hakuna kitu kama.hicho unacho kisema wewe
JF ikupatie tuzo ya mbishi wa mwaka 😂😂😂
 
Muhimu hapa tupamgane SoMo la kiingereza lifundishwe kuazia awali hukuhuku kayumba

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
Mkuu hata likifindishwa kuenxis awali hamba kitu.
Kufundisha kuna ambatana na vitu vingi sana. Kipindi tu cha kufundisha ni dk 40 utajua kingereza cha nani ?
Lugha inahitaji practice je ni saaa nfspi wanajixoeza kuongea?
Bado umahurivwa walimu, bado vitabu,
Bado computer au vishikwambi.
Ufundishaji wa lugha ni mgumu sana .
 
umeongea bonge la point ambayo ni wachache sana wanaweza iona
Connection na exposure ni muhimu zaid hata ya cheti kizuri
Ni juzi tu mjukuu wa Azam kaoa, picha waliyoitoa alipiga Yeye, Mtoto wa MO, GSM na mwingine hatumjui, na wote wamesoma shule moja IST
 
Daddy & Mummy maana yake ni baba na mama. Sasa shida ipo wapi? Hivi unajua ya kuwa asilimia kubwa ya tabia za hovyo mtoto anajifunza katika hizi shule za Swahili medium? Mimi ninashauri kila mmoja afanye jambo kulingana na hali yake ya uchumi.
Huko wanafundishana ujinga maana anajua hawezi fukuzwa.

Huwezi kuta mtoto wa Tusiime,Alpha, kemebos anafanya ujinga maana anajua akifukuzwa Baba yake anaumia mfukoni na kufukuzwa ni dakika
 
Unaikumbuka vita baina ya Secondary ya Tambaza na Azania? Vijana well-mannered wanaweza kufanya vita kama ile?
Kwamza kwa muda aliotaja shule binafsi zilikuwa chache,wanafunzi wengi walisomeshwa Kenya na Uganda.
Hata Serikali haikuwa na Kayumba, hizi Kayumba zimeanzishwa na Lowasa alipokuwa Waziri Mkuu, kabla ya hapo shule zilikuwa nzuri za serikali. Kupangiwa kipaji maalumu mtu lazima uchekelee, ila siku hizi mtu anaona bora aende privy
 
well said
 
Sasa imekuwaje leo ukaandika sentensi kama ya mtu wa form one B huko Oljoro Secondary School?
Niko oldonyowas ,na hapa kazini nimejifunza kichina ndicho tunachofanyia kazi, brain ya binadamu Ni very complex kiasi kwamba huwa haiwezi kuelezeka kwa maneno ya kawaida.
Yaani huwa hatutumii hata 1% ya ubongo wetu tukiwa hapa duniani. Ni sie wenyewe tunaji limit. Yaani mtt alipenda kitu ndio mafanikio yake. Nakumbuka Niko la kwanza Kuna siku nimeokota 500 sokoni nikaenda kununua kitabu kile punda na pundamilia,mfalme mwenye masikio Kama punda, yaani unafaulu hesabu mpaka mwalimu anakuuliza kuwa unasoma twisheni unamjibu hapana,anakuambia lete daftari lako la hesabu nione. Sidhani kuwa kuingiza kitu kichwani mwako kunahitajika mtu aniwekee hizo Ni bidii zangu binafsi na uhiyari wangu na tamaa ya kutaka kujua ama kula maarifa siamini kuwa Ni lazima nilipe mabilioni.
Elon musk anasema you can anything mtandaoni Kama unahitaji kujifunza.
 
Mwanangu najua inakuuma sana kukosea kuandika kiingereza ndo maana unatoa maelezo mengi ya kutaka kuonewa huruma. Mimi nisingehoji kama na wewe usingejimwambafy kwamba ulikuwa unajua kiingereza kuliko hata waliotoka medium. Siku nyingine acha sifa za kijinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…