Mrejesho wa kutafuta kazi

Mrejesho wa kutafuta kazi

Kama uko seriuos piga namba hiyo kwenye tangazo
Screenshot_20240823-223631_WhatsAppBusiness.jpg
 
All the best mwamba,binadamu tunapitia changamoto tofauti tofauti,muhimu kila hatua dua isikosekane! Mimi ni mdau wa ujenzi....naweza kuku accomodate kwa ujira wa 15000 kwa siku kwa msaidizi wa fundi tatizo ushasema una hitilafu ya kiafya!
Shukurani sana mkuu kwa msaada wako. Mimi nabeba sio zaidi ya kg 30 kwa vitu vizito hata niliowahi kuongea nao wanajua hilo. Sasa sijajua kwa sector yako kama ina vitu vizito zaidi au la
 
Ila kuacha kazi kwa sababu wanalipa katikati na mwezi wa mwezi haijakaa poa. Labda ungesema mshahara ni mdogo au mazingira ya kazi ni magumu, tungeweza kuelewa.
Mkuu sio kama nimeacha kazi zaidi sababu hiyo hapana. Kumbuka kuna nauli ya kwenda na kurudi kazini then family nayo inabidi ile, yote ndo inabidi itoke kwenye hiyo hiyo hela ndo maana nikasema hivyo
 
Habari za siku kadhaa ndugu zangu.

Narudi tena kwenu wakuu. Week kadhaa zilizopita nilileta bandiko la kutafuta kazi hapa, sipendi nieleze tena mapito yangu ila nataka kusema tu bado kwa upande wangu giza ni kubwa sioni mwangaza

Nimejaribu haya kwa upande wangu

1. Nimejaribu viwandani, nilienda kiwanda cha rasta pale mbagala lakini nilishindwa sababu ya kwamba hawalipi kwa siku wao wanalipa katikati ya mwezi na mwisho wa mwezi, ambapo kwa upande wangu ni vigumu sababu mimi nahitaji hela ya mlo wa siku na familia. Sikuweza kwenda viwanda vya kubeba vitu vizito sababu nina shida ya mbavu

2. Nimejaribu kusema na ndugu zangu wa karibu japo wanikopeshe mtaji nifanye business, niliwaza kufanya biashara ya kuku wa kuchoma, phone accessories, vile visendo vya kina dada au nyingine yoyote mradi kipatikane kipato kwa siku lakini bahati mbaya ndugu nao wanasema hawana kitu

3. Nimejaribu kutafuta mteja ili niuze eneo langu lipo huko mkoa wa kusini nusu eka, nililinunua nilipokuwa huko maana nilipata kazi ya kusimamia mradi wa mtu kwa muda. Lengo ilikuwa niuze nipate mtaji maana sina jinsi, lakini nalo kwa bahati mbaya sijapata mteja mpaka sasa

4. Nimejaribu kadili ya uwezo wangu kutafuta channels sehemu tofauti tofauti lakini wapi! Bado naona giza



Naishi vipi sasahivi?

Kiukweli kwasasa wife ndio anapush jahazi hivyo hivyo mdogo mdogo. Ipo hivi, baada ya upande wangu kuona mambo magumu ikabidi nimwambie yeye ajaribu kutafuta hata hizi za mama lishe za 3000 kwa siku, Mungu ni mwema kweli kuna sehemu amepata ndio hapo anajishikiza, akipata hiyo 3k akitoa nauli 1000 inabaki 2000 ndo anarudi na chochote cha kula siku hiyo.


Kwanini nimerudi tena? Nataka nini?

Kiukweli ndugu zangu hii ishu anayofanya wife mpaka mwenyewe namuonea huruma, huwa ananieleza changamoto anazokutana nazo nadhani wenyewe mnajua wanayopitia mama lishe, mbali ya hizo changamoto ni kwamba ikitokea siku biashara imeenda vibaya basi ndo harudi na chochote. Kwa upande wangu nashindwa tena kutoka kuangaika sababu yeye akitoka asubuhi mimi nabaki na watoto kuwazingatia mpaka usiku anaporudi kwahiyo siku inaisha hivyo.

Sasa nimerudi tena kuwaomba ndugu zangu, sihitaji msaada wa pesa hapana ila nipe tu kazi kama unayo ambayo naweza kupata kuanzia 5000 kwa siku utakuwa umenisaidia sana ili tu huyu mama nimpumzishe nyumbani awalee watoto wake vizuri. Hiko ndicho ninachohitaji ndugu zangu hata kama kazi yako inatoa ujira kwa mwezi, me nilipe tu kwa siku ili family ipate kula basi! Vinginevyo naona kabisa mzigo unanielemea halafu wa kunitetea sina


Kuna muda napata mawazo mabaya ya kumkosea Mungu lakini kila nikifikiria naona hata! Huu mzigo ni wangu sina wa kumuachia! Labda ningekuwa mwenyewe pengine ningesema nikajaribu maisha nchi za watu hapa bongo pamenikataa.

Naomba mnishike mkono ndugu zangu. Asanteni, usiku mwema
Mkuu pole sana kwa changamoto unayopitia
Mimi ni semi jobless lakin nimeumia sana kwa changamoto

Kama upo dar es salaam ni PM upate hata kimchongo ujipatie kipato mkuu kikubwa unamiliki smartphone so mbaya njoo ujaribu networkmarketing mkuu🙏
 
Habari za siku kadhaa ndugu zangu.

Narudi tena kwenu wakuu. Week kadhaa zilizopita nilileta bandiko la kutafuta kazi hapa, sipendi nieleze tena mapito yangu ila nataka kusema tu bado kwa upande wangu giza ni kubwa sioni mwangaza

Nimejaribu haya kwa upande wangu

1. Nimejaribu viwandani, nilienda kiwanda cha rasta pale mbagala lakini nilishindwa sababu ya kwamba hawalipi kwa siku wao wanalipa katikati ya mwezi na mwisho wa mwezi, ambapo kwa upande wangu ni vigumu sababu mimi nahitaji hela ya mlo wa siku na familia. Sikuweza kwenda viwanda vya kubeba vitu vizito sababu nina shida ya mbavu

2. Nimejaribu kusema na ndugu zangu wa karibu japo wanikopeshe mtaji nifanye business, niliwaza kufanya biashara ya kuku wa kuchoma, phone accessories, vile visendo vya kina dada au nyingine yoyote mradi kipatikane kipato kwa siku lakini bahati mbaya ndugu nao wanasema hawana kitu

3. Nimejaribu kutafuta mteja ili niuze eneo langu lipo huko mkoa wa kusini nusu eka, nililinunua nilipokuwa huko maana nilipata kazi ya kusimamia mradi wa mtu kwa muda. Lengo ilikuwa niuze nipate mtaji maana sina jinsi, lakini nalo kwa bahati mbaya sijapata mteja mpaka sasa

4. Nimejaribu kadili ya uwezo wangu kutafuta channels sehemu tofauti tofauti lakini wapi! Bado naona giza



Naishi vipi sasahivi?

Kiukweli kwasasa wife ndio anapush jahazi hivyo hivyo mdogo mdogo. Ipo hivi, baada ya upande wangu kuona mambo magumu ikabidi nimwambie yeye ajaribu kutafuta hata hizi za mama lishe za 3000 kwa siku, Mungu ni mwema kweli kuna sehemu amepata ndio hapo anajishikiza, akipata hiyo 3k akitoa nauli 1000 inabaki 2000 ndo anarudi na chochote cha kula siku hiyo.


Kwanini nimerudi tena? Nataka nini?

Kiukweli ndugu zangu hii ishu anayofanya wife mpaka mwenyewe namuonea huruma, huwa ananieleza changamoto anazokutana nazo nadhani wenyewe mnajua wanayopitia mama lishe, mbali ya hizo changamoto ni kwamba ikitokea siku biashara imeenda vibaya basi ndo harudi na chochote. Kwa upande wangu nashindwa tena kutoka kuangaika sababu yeye akitoka asubuhi mimi nabaki na watoto kuwazingatia mpaka usiku anaporudi kwahiyo siku inaisha hivyo.

Sasa nimerudi tena kuwaomba ndugu zangu, sihitaji msaada wa pesa hapana ila nipe tu kazi kama unayo ambayo naweza kupata kuanzia 5000 kwa siku utakuwa umenisaidia sana ili tu huyu mama nimpumzishe nyumbani awalee watoto wake vizuri. Hiko ndicho ninachohitaji ndugu zangu hata kama kazi yako inatoa ujira kwa mwezi, me nilipe tu kwa siku ili family ipate kula basi! Vinginevyo naona kabisa mzigo unanielemea halafu wa kunitetea sina


Kuna muda napata mawazo mabaya ya kumkosea Mungu lakini kila nikifikiria naona hata! Huu mzigo ni wangu sina wa kumuachia! Labda ningekuwa mwenyewe pengine ningesema nikajaribu maisha nchi za watu hapa bongo pamenikataa.

Naomba mnishike mkono ndugu zangu. Asanteni, usiku mwema
Pole sana mkuu.
M,Mungu akufanyie wepesi katika kila jambo lako inshaallah..

Mungu akupe roho ya subra kaka angu.
 
Hiyo ni kampuni kaka inaitwa Chanika Poultry farm ltd.
WaAlishaji wa kuku wa nyama na mayai. Ni kweli huwa wanatoa ajira Kwa vijana wengi tu na vigezo ni kwamba uwe na TIN number, kitambulisho Cha taifa au namba, cheti at least Cha form 4 au hata kama huna maana Kuna kazi za nguvu tu.
Changamoto itakayompata ndugu yetu ni kwamba pale wanalipa Kwa mwezi, Yani Kila tarehe 30 hata ukianza kazi Leo ikifika tarehe 30 mnalipwa wote.
Mkuu hawa kwa sababu nipo nao karibu kesho j'pili nitaenda kuwaona ili nipate maelekezo zaidi maana kwa vigezo hivyo hapo ninavyo vyote na zaidi nina certificate ya poultry training niliipata Silverland Iringa
 
Kwa nini uzi wa kwanza umeufuta mkuu?
View attachment 3077764

Vipi huyu jamaa ulimcontact?

View attachment 3077766
Mkuu kuhusu kufuta uzi naweza nikawa na sababu ambayo kwa mwingine haina maana, ila yote kwa yote ni ile kila nilikuwa nikiusoma napata huzuni tu kwa mapito yangu ndo maana nikafuta. Kuhusu huyo mdau hakuweza kunisaidia sababu alisema nipo mbali nisingeweza kazi, japo nilimsihi kuwa nitaweza lakini haikuwezekana
 
Halafu baadaye ukifanikiwa nawe uje useme hela ya mwanamke ni yake au mwanamke akihudumia familia kidogo anaanza dharau kwa mumewe, halafu baada ya hapo uachane naye kisha uanze kutafuta wanawake wazuri ambao walikukataa kipindi ambacho ni kapuku, nyuzi kama hizi kina Natafuta Ajira huwa wanajifanya hawazioni wao wanaziona zile za wanaofanyiwa mabaya tu na wanawake
 
Halafu baadaye ukifanikiwa nawe uje useme hela ya mwanamke ni yake au mwanamke akihudumia familia kidogo anaanza dharau kwa mumewe, halafu baada ya hapo uachane naye kisha uanze kutafuta wanawake wazuri ambao walikukataa kipindi ambacho ni kapuku, nyuzi kama hizi kina Natafuta Ajira huwa wanajifanya hawazioni wao wanaziona zile za wanaofanyiwa mabaya tu na wanawake
Akipata atamtafuta WA hadhi yake
 
Halafu baadaye ukifanikiwa nawe uje useme hela ya mwanamke ni yake au mwanamke akihudumia familia kidogo anaanza dharau kwa mumewe, halafu baada ya hapo uachane naye kisha uanze kutafuta wanawake wazuri ambao walikukataa kipindi ambacho ni kapuku, nyuzi kama hizi kina Natafuta Ajira huwa wanajifanya hawazioni wao wanaziona zile za wanaofanyiwa mabaya tu na wanawake
Hapana mkuu namuomba Mungu aepushe hilo
 
Back
Top Bottom