Mrejesho wa kutafuta kazi

All the best mwamba,binadamu tunapitia changamoto tofauti tofauti,muhimu kila hatua dua isikosekane! Mimi ni mdau wa ujenzi....naweza kuku accomodate kwa ujira wa 15000 kwa siku kwa msaidizi wa fundi tatizo ushasema una hitilafu ya kiafya!
Shukurani sana mkuu kwa msaada wako. Mimi nabeba sio zaidi ya kg 30 kwa vitu vizito hata niliowahi kuongea nao wanajua hilo. Sasa sijajua kwa sector yako kama ina vitu vizito zaidi au la
 
Ila kuacha kazi kwa sababu wanalipa katikati na mwezi wa mwezi haijakaa poa. Labda ungesema mshahara ni mdogo au mazingira ya kazi ni magumu, tungeweza kuelewa.
Mkuu sio kama nimeacha kazi zaidi sababu hiyo hapana. Kumbuka kuna nauli ya kwenda na kurudi kazini then family nayo inabidi ile, yote ndo inabidi itoke kwenye hiyo hiyo hela ndo maana nikasema hivyo
 
Mkuu pole sana kwa changamoto unayopitia
Mimi ni semi jobless lakin nimeumia sana kwa changamoto

Kama upo dar es salaam ni PM upate hata kimchongo ujipatie kipato mkuu kikubwa unamiliki smartphone so mbaya njoo ujaribu networkmarketing mkuu🙏
 
Pole sana mkuu.
M,Mungu akufanyie wepesi katika kila jambo lako inshaallah..

Mungu akupe roho ya subra kaka angu.
 
Mkuu hawa kwa sababu nipo nao karibu kesho j'pili nitaenda kuwaona ili nipate maelekezo zaidi maana kwa vigezo hivyo hapo ninavyo vyote na zaidi nina certificate ya poultry training niliipata Silverland Iringa
 
Kwa nini uzi wa kwanza umeufuta mkuu?
View attachment 3077764

Vipi huyu jamaa ulimcontact?

View attachment 3077766
Mkuu kuhusu kufuta uzi naweza nikawa na sababu ambayo kwa mwingine haina maana, ila yote kwa yote ni ile kila nilikuwa nikiusoma napata huzuni tu kwa mapito yangu ndo maana nikafuta. Kuhusu huyo mdau hakuweza kunisaidia sababu alisema nipo mbali nisingeweza kazi, japo nilimsihi kuwa nitaweza lakini haikuwezekana
 
Halafu baadaye ukifanikiwa nawe uje useme hela ya mwanamke ni yake au mwanamke akihudumia familia kidogo anaanza dharau kwa mumewe, halafu baada ya hapo uachane naye kisha uanze kutafuta wanawake wazuri ambao walikukataa kipindi ambacho ni kapuku, nyuzi kama hizi kina Natafuta Ajira huwa wanajifanya hawazioni wao wanaziona zile za wanaofanyiwa mabaya tu na wanawake
 
Akipata atamtafuta WA hadhi yake
 
Hapana mkuu namuomba Mungu aepushe hilo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…