Mrejesho: Ni baada ya kupatiwa matibabu dhidi ya ugonjwa ulionikumba ghafla hadi kupelekea kulazwa hospitalini kwa siku mbili(2)

Mungu ni mwema mkuu akupe afya njema urudi kwenye hali yako ya zamani πŸ™πŸ™ dua zetu tu pamoja nawe
 
Umelazwa siku mbili unalialia hivi, laiti ungejua kuna watu wanapitia makubwa kuliko yako basi usingedeka humu.

Halafu kuumwa ni ibada sasa nini kinachokufanya ulielie na kutia huruma,je unadhani pole za watu ndio zimekufanya upone? Ongea na Mungu wako.
 
Sikuwa na lengo la kuonyesha kuwa nalia hapana ila umenielewa tofauti..

Hii ni sehemu ya Shukrani zangu kwa wanajamii wenzangu kwa moyo wa upendo walionyesha na kuguswa juu ya nilichopitia na hata mungu nimemkumbuka kwa sala na toba pia..Ahsante kwa ushauri wako.
 
Chemsha samaki halafu ichemkee sana unywe na supu usiweke nyanya ni hivyo hivyo na chumvi kidogo sana , penda mayai, mboga ya majani ni spinach na salad usiweke nyanya weka karoti , kitunguu , penda mafuta ya majani olive oil , au elianto usiweke nyingi sana wastani ila izidi mboga kidogo , nyama ya ng'ombe na uchemshe bila kuweka chochote.

Vizazi vitami, mihogo,siagi ya karanga , uji lishe weka blue band,kuku pia ni nzuri sana mwaya ukichemsha na kabeji kidogo Kwa mbali ila kabeji iliyo chemshwa tayari , ndio uweke kwenye hiyo supu penda karoti sana sio nyanya Tena na acha pombe good day
 
Sawa Ahsante sana nitazingatia haya ndio vitakua vyakula vyangu kuanzia sasa shukrani kwa msaada wa ushauri wako.

Ubarikiwe sanaπŸ™πŸΌ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…