Mrejesho: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga

Mrejesho: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga

Nilivyosoma stori aisee, nimependa namna unavyoweka wazi majibu ya mke, umepata mke mwenye hekima sana, ana majibu yenye busara na upole.

Nikirudi kwako, embu rahisisha tu mambo. Mwache aandike kwa jina lake maana hata kiwanja ni chake, yaan ukiona MTU anakwambia ngoja nikajifikirie ujue bado hajaafiki, watoto analea mama pale ,wewe unakuja Mara mojamoja, kwann usimwamini mkeo, mbona kama umekaa attention sana.

Hata mkiachana kwa ajili ya watoto bado itakubidi uwaachie Nyumba(kwa mwanaume Mwenye akili hawez taka watoto wataabike pa kuishi), ulisema una kiwanja kama ulivyosema wewe ni mwanaume ,kichwa cha familia em pambana tena jenga kwenye kiwanja chako then waandike wanao.

Usitumie ubabe, tafadhali mwachie tu kama zawadi hiyo Nyumba. Ni mkeo huyo analea na kuishi hapo na watoto wako.(usipojiangalia, ndoa yako ndo inaenda kufall apart Mkuu)
Huu ushauri usiufuate hata
Akikomaa tafuta uwanja mwingine kajenge.
Hiyo nyumba either muuze au ibomoe tu umuachie uwanja wake.
Ipo siku kaka zake watakuja wakufukuze hapo.
Watasema ni kwetu
Sisi ndio tulinunua huu uwanja
 
Hata mume siyo ndugu ila sasa mmejenga kwa ajili ya watoto...kwann mfarakane kwa vitu vya kupita mkuu
Watoto wanaweza ungana na mama kumfukuza baba.
Aafu ukute hata watoto kauziwa mbuzi kwenye gunia
 
ushauri wa bure kwa wengine unapooa na kukuta mwenzio ana umiliki wa kiwanja ama nini kitu cha kwanza mkubaliane kubadili umiliki,ni juzi jamaa alipewa kiwanja kama zawadi siku ya ndoa kutoka kwa mama mkwe badae wakajenga kwenye kiwanja ambacho kina umiliki wa mama mkwe,juzi jamaa kaambiwa afungashe virago mama anataka nyumba yake
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Aisee pole sana (ingawa hii mada sijaiona kwa wakati muafaka ila lazima nichangie kidogo pia ili wadau wengine wapate uzoefu kwa yanayotukuta sisi wanaume.
Kwanza kwa ushauri kuhusu mgogoro wenu aisee naomba ukomae NA msimamo wako.Mimi nilioa mwaka 1999 mke ambaye alikuwa NA mtoto wake wa kiume.
Yeye alikuwa anafanya biashara NA Mimi ni mtumishi.Kwa vile tulikuwa hatukai sehemu moja Siku moja week end nilikuja nyumbani tulipokuwa tumepangisha nakumbuka ulikuwa mwaka 2010! Akaniambia mume wangu nimesikia kuna kiwanja kinauzwa naomba twende tukakiangalie basi tukafuatana nikakiona NA nikaridhika nacho ila nikamuambia kwa sasa sina fedha akadai anayo akiba kdg tukinunue nikaridhia lakini nikamwambia usije ukaniletea matatizo baadae! Akasema hakutakuwa na shida yoyote BASI tukatafuta mashahidi tukaweka utaratibu tukakinunua kwa fedha yake.
Tulianza ujenzi kwa kishirikiana akipata fedha inatumika kwenye ujenzi NA Mimi Hali kadhalika.
NYUMBA iliisha tukaweka umeme tukahamia.Siku za baadae kidogo nakumbuka tulikuwa uani tunawapa chanjo kuku akanitamkia ya kuwa Nioe nimuache pale NA watoto wake (Yaani wawili
tuliozaa pamoja NA yule wakufikia) Nilistaajabu nikamwambia umri huu!
Siku zilizofuata nilishtuka nikanunua kiwanja kwa fedha yangu nikakiacha kilikuwa NA msingi wa vyumba vitatu !
Watoto walipokua NA kuajiriwa mke akaanza ujeuri NA nahisi aliwa feed watoto kuwa NYUMBA ni yake. Siku moja nilipokuwa nakagua nyaraka mbali mbali nikagundua ameiba hati ya kiwanja NA kuihamisha.....Nilichukia nikaanza ujenzi kwenye kiwanja changu mwaka 2021 January! Ile NYUMBA imeisha kiasi nimeweka umeme NA kuondoka pale nyumbani. Hakuridhika ila niliona niache ile NYUMBA tusije mwisho tukauana bure!
MY TAKE Wanawake sio wakuamini sana nakushauri uweke msimamo wa kutumia jina lako kwenye hicho kiwanja kwa kuwa dalili zinaonesha uzeeni utanyang'anywa hiyo NYUMBA.Au kama unaweza iache ilivyo utafute kiwanja ujenge nyingine hata kama ndogo Heshima itarudi!
Yaani mimi ni mwanamke, lakini mambo mengine yanafanya wanawake wote tuonekane tunajali mali kuliko ndoa. Mimi katika maisha yangu sitaki dhulma kabisa. Nina mwanaume nimenkuta ana watoto 2 , anajenga nyumba nikamuambia andika jina lako na watoto wako 2. Huyu mwingine wa kwangu ana mali zake ambazo ni zangu. Ikitokea la kutokea atarithi vyangu. Let's be fair kwenye haya maisha, mali ya dhulma haitakufikisha popote.
 
Acha tu sikujua hizo changamoto zingetokea. Ila hili limenivuruga kabisa. Yaani aliposema sema tuandike Majina yetu wote akapendekeza pia na kile kiwanja changu tufanye hivyo hivyo pia. Aise ni mtihani mkubwa.
Hahahah umeliwq kichwa. Pole sana. Ndio unajifunza sasq, hutafanya tena kosa hili hapo baadae.
 
Ukishaona mnagombea umiliki wa nyumba huku mmeoana ujue ndoa inaelekea pabaya, akikataa umiliki wa pamoja mwachie tuu, anza kujenga yako na weka clear ni yako 100% na unafanya hivyo kwa sababu ya alichofanya nyumba ya kwanza, hakikisha unajenga nzuri kuliko yake, sounds utoto lakini dawa ya moto ni moto na kisheria wote mtashindwa mtaishia kugawana nusu kwa nusu tuu
Ushauri wako kisheria si sawa. Mkishaoana chochote kinachopatikana wakati mkiwa katika ndoa ni mali ya wanandoa. Hata hiyo nyumba kama imejengwa baada ya ndoa katika kiwanja cha mke inapaswa mume alipwe fidia ya nyumba iliyojengwa katika kipindi mpo ndoani

Mtoa mada fuatilia kuhusu sheria inasemaje na haki zako katika hiyo nyumba.
 
Najaribu kuwaza, siku mvurugane kisha muachane. Anaweza kukutimua wewe na Wanao kwenye hiyo nyumba kwa Kigezo kwamba ni Jukumu lako kuwapatia Urithi wanao, halafu yeye akaingiza mwanaume mwingine wakaendelea kuishi kwenye hiyo Nyumba...
😀😀😀😀. God dictates
 
Usikubali mkuu!

Andika Watoto TU!!

Kama ndoa ina migogoro usikubali huo mkenge!!!



Mtaviziana kama wachawi vile!


Mwanamke anayepinga wanawe wasiandikwe kwenye hati ni hatari Sana!!

Kinachomfanya aogope kufanya Hivyo Ndio hatari Zaidi!

Wachout!
Mwanamke hataki watoto waandikwe ili yeye akiwahi kufa ili ndugu zake wapate mgao (wazazi )
 
Sakata lako linafanana na la kwangu. Hapa naanza kudunduliza nikatafute sehemu yangu nitoke hapa nimwachie nyumba yake. Maana nishadhalilishwa hapa ninapoishi sema navumilia kwa sababu nipo kwenye mchakato wa kutafuta hela niondoke.

Sent from my SM-J111F using JamiiForums mobile app
Mkuu mchako wa kutafuta pesa ni endelevu mpaka kifo inamaana bado upo upo
 
Hata mume siyo ndugu ila sasa mmejenga kwa ajili ya watoto...kwann mfarakane kwa vitu vya kupita mkuu
Nyumba ni kitu cha kupita???
Kiuchumi nyumba ni fixed. Siku ukiipita wewe na kuishia kutangatanga kulala kwenye penu za nyunba za watu au stand ndiyo utajua kumbe nyumba siyo kitu cha kupita
 
Nyumba ni kitu cha kupita???
Kiuchumi nyumba ni fixed. Siku ukiipita wewe na kuishia kutangatanga kulala kwenye penu za nyunba za watu au stand ndiyo utajua kumbe nyumba siyo kitu cha kupita
Vizuri
 
Kwanini msiandike majina yenu wote? Yaani watoto na wazazi? Hata wanaume huwa mna huo mchezo wa kudhulumu mali. Kwa mfano ukija kuoa mke mwengine, huyo uliejenga nae ataenda kukaa wapi wakati jina ni lako
 
Wanaume wengine bana! Unakuta mwanamke ana kiwanja yaan unaweka room mbili unataka uwe mmiliki? Unampora haki ya jasho lake? Kuna wanaume mlipewa hiyo jinsia kwa bahati mbaya kabisa! Khaaa nliolewa na mume wangu nikiwa nimeanza maisha yangu nikiwa na assets kadhaa nyumba na viwanja vikiwemo, nikwambie mwanaume wewe kuwa, haijawahi kutokea hata mume wangu akaongelea chochote kuhusu alichokikuta maana anajua hata asipomiliki yeye watoto wake ndo wamiliki! Na kuna vitu vingi amefanya juu ya hizo assets na hata haziongelei eti sjui amiliki nan, anachofanya ni kunishauri tuuu na anapitaga anaviangalia nyumba anaenda kwa wapangaji anasimamia yaan wanajua ndo mmiliki ila vyoote alivyonikuta navyo viko kwa majina yangu na alisaidia kupata hati hata haongelei khhhhaaaa namhurumia huyo mwanamke mwenzangu aisee
 
Nilivyosoma stori aisee, nimependa namna unavyoweka wazi majibu ya mke, umepata mke mwenye hekima sana, ana majibu yenye busara na upole.

Nikirudi kwako, embu rahisisha tu mambo. Mwache aandike kwa jina lake maana hata kiwanja ni chake, yaan ukiona MTU anakwambia ngoja nikajifikirie ujue bado hajaafiki, watoto analea mama pale ,wewe unakuja Mara mojamoja, kwann usimwamini mkeo, mbona kama umekaa attention sana.

Hata mkiachana kwa ajili ya watoto bado itakubidi uwaachie Nyumba(kwa mwanaume Mwenye akili hawez taka watoto wataabike pa kuishi), ulisema una kiwanja kama ulivyosema wewe ni mwanaume ,kichwa cha familia em pambana tena jenga kwenye kiwanja chako then waandike wanao.

Usitumie ubabe, tafadhali mwachie tu kama zawadi hiyo Nyumba. Ni mkeo huyo analea na kuishi hapo na watoto wako.(usipojiangalia, ndoa yako ndo inaenda kufall apart Mkuu)

kwa nini msiandike majina yenu wote ikawa ni mali ambayo nu joint owned, numeshaona hati zenye majina mawili mke na mume
 
Sasa nimeongea na mke wangu kuhusu nyumba ambayo nimejenga kwenye kiwanja chake kuhusu umiliki kwasababu yeye alitaka kuandika jina lake tena kwa siri. Nimemuuliza kwanza kwamba tangu tuoane hatujawahi kuongelea kuhusu hicho kiwanja chake.

Akanikumbusha kwamba wakati tunaoana mimi nilimshauri akiuze na ilituletea mtafaruku kweli. Na ni kweli nilisita sana kujenga kwenye kiwanja cha mke wangu kwasababu nilishaona ni mtu mpenda vyake na asiye na muda na vyangu ilihali tayari sisi ni mke na mume.

Na niwarudishe kidogo kilichonifanya nimuone wa tofauti kidogo baada ya kuhamia pale, siku moja mwisho wa mwezi nilienda kuitembelea familia. Asubuhi tukiwa mimi na watoto akaleta mada kwamba Joyce (siyo jina halisi) ambaye yeye ni shangazi kwa Joyce. Joyce ameniomba Jack (siyo jina halisi) yaani mtoto wa Joyce aje aishi hapa na aende shule akikaa kwetu.

Sasa Joyce tuliwahi kukaa naye kama ndugu yake mke wangu, akawa anatusaidia kazi lakini alikuja kuondoka kwa ugomvi na mke wangu. Aliponipa hizo stori akili yangu iliyafanya mrejeo haraka sana nikakumbuka jinsi Joyce alivyoondoka kwa shangazi yake kwa maneno.

Nikamwambia mke hilo kwasasa haitawezekana na sababu niliyompa ni kwamba mtoto wetu kwasasa anasoma 'English Medium' halafu huyu Jack akija aende shule ya kawaida (serikali) mimi sitajisikia vizuri na haitakuwa sawa hata kwa tafsiri za watu wengi.

Nikamshauri kwamba, kama ni kwa ajili ya kwenda shule basi aende kwa shemeji (kaka yake mke) ambaye kimsingi yupo karibu na shule hiyo ya serikali na ni baba mdogo wake Joyce. Mke wangu alikuja juu sana na kuzua ugomvi kidogo nimpige.

Lakini maneno yaliyonikera sana ni kwamba, mimi siwataki ndugu zake na huwa nakuja hapa kuleta vurugu na kwamba anajuta kuolewa na mimi na akakimbilia nje. Baadaye nilimuita, akaja tukaongea, nikaamua kutulia ili nione maisha yanaendaje baada ya pale.

Na hapa wiki moja kabla alinijulisha swala la kuwekewa 'bcone' kwenye like eneo, kwamba inahitahijika 100,000 akanipa na ukomo wa muda, sikutaka maneno nikampa ile hela akalipa. Niliporudi akanionesha risiti, nikamwambia wafuatilie waweke.

Wiki inayofuata akanitaarifu kwamba wameshaweka 'bcone' lakini wanahitaji paspoti saba kwa maandalizi ya hati nikamwambia sawa. Nilipoenda nikamwambia ebu nenda idara ya maji ukaulizie utaratibu wa kupata maji kwa bomba binafsi, yaani kufungiwa mita ya maji kwenye hiyo nyumba.

Alienda baadaye akaniambia wanahitaji tujaze fomu na paspoti mbili, na fomu hurusiwi kuchukua unajazia kule idara ya maji, nikamwambia sawa. Jioni akaniambia kesho nataka nikapige zile picha ajaze hizo fomu na kupeleka zile picha saba kwa ajili ya hati, mimi nikaitikia sawa.

Asubuhi kulipokucha nikamwambia simamisha hilo zoezi hadi nije. Lakini nilimpigia simu jamaa yangu ambaye naye amejaza hiyo fomu, nikamuulizi hivi hizi fomu hurusiwi kutokana nazo ukajazie nyumbani? Jamaa akasema mbona mimi nilijazie nyumbani nikarudisha?!

Nikamwambia sawa, mimi nilikuwa naendelea kukusanya taarifa zangu. Jana nikafanya ziara ya kustukiza, nikafika nyumba lakini nikiwa njiani niliandika ujumbe kumjulia hali yeye na watoto nikamwambia nipo njiani nakuja huko.

Basi nikafika yeye alikuwa ametoka na watoto, nikafungua nikaingia nikampigia akasema anakuja na kweli wakawasili na watoto, watoto wangu wananipenda sana wakafurahi stori mbili tatu.

Mimi sikutaka kikao kichukue muda, nikaanza kikao na yeye nikamwambia mimi nimekuja kwa mazungumzo na wewe, akastuka sana. Nikamwambia mazungumzo ni ya kawaida ya kifamilia. Tukaongea nikamwambia hiki kiwanja si unajua ni chako, akasema ndiyo.

Nikamwambia lakini bahati nzuri tumejaliwa kujenga nyumba ya familia, akasema ndiyo. Nikamwambia kuna vitu tusipoviweka sawa huko mbeleni vitatuletea shida, akashangaa. Nikamwambia kwasasa tunaelekea kwenye swala la umiliki sasa tuamue mimi na wewe mmliki wa nyumba ya familia yetu kwenye kiwanja chako kitakuwa na umiliki wa nani? Hana jibu!

Nikamuuliza je maji na hilo suala la picha za hati mmiliki ungeandika? Akasema mimi nilijua ni vitu vya kawaida wala sikufikiria yote hayo! Nikamuuliza kwa mkuu wa familia ni nani akasema ni wewe (mimi). Nikamuuliza sasa mbona siku ile ulifanya tu kunipa taarifa tu unataka kwenda kupiga picha bila kuuliza tuandike jina la nani? Akasema mimi niliona hata nikiandika jina langu ni sawa tu na kwasababu nilikupa taarifa niliona hakuna shida.

Nikamwambia sasa mimi natambua kwamba kiwanja ni chako lakini nimejenga nyumba ya familia yangu ambayo ni sisi sote. Nimekuja tupate mwafaka wa hicho kiwanja na mimi nipo kwa ajili kuidhamini familia yangu na katika hii familia tunaojielewa kwasasa ni mimi na wewe vijana wetu bado wadogo.

Nikamwambia mimi nina majibu yangu lakini nahitaji majibu yako juu ya kiwanja hiki. Nikamkumbusha, kwamba siku ile ulivyoongea maneno ya kwamba mimi huwa nakuja kukuletea vurugu na kwamba unajuta kuolewa na mimi nilizingatia na hivyo sitakubaki kuiweka rehani familia kwa kuruhusu mambo yaende kiholela.

Akahamaki na kudai kwanini namkumbusha mambo ya zamani, nikamwambia haikuwa sehemu ya mada lakini nimeona nikukumbushe ili ujirekebishe kimawazo, kauli na kimtazamo na ufahamu mipaka yake kama mke. Akasema yale alitamka kwa hasira kwasababu ulinikemea mbele ya watoto n.k, nikamwambia mimi uliniletea mada yako mbele ya watoto na nilipopinga wewe ndiyo ukaleta ugomvi.

Akasema tuyamalize kwanza haya ndiyo tuje swala la umiliki wa nyumba. Ila nikamwambia mimi siwezi tena kukuruhusu kumiliki hii nyumba kwasababu hustahili, utashindwa kuzuia hisia zako na utaendelea kuropoka zaidi na huenda hata kuna siku utamleta mwanaume humu na sitaweza kuzuia. Naye akasema na wewe unaweza kumleta mwanamke halafu unitoe mimi.

Mwisho akasema nimpe muda atafakari swala la umiliki wa hii nyumba halafu atanipa jibu kwamba hawezi kupata jibu la haraka. Lakini nimemwambia mimi ndiye nina wajibu na jukumu la kulinda, kuhifadhi na kutunza mali za familia hivyo yeye ni mtu wa pili kutoka kwangu na akaona ugumu nipo tayari kumpa pesa yenye thamani ya kiwanja chake, yeye atajua atazifanyaje hizo hela lakini kiwanja kiwe chini ya familia na chini yangu kama mwenyewe dhamana ya familia namba moja.

Kwa hiyo namsubiri aamue halafu nami nitaweka msimamo wa kiti. Japo sasa amenuna lakini mgonjwa haulizwi dawa. Mimi kiukweli sina mpango B ya hilo, nahitaji heshima iwepo kwangu kama mwenye nyumba na siwezi kuwa mtalii kwenye familia yangu. Lazima kiti kiheshimiwe bila hivyo panya watatawala.

Naomba kuwasilisha kwa ajili yenu kujifunza na kutoa ushauri.

Asanteni.

Pia soma: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga
Tafuta kiwanja kingine jenga nyumba mpya...alafu rudi uza hiyo nyumba ya sasa....60% ya hela baki nayo yeye mpe 40%

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa nimeongea na mke wangu kuhusu nyumba ambayo nimejenga kwenye kiwanja chake kuhusu umiliki kwasababu yeye alitaka kuandika jina lake tena kwa siri. Nimemuuliza kwanza kwamba tangu tuoane hatujawahi kuongelea kuhusu hicho kiwanja chake.

Akanikumbusha kwamba wakati tunaoana mimi nilimshauri akiuze na ilituletea mtafaruku kweli. Na ni kweli nilisita sana kujenga kwenye kiwanja cha mke wangu kwasababu nilishaona ni mtu mpenda vyake na asiye na muda na vyangu ilihali tayari sisi ni mke na mume.

Na niwarudishe kidogo kilichonifanya nimuone wa tofauti kidogo baada ya kuhamia pale, siku moja mwisho wa mwezi nilienda kuitembelea familia. Asubuhi tukiwa mimi na watoto akaleta mada kwamba Joyce (siyo jina halisi) ambaye yeye ni shangazi kwa Joyce. Joyce ameniomba Jack (siyo jina halisi) yaani mtoto wa Joyce aje aishi hapa na aende shule akikaa kwetu.

Sasa Joyce tuliwahi kukaa naye kama ndugu yake mke wangu, akawa anatusaidia kazi lakini alikuja kuondoka kwa ugomvi na mke wangu. Aliponipa hizo stori akili yangu iliyafanya mrejeo haraka sana nikakumbuka jinsi Joyce alivyoondoka kwa shangazi yake kwa maneno.

Nikamwambia mke hilo kwasasa haitawezekana na sababu niliyompa ni kwamba mtoto wetu kwasasa anasoma 'English Medium' halafu huyu Jack akija aende shule ya kawaida (serikali) mimi sitajisikia vizuri na haitakuwa sawa hata kwa tafsiri za watu wengi.

Nikamshauri kwamba, kama ni kwa ajili ya kwenda shule basi aende kwa shemeji (kaka yake mke) ambaye kimsingi yupo karibu na shule hiyo ya serikali na ni baba mdogo wake Joyce. Mke wangu alikuja juu sana na kuzua ugomvi kidogo nimpige.

Lakini maneno yaliyonikera sana ni kwamba, mimi siwataki ndugu zake na huwa nakuja hapa kuleta vurugu na kwamba anajuta kuolewa na mimi na akakimbilia nje. Baadaye nilimuita, akaja tukaongea, nikaamua kutulia ili nione maisha yanaendaje baada ya pale.

Na hapa wiki moja kabla alinijulisha swala la kuwekewa 'bcone' kwenye like eneo, kwamba inahitahijika 100,000 akanipa na ukomo wa muda, sikutaka maneno nikampa ile hela akalipa. Niliporudi akanionesha risiti, nikamwambia wafuatilie waweke.

Wiki inayofuata akanitaarifu kwamba wameshaweka 'bcone' lakini wanahitaji paspoti saba kwa maandalizi ya hati nikamwambia sawa. Nilipoenda nikamwambia ebu nenda idara ya maji ukaulizie utaratibu wa kupata maji kwa bomba binafsi, yaani kufungiwa mita ya maji kwenye hiyo nyumba.

Alienda baadaye akaniambia wanahitaji tujaze fomu na paspoti mbili, na fomu hurusiwi kuchukua unajazia kule idara ya maji, nikamwambia sawa. Jioni akaniambia kesho nataka nikapige zile picha ajaze hizo fomu na kupeleka zile picha saba kwa ajili ya hati, mimi nikaitikia sawa.

Asubuhi kulipokucha nikamwambia simamisha hilo zoezi hadi nije. Lakini nilimpigia simu jamaa yangu ambaye naye amejaza hiyo fomu, nikamuulizi hivi hizi fomu hurusiwi kutokana nazo ukajazie nyumbani? Jamaa akasema mbona mimi nilijazie nyumbani nikarudisha?!

Nikamwambia sawa, mimi nilikuwa naendelea kukusanya taarifa zangu. Jana nikafanya ziara ya kustukiza, nikafika nyumba lakini nikiwa njiani niliandika ujumbe kumjulia hali yeye na watoto nikamwambia nipo njiani nakuja huko.

Basi nikafika yeye alikuwa ametoka na watoto, nikafungua nikaingia nikampigia akasema anakuja na kweli wakawasili na watoto, watoto wangu wananipenda sana wakafurahi stori mbili tatu.

Mimi sikutaka kikao kichukue muda, nikaanza kikao na yeye nikamwambia mimi nimekuja kwa mazungumzo na wewe, akastuka sana. Nikamwambia mazungumzo ni ya kawaida ya kifamilia. Tukaongea nikamwambia hiki kiwanja si unajua ni chako, akasema ndiyo.

Nikamwambia lakini bahati nzuri tumejaliwa kujenga nyumba ya familia, akasema ndiyo. Nikamwambia kuna vitu tusipoviweka sawa huko mbeleni vitatuletea shida, akashangaa. Nikamwambia kwasasa tunaelekea kwenye swala la umiliki sasa tuamue mimi na wewe mmliki wa nyumba ya familia yetu kwenye kiwanja chako kitakuwa na umiliki wa nani? Hana jibu!

Nikamuuliza je maji na hilo suala la picha za hati mmiliki ungeandika? Akasema mimi nilijua ni vitu vya kawaida wala sikufikiria yote hayo! Nikamuuliza kwa mkuu wa familia ni nani akasema ni wewe (mimi). Nikamuuliza sasa mbona siku ile ulifanya tu kunipa taarifa tu unataka kwenda kupiga picha bila kuuliza tuandike jina la nani? Akasema mimi niliona hata nikiandika jina langu ni sawa tu na kwasababu nilikupa taarifa niliona hakuna shida.

Nikamwambia sasa mimi natambua kwamba kiwanja ni chako lakini nimejenga nyumba ya familia yangu ambayo ni sisi sote. Nimekuja tupate mwafaka wa hicho kiwanja na mimi nipo kwa ajili kuidhamini familia yangu na katika hii familia tunaojielewa kwasasa ni mimi na wewe vijana wetu bado wadogo.

Nikamwambia mimi nina majibu yangu lakini nahitaji majibu yako juu ya kiwanja hiki. Nikamkumbusha, kwamba siku ile ulivyoongea maneno ya kwamba mimi huwa nakuja kukuletea vurugu na kwamba unajuta kuolewa na mimi nilizingatia na hivyo sitakubaki kuiweka rehani familia kwa kuruhusu mambo yaende kiholela.

Akahamaki na kudai kwanini namkumbusha mambo ya zamani, nikamwambia haikuwa sehemu ya mada lakini nimeona nikukumbushe ili ujirekebishe kimawazo, kauli na kimtazamo na ufahamu mipaka yake kama mke. Akasema yale alitamka kwa hasira kwasababu ulinikemea mbele ya watoto n.k, nikamwambia mimi uliniletea mada yako mbele ya watoto na nilipopinga wewe ndiyo ukaleta ugomvi.

Akasema tuyamalize kwanza haya ndiyo tuje swala la umiliki wa nyumba. Ila nikamwambia mimi siwezi tena kukuruhusu kumiliki hii nyumba kwasababu hustahili, utashindwa kuzuia hisia zako na utaendelea kuropoka zaidi na huenda hata kuna siku utamleta mwanaume humu na sitaweza kuzuia. Naye akasema na wewe unaweza kumleta mwanamke halafu unitoe mimi.

Mwisho akasema nimpe muda atafakari swala la umiliki wa hii nyumba halafu atanipa jibu kwamba hawezi kupata jibu la haraka. Lakini nimemwambia mimi ndiye nina wajibu na jukumu la kulinda, kuhifadhi na kutunza mali za familia hivyo yeye ni mtu wa pili kutoka kwangu na akaona ugumu nipo tayari kumpa pesa yenye thamani ya kiwanja chake, yeye atajua atazifanyaje hizo hela lakini kiwanja kiwe chini ya familia na chini yangu kama mwenyewe dhamana ya familia namba moja.

Kwa hiyo namsubiri aamue halafu nami nitaweka msimamo wa kiti. Japo sasa amenuna lakini mgonjwa haulizwi dawa. Mimi kiukweli sina mpango B ya hilo, nahitaji heshima iwepo kwangu kama mwenye nyumba na siwezi kuwa mtalii kwenye familia yangu. Lazima kiti kiheshimiwe bila hivyo panya watatawala.

Naomba kuwasilisha kwa ajili yenu kujifunza na kutoa ushauri.

Asanteni.

Pia soma: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga
1. Kwa kuwa, umekiri kwamba ninyi ni wanandoa (mmefunga ndoa), na,
2. Kwa kuwa, umekiri pia kwamba mna watoto wenu wa wawili ambao wamezaliwa ndani ya ndoa.
Hivyo Basi, suluhisho sahihi zaidi kuhusiana na hili suala lako ni:-
(I) AIDHA, Ardhi hiyo mnapaswa kuimiliki kwa pamoja nyinyi wote wawili kwa umiliki wa pamoja (Joint Occupation or by means of Occupation in Common.
(a) Mmiliki Ardhi hiyo wote kwa pamoja kwa umiliki wenye maslahi yasiyogawanyika, yaani Joint Tenants (Matrimonial Property).
Majina yenu wote wawili (jina lako na la huyo mwanamke) yawepo kwenye Hati ya Umiliki wa Ardhi, hii itaondoa utata na wasiwasi wa kudhulumiana hiyo Ardhi.
(b) Mmiliki Ardhi hiyo wote kwa pamoja kwa Hisa, yaani Common Occupiers in Shares. Mnaweza mkagawana Hisa za umiliki wa hiyo Ardhi, kila Mwanandoa anaweza akamiliki Ardhi hiyo kwa Hisa ya 50% au vinginevyo kwa kadiri mtakavyokubaliana ninyi wenyewe kwa hiyari yenu.

( ii) AU, Wote wawili, yaani wewe na mkeo mnaweza mkajitoa kwenye suala la Umiliki wa hiyo Ardhi, badala yake Ardhi hiyo muimilikishe kwa Watoto wenu na nyinyi mkabaki kuwa wasimamizi tu wa Ardhi husika (Guardianship) hadi hapo watoto wenu watakapofikia umri wa utu uzima wa miaka 18 au zaidi.

NB: Nimeshauri kulingana na uzoefu wangu binafsi wa kimataifa, yawezekana pengine ushauri wangu unakinzana na matakwa ya Sheria za Tanzania, Sina uhakika kuhusu suala hili lakini.
Lakini sehemu nyingi Sana ambazo nimewahi kuzuru, ushauri Kama huu umesaidia Sana katika kutatua Migogoro Kama huu wa kwako.
Naomba kuwasilisha.
I stand to be corrected!
 
Back
Top Bottom