MREJESHO: Niliomba ushauri juu ya sehemu sahihi ya kutoa fungu la kumi

MREJESHO: Niliomba ushauri juu ya sehemu sahihi ya kutoa fungu la kumi

Hiyo ndio sadaka ya kweli sasa sio ile wapuuzi anapandwa mzuka anaenda kumpa mhuni fulani huku akinengua viuno kisa kaambiwa mwaka huu utapata nyumba na gari.
Yani unaenda kumpa mtu hela akanunue V8 au akajenge Hotel halafu unaona umetoa sadaka wakati kuna maelfu hawana hata chakula.
Kama huwa unafanya hivyo jihesabu wewe ni kiazi mbatata,mpuuzi asiye na akili ya ubinadamu.
Na hii ni kwa wote wale wa makanisa ya mwendokasi na yale makongwe,tuache ufala
 
Baada ya kuomba ushauri hapa jukwaani, watu walichangia kwa hekima, kuna waliosisitiza nikatoe mahala ninapoabudu pia kuna walionishauri nikatoe kwa watu wenye uhitaji.
Pia kunawaliosema nikatoe ninapoabudu halafu pia nikatoe kwa wahitaji.

WOTE MLIOCHANGIA, NAWASHUKURU SANA.

Mm na mke wangu tulionelea tukatoe kwenye kituo cha yatima.

Si kwamba hatuheshimu madhabahu, Ni kwamba uwezo wetu kwa sasa ni duni hatuwezi kumudu kutoa sehemu zote mbili.

Hata huko kwa yatima tulikoenda tulienda kwa aibu, maana tulichonacho nikidogo mno.

Ila mkipata nafasi nendeni mkawaone hao watoto, maana kwa mujibu wa alietupokea ni kwamba several times wanalia uji.

Ni hayo tu.
ITOSHE KUSEMA AHSANTE KWA USHIRIKIANO
Nilijizuia kusema cho chote kwenye uzi wa swali, lakini kwa kuwa umeshatekeleza, acha na mimi niseme kidogo kwa njia ya ushuhuda binafsi.

Kwa mtazamo wangu, fungu la kumi ni la Mungu. Na kama ndivyo, anaweza kuamua itakavyotumika.

Nilianza kujifunza masuala ya fungu la kumi kwenye miaka ya elfu mbili hivi, mmoja wa walimu wangu wa mwanzoni kabisa akiwa ni dada yangu katika ukoo ambaye tulikuwa tukisali madhehebu tofauti.

Alinifundisha kwa msisitizo mkubwa sana umuhimu wa kutoa fungu la kumi. Na aliniambia, mahali pekee pa kulitoa fungu la kumi ni Kanisani ninakoabudu (Hata hivyo, kwa miaka ya hivi karibuni, amebadilisha mtazamo).

Na mimi nilijitajidi kufanya hivyo tokea kipindi hicho.

Lakini miaka kadhaa baadaye, nikamsikia mtumishi mmoja akifundisha kuwa kwa kuwa fungu la kumi ni la Mungu, hupaswi kutoa tu mahali po pote, bali umwulize kwanza ndipo upeleke atakakokuelekeza. Kupitia mafundisho hayo, nilifahamu kuwa Mungu anaweza akakuelekeza ulipeleke hilo fungu la kumi Kanisani, kwa Mchungaji, kwa mtumishi, kwa yatima, kwa mjane, kwa mhitaji, n.k.

Siku zilienda, na hatimaye mwishoni mwa mwaka 2006, nikapata nafasi ya kulifanyisha hilo kazi. Baada ya kupata kimuujiza "kibarua" mahali fulani, nililitenga fungu la kumi, na kuiahidi nafasi yangu kuwa safari hiyo, sitapeleka tu Kanisani kama kama kawaida, bali atakakonielekeza Mungu. Japo sikujua angenijibuje, lakini nilidhamiria kuitii sauti Yake.

Niliichukua hiyo sadaka nikaiweka kwenye bahasha na kuanza kuiombea kila siku Mungu anielekeze anakotaka niipeleke. Niliomba kwa siku kadhaa lakini sikusikia chochote, wala kupata ishara yo yote ile kuhusiana na hilo.

Niliamua kubadilisha namna ya uombaji. Nilianza kuomba kwa kumweleza Mungu anijulishe anakotaka hiyo sadaka iende kati ya maeneo matatu: mahali nilikokuwa nikiabudi, kwenye huduma ya mtumishi fulani niliyekuwa nikibarikiwa sana na huduma yake, au kwa watoto yatima.

Kituo chenyewe cha watoto hakikuwa kikubwa. Ilikuwa ni huduma iliyoanzishwa na dada yangu katika ukoo (aliyenifundisha kutoa fungu la kumi) akishirikiana na rafiki yake. Kwa kuwa rafiki yake alikuwa na nyumba kubwa, na dada yangu alikuwa anapenda sana kuwasaidia watoto wahitaji, alimshwawishi rafiki yake
mpaka akakubali waitumie nyumba yake kuanzisha huduma ya watoto. Hawakuwa na maandalizi yo yote, waliamua kuanza na kidogo walichokuwa nacho.

Sasa, nilipokuwa nimeanza kuomba kwa kuyataja hayo maeneo matatu, kulitokea hali fulani ambayo niliichukulia kuwa ni ishara ya maombi kujibiwa. Siku moja niliamka, na nilipotaka kuendelea kuomba kumwuliza Mungu, sikujisikia kuomba. Na nilipofikiria kuipeleka hiyo sadaka Kanisani ninakoabudu au kwenye huduma ya mtumishi binafsi, moyo wangu ulikataa kabisa. Nilikuwa nikikosa amani kabisa kila nilipofikiria kuipeleka Kanisani au kwenye huduma ya mhubiri binafsi. Ilikuwa nikiwazia tu mojawapo ya hayo maeneo mawili, nilikuwa nahisi hali ya mshtuko wa kupgofya sana. Ni kama vile ningeenda kufa kama ningepeleka maeneo hayo.

Lakini nilipofikiria kuipeleka kwenye kituo cha watoto kilichokuwa kinasimamiwa na hao wadada, nilikuwa nikipata amani ya hali ya juu mno. Niliamua kusubiri hadi kesho yake kuona kama hiyo hali itabdilika.

Lakini hata kesho yake, hali ilikuwa vile vile. Kwa siku hiyo, niliamua kuwa siku hiyo, nitakapoenda kula chakula cha Mchana, nitaipeleka hiyo sadaka.


Mchana, baada ya kumaliza kula, kwenye saa tisa Alasiri, niliamua kuahirisha tena hadi Jioni nitakaporidi kutoka kazini. Kwa sababu nilikuwa nikifundisha tuisheni mahali fulani, nililichukua daftari lenye notisi nikaanza safari ya kwenda kwenye kipindi, akilini nikiwa na wazo kuwa nirudipo tu, naipeleka hiyo sadaka kwa hao wadada wanaowalea watoto wahitaji.

Lakini nilipokuwa njiani kuelekea kwenye kipindi, tena nikiwa nimefika katikakati ya safari, kulitokea kiti cha ajabu kilichoniogofya mno. Nilijishtukizia kama vile nimekamatwa bega la kulia na kushoto na kugeuzwa ghafala kwa nguvu nikajikuta nimetazama nilikotokea. Sikumwona mtu yeyote aliyenishika na kunigeuza, lakini nilielewa maana yake.

Kwa haraka sana , nilienda hadi nyumbani nikaitupa mezani daftari na kuichukua hiyo sadaka ambayo tayari nilikuwa nimeshaiweka kwenye bahasha, na moja kwa moja hadi nyumbani wanakolelewa hao watoto wahitaji.

Nilimkuta mmoja wa hao wasimamizi wa hicho kituo. Dada "yangu" yeye hakuwepo muda huo.

Nilipofika, nilimkabidhi hiyo bahasha huyo niliyemkuta na kumwambia huo ni i ujumbe niliopata kibali kuupeleka hapo. Nilikwepa kumwambia kuwa ni fungu la kumi kwa sababu nilihofia huenda wasingepokea. Baada tu ya kukabidhi na kumwambia hayo, alitamka hivi"Mungu wa Israeli", na kubaki akiwa ameduwaa. Ili asije akapata nafasi ya kunihoji, niliamua kuaga na kuondoka huku yeye akiwa angali ameduwaa. Wakati naondoka, na mimi nilikuwa namshangaa kilichomduwaza wakati hajui kilichomo humo kwenye bahasha niliyomkabidhi.

Siku chache baadaye, nilionana na mwenzake ambaye hakusita kunisimulia ushuhuda waliotendewa na Mungu kwenye huduma yao ya kuhudumia watoto.

Alinisimulia kuwa siku niliyopeleka hiyo sadaka, walikuwa wameishiwa na mahitaji muhimu ukiwemo unga. Na Jana yake Usiku, baada ya kushauriana cha kufanya, waligundua kuwa hawakuwa na ujanja zaidi ya kuomba. Walikubaliana kumwomba Mungu kwa kuisimamia Ahadi ya Neno Lake kuwa Yeye ni Baba wa yatima. Walimweleza kuwa watoto Wake hawakuwa na chakula kwa hiyo awapelekee hela ya chakula.

Aliendelea kunisimulia kuwa Usiku, Mungu "aliwaonesha" kuwa kesho yake hela itapelekwa. Kwa hiyo kilipokucha, walimshikuru Mungu na kuendelea kusubiria pesa kwa shauku kubwa mno.

Asubuhi ilipita bila ya hela kupelekwa. Mchana nao ukapita vivyo hivyo. Kumbuka watoto walikuwa hawana hata unga wa uji, na walishakubaliana kuwa hawataenda kukopa popote, watasubiria mpaka Mungu awapelekee. Ingelikuwa ni wewe ungefanyeje? Unafikiri wao walifanyeje zaidi ya kumwuliza Mungu pesa aliyowaahidi?

Mpaka hapo, kama unaamini kuwa ni kweli Mungu aliwaonesha hela ikipelekwa hapo kituoni kwao, utanilewa ni nini kilichonigeuza ghafla kinyume na ratiba yangu na hatimaye nikaenda kuipeleka hiyo hela.

Kwa hiyo ungeniuliza mimi suala la fungu la kumi, ningekujibu kuwa ni sahihi kupeleka Kanisani, ni sahihi kuwapa watumishi wa Mungu, ni sahihi kuwapa yatima, wajane, wahitaji mbali mbali, n.k. lakini muhimu, msikilize Mungu kwanza.

Mungu akisema nawe, na ukawa na uhakika kuwa ni Mungu, fanya akuambiavyo hata kama ni kinyume na dini yenu.
 
Baada ya kuomba ushauri hapa jukwaani, watu walichangia kwa hekima, kuna waliosisitiza nikatoe mahala ninapoabudu pia kuna walionishauri nikatoe kwa watu wenye uhitaji.
Pia kunawaliosema nikatoe ninapoabudu halafu pia nikatoe kwa wahitaji.

WOTE MLIOCHANGIA, NAWASHUKURU SANA.

Mm na mke wangu tulionelea tukatoe kwenye kituo cha yatima.

Si kwamba hatuheshimu madhabahu, Ni kwamba uwezo wetu kwa sasa ni duni hatuwezi kumudu kutoa sehemu zote mbili.

Hata huko kwa yatima tulikoenda tulienda kwa aibu, maana tulichonacho nikidogo mno.

Ila mkipata nafasi nendeni mkawaone hao watoto, maana kwa mujibu wa alietupokea ni kwamba several times wanalia uji.

Ni hayo tu.
ITOSHE KUSEMA AHSANTE KWA USHIRIKIANO
Inaelekea hujui maana ya fungu la kumi.

Fungu la kumi kamwe haliwezi kuwa dogo au kubwa ni 10% ya faida au mapato yako.

Kama una 20,000 hivyo sehemu ya kumi ni 2,000. Hii sio ndogo bali tunaita zaka kamili, hujapunguza kitu
 
Hongera mkuu, kanisani pia kuna sanduku maalumu kwa ajili ya yatima, na wengi wanaohudumiwa na kanisa ni wale wanaoishi majumbani aidha na bibi
zao ama ndugu wa karibu ambao baadhi yao wanaishi hali duni.

Kuna nyakati tunapitia wakati mwingine, ila unakuta unapitishwa pale ili ujifunze na kubadilika.

Mungu atutie nguvu tusijipende wenyewe
 
Hongera na Ubarikiwe sana, na umetoa sehemu sahihi ata kama ni kidogo.
 
Kuna Zaka, Dhabihu na Malimbuko

Zaka - Madhabahuni kwa kuhani au Mtumishi wako anayekuhudumia...hata kama sio kanisani kwako

Dhabihu - Popote hata kwa watoto yatima, Wagonjwa, Wafungwa n.k

Malimbuko - ni Uzao wa kwanza wa mifugo yako au mazao ya kwanza katika kuvuna

Nijuavyo ni hivyo
Upo sahihi mtumishi lakini lakini kwenye dhabihu ni sadaka isiyo usisha fedha inaweza kuwa mifugo, chakula nk kama sijakosea, sehem
 
Baada ya kuomba ushauri hapa jukwaani, watu walichangia kwa hekima, kuna waliosisitiza nikatoe mahala ninapoabudu pia kuna walionishauri nikatoe kwa watu wenye uhitaji.

Pia kunawaliosema nikatoe ninapoabudu halafu pia nikatoe kwa wahitaji.

WOTE MLIOCHANGIA, NAWASHUKURU SANA.

Mm na mke wangu tulionelea tukatoe kwenye kituo cha yatima.

Si kwamba hatuheshimu madhabahu, Ni kwamba uwezo wetu kwa sasa ni duni hatuwezi kumudu kutoa sehemu zote mbili.

Hata huko kwa yatima tulikoenda tulienda kwa aibu, maana tulichonacho nikidogo mno.

Ila mkipata nafasi nendeni mkawaone hao watoto, maana kwa mujibu wa alietupokea ni kwamba several times wanalia uji.

Ni hayo tu.
ITOSHE KUSEMA AHSANTE KWA USHIRIKIANO
Mtumishi usijali umetoa kiasi gani Mungu wetu haangalii umetoa kidogo anaangalia dhamira na je hiyo sadaka uliyotoa umejinyima vingapi, sadaka ina siri kubwa sana katika kukufanikisha, kuna andiko linasema ukiwa mtoaji hata kama unamkosea Mungu basi Mungu hataangalia mabaya yako na na atakubariki. Ila siku nyingine zaka peleka madhabahuni, hiyo uliyopeleka chukulia tu kama umetoa msaada kwa watu wenye uhuitaji maalumu
 
Kuna Zaka, Dhabihu na Malimbuko

Zaka - Madhabahuni kwa kuhani au Mtumishi wako anayekuhudumia...hata kama sio kanisani kwako

Dhabihu - Popote hata kwa watoto yatima, Wagonjwa, Wafungwa n.k

Malimbuko - ni Uzao wa kwanza wa mifugo yako au mazao ya kwanza katika kuvuna

Nijuavyo ni hivyo


Usimshauri, hata kuelewa, ni either ana wivu na mchungaji wake au hamwamini, bora ahame kwa anayemwamini na atoe zaka mazabahuni.
 
Baada ya kuomba ushauri hapa jukwaani, watu walichangia kwa hekima, kuna waliosisitiza nikatoe mahala ninapoabudu pia kuna walionishauri nikatoe kwa watu wenye uhitaji.

Pia kunawaliosema nikatoe ninapoabudu halafu pia nikatoe kwa wahitaji.

WOTE MLIOCHANGIA, NAWASHUKURU SANA.

Mm na mke wangu tulionelea tukatoe kwenye kituo cha yatima.

Si kwamba hatuheshimu madhabahu, Ni kwamba uwezo wetu kwa sasa ni duni hatuwezi kumudu kutoa sehemu zote mbili.

Hata huko kwa yatima tulikoenda tulienda kwa aibu, maana tulichonacho nikidogo mno.

Ila mkipata nafasi nendeni mkawaone hao watoto, maana kwa mujibu wa alietupokea ni kwamba several times wanalia uji.

Ni hayo tu.
ITOSHE KUSEMA AHSANTE KWA USHIRIKIANO
2 Wakorintho 9:7......inasema hivi, mtoe kwa ukunjufu (cheerful giver)

7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

8 Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;

9 kama ilivyoandikwa, Ametapanya, amewapa maskini, Haki yake yakaa milele.

10 Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu;

11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.
 
Pia vipo vituo feki ambavyo sio yatima bali watoto wa mazingira magumu. Watoto ambao wana wazazi wote ila hali ngumu.

Wengine yalitukuta.

Sasa tumeamua kushiriki ujenzi wa makanisa...haswa yale machanga.. mtumishi ana wito haswa, waumini wachache wasio na kitu...
 
Kuna Zaka, Dhabihu na Malimbuko

Zaka - Madhabahuni kwa kuhani au Mtumishi wako anayekuhudumia...hata kama sio kanisani kwako

Dhabihu - Popote hata kwa watoto yatima, Wagonjwa, Wafungwa n.k

Malimbuko - ni Uzao wa kwanza wa mifugo yako au mazao ya kwanza katika kuvuna

Nijuavyo ni hivyo
Hapo kwenye malimbuko. Mimi nafuga mbwa....naweza peleka?
 
Baada ya kuomba ushauri hapa jukwaani, watu walichangia kwa hekima, kuna waliosisitiza nikatoe mahala ninapoabudu pia kuna walionishauri nikatoe kwa watu wenye uhitaji.

Pia kunawaliosema nikatoe ninapoabudu halafu pia nikatoe kwa wahitaji.

WOTE MLIOCHANGIA, NAWASHUKURU SANA.

Mm na mke wangu tulionelea tukatoe kwenye kituo cha yatima.

Si kwamba hatuheshimu madhabahu, Ni kwamba uwezo wetu kwa sasa ni duni hatuwezi kumudu kutoa sehemu zote mbili.

Hata huko kwa yatima tulikoenda tulienda kwa aibu, maana tulichonacho nikidogo mno.

Ila mkipata nafasi nendeni mkawaone hao watoto, maana kwa mujibu wa alietupokea ni kwamba several times wanalia uji.

Ni hayo tu.
ITOSHE KUSEMA AHSANTE KWA USHIRIKIANO
Na kuhusu zaka inatakiwa iende madhabahuni, nakuonyesha andiko nilete linalosema juu ya zaka msichanganye tu, nia ni nzuri ya kutoa zaka ila unatakiwa ujue kila sadaka ina mahali pake na ni muhumi kutambua hilo.
 
Mambo ya Walawi 27.....

Mtambue zaka ni za kupeleka madhabahuni, kwa kuhani/padri/mchungaji wako


1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Hapo mtu atakapoondoa nadhiri, hizo nafsi za watu zitakuwa kwa Bwana, kama utakavyowahesabia wewe.

3 Na hesabu yako itakuwa kwa mtu mume, tokea aliye na umri wa miaka ishirini hata umri wa miaka sitini, hesabu yako itakuwa shekeli hamsini za fedha, kwa shekeli ya mahali patakatifu.

4 Kama ni mwanamke, hesabu yako itakuwa shekeli thelathini.

5 Tena akiwa mwenye umri wa miaka mitano hata umri wa miaka ishirini, ndipo hesabu yako itakuwa shekeli ishirini kwa mwanamume, na shekeli kumi kwa mwanamke.

6 Tena akiwa mwenye umri wa mwezi mmoja hata umri wa miaka mitano, ndipo hesabu yako itakuwa shekeli tano za fedha kwa mwanamume, na hesabu yako itakuwa shekeli tatu za fedha kwa mwanamke.

7 Tena akiwa mwenye umri wa miaka sitini na kuzidi; kama ni mwanamume, hesabu yako itakuwa shekeli kumi na tano, na kwa mwanamke shekeli kumi.

8 Lakini kwamba ni maskini zaidi ya kuhesabu kwako, ndipo atawekwa mbele ya kuhani, na huyo kuhani atamtia kima; kama uwezo wake huyo aliyeweka nadhiri ulivyo, ndivyo kuhani atakavyomtia kima.

9 Tena kama ni mnyama wa namna ambayo watu husongeza kuwa sadaka kwa Bwana, kila mmoja katika wanyama hao atakayetolewa kwa Bwana, na mtu ye yote, atakuwa ni mtakatifu.

10 Yeye hatamgeuza, wala kumbadili mwema kwa mbaya, au mbaya kwa mwema; kwamba atabadili mnyama kwa mnyama ye yote, ndipo mnyama huyo na yule waliobadiliwa wote wawili watakuwa watakatifu.

11 Na kama ni mnyama ye yote asiye safi, wa namna ambayo hawamsongezi kwa Bwana, basi atamweka huyo mnyama mbele ya kuhani;

12 na kuhani atamtia kima, akiwa mwema akiwa mbaya; kama wewe kuhani utakavyomtia kima, ndivyo itakavyokuwa.

13 Lakini kwamba ataka kumkomboa kweli, ndipo atakapoongeza sehemu ya tano juu ya hesabu yako.

14 Na mtu atakapoiweka nyumba yake iwe wakfu kwa Bwana ndipo kuhani ataihesabu kima chake hiyo nyumba, ikiwa njema ikiwa mbaya; kama kuhani atakavyoihesabu kima chake ndivyo itakavyokuwa.

15 Tena mtu huyo aliyeweka nyumba yake iwe wakfu kama akitaka kuikomboa, ndipo atakapoongeza sehemu ya tano ya hiyo fedha ya hesabu yako, nayo itakuwa mali yake.

16 Tena kama mtu akiweka wakfu kwa Bwana sehemu ya shamba la milki yake, ndipo hesabu yako itakuwa kama kule kupanda kwake kulivyo; kupanda kwake homeri moja ya mbegu ya shayiri, kutahesabiwa kuwa ni shekeli hamsini za fedha.

17 Kwamba anaweka shamba lake liwe wakfu tangu mwaka wa yubile, litasimama vivyo kama hesabu yako ilivyo.

18 Lakini akiliweka shamba lake wakfu baada ya yubile, ndipo kuhani atamhesabia hiyo fedha kama hesabu ya miaka iliyobaki hata mwaka wa yubile, na kuhesabiwa kwako kutapunguzwa.

19 Na kama yeye aliyeliweka shamba wakfu akitaka kulikomboa kweli, ndipo atakapoongeza sehemu ya tano ya hiyo fedha ya hesabu yako, nalo litathibitishwa kwake.

20 Lakini asipotaka kulikomboa shamba, au kama amemwuzia mtu mwingine hilo shamba, halitakombolewa tena kabisa;

21 ila hilo shamba litakuwa takatifu kwa Bwana litakapotoka katika yubile, kama ni shamba lililowekwa wakfu; litakuwa mali ya kuhani.

22 Tena kama akiweka wakfu kwa Bwana shamba ambalo amelinunua, ambalo si shamba la milki yake;

23 ndipo kuhani atamhesabia kima cha kuhesabu kwako hata mwaka wa yubile: naye atatoa siku hiyo kama hesabu yako, kuwa ni kitu kitakatifu kwa Bwana.

24 Mwaka wa yubile shamba hilo litarejea kwake huyo ambaye lilinunuliwa kwake, yaani, huyo ambaye nchi hiyo ni milki yake.

25 Na hesabu zako zote zitaandamana shekeli ya mahali patakatifu; gera ishirini zitakuwa shekeli moja.

26 Mzaliwa wa kwanza tu katika wanyama, aliyewekwa kuwa mzaliwa wa kwanza kwa Bwana, mtu awaye yote hatamweka kuwa mtakatifu; kama ni ng'ombe, kama ni kondoo, huyo ni wa Bwana.

27 Na kama ni wa mnyama asiye safi, ndipo atamkomboa kama hesabu yako ilivyo, naye ataongeza sehemu ya tano ya bei yake; au asipokombolewa, ndipo atauzwa kama hesabu yako ilivyo.

28 Pamoja na hayo, hakitauzwa wala kukombolewa kitu cho chote kilichowekwa wakfu, ambacho mtu amekiweka wakfu kwa Bwana, katika vitu vyote alivyo navyo, kama ni mtu, au mnyama, au kama ni shamba la milki yake; kila kitu kilichowekwa wakfu ni kitakatifu sana kwa Bwana.

29 Kila aliyewekwa wakfu, aliyewekwa wakfu na binadamu, hatakombolewa; sharti atauawa.

30 Tena zaka yote ya nchi, kama ni mbegu ya nchi, au kama ni matunda ya nchi, ni ya Bwana; ni takatifu kwa Bwana.

31 Na kama mtu akitaka kukomboa cho chote cha zaka yake, ataongeza sehemu yake ya tano juu yake.

32 Tena zaka yote ya ng'ombe, au ya kondoo, kila apitaye chini ya fimbo; sehemu ya kumi watakuwa ni watakatifu kwa Bwana.

33 Hataangalia kwamba ni mwema au kwamba ni mbaya, wala hatambadili; na kama akimbadili na yo yote, ndipo wote wawili, huyo na huyo waliobadiliwa watakuwa ni watakatifu; hatakombolewa.

34 Haya ndiyo maagizo, Bwana aliyomwagiza Musa kwa ajili ya wana wa Israeli katika mlima wa Sinza
 
Kuna Zaka, Dhabihu na Malimbuko

Zaka - Madhabahuni kwa kuhani au Mtumishi wako anayekuhudumia...hata kama sio kanisani kwako

Dhabihu - Popote hata kwa watoto yatima, Wagonjwa, Wafungwa n.k

Malimbuko - ni Uzao wa kwanza wa mifugo yako au mazao ya kwanza katika kuvuna

Nijuavyo ni hivyo

Barikiwa sana,huu ndio muongozo
 
Hiyo ndio sadaka ya kweli sasa sio ile wapuuzi anapandwa mzuka anaenda kumpa mhuni fulani huku akinengua viuno kisa kaambiwa mwaka huu utapata nyumba na gari.
Yani unaenda kumpa mtu hela akanunue V8 au akajenge Hotel halafu unaona umetoa sadaka wakati kuna maelfu hawana hata chakula.
Kama huwa unafanya hivyo jihesabu wewe ni kiazi mbatata,mpuuzi asiye na akili ya ubinadamu.
Na hii ni kwa wote wale wa makanisa ya mwendokasi na yale makongwe,tuache ufala

Usimpotoshe zaka unapeleka mahali unapo abudia kwaajili ya kazi ya bwana kama unapoabudia unapaona chenga nenda sehemu unayoona ni sahihi kaabudu na kutoa zaka hapo.
 
Kuna Zaka, Dhabihu na Malimbuko

Zaka - Madhabahuni kwa kuhani au Mtumishi wako anayekuhudumia...hata kama sio kanisani kwako

Dhabihu - Popote hata kwa watoto yatima, Wagonjwa, Wafungwa n.k

Malimbuko - ni Uzao wa kwanza wa mifugo yako au mazao ya kwanza katika kuvuna

Nijuavyo ni hivyo

Mnatoa zaka kwani nyie ni wayahudi?
 
Back
Top Bottom