Unajua mkuu mimi nafikiri wewe haukusoma mwanzo wa hili sagala, ndomaana sioni sabahu ya kukulaumu. Ni hivi huyo mmama alikuwa anamtesa huyo mtoto muda mrefu tu na mimi na mke wangu tulikuwa tunajua kinachoendelea, mpaka kufikia hatua ya huyo mmama kugombana na mke wangu kisa akija kucheza na watoto wangu tunampa chakula na wenzake wanakula wote kwa sababu mama wa kambo alikuwa hampi chakula mpaka pale baba yake anapokuwa karibu.
Pamoja na kugombana na mke wangu kisa anampa mtoto chakula na vihela kidogo vya kununua pipi na wenzake, lakn bado tuliendelea kuweka siri ile ili tusiharibu ndoa ya watu. Hili nilikuwa nalijua na kujiepusha nalo kitambo sana. Mziki ulikuja nilipompelekea mtoto nguo na kumkabidhi mama wa kambo. Nikamwambia kistarab tu kwamba hizo nguo nilikuwa nimemnunulia mwanangu lakini kwa bahati mbaya nimekuta hazimtoshi yani amerefuka. So chukua hizo nguo umpe mtoto, halafu mimi nitamnunulia mwanangu zingine. Ule mmama ukapokea. Kama aliona tatizo kuzipokea, basi angesema shemej wewe nenda nazo tu, ila alizipokea, kesho yake akaenda kununua nguo zingine town, akamsubiri mumewe aje ili afanye jambo.
Kweli mume alipofika akanigeuzia mpira. Akadai kuwa mimi huwa namtaka na mara kibao nimekuwa nikimsumbua lakini anashindwa kumwambia. Eti baada ya kuona hanitaki nikaenda kununua nguo zake (akamuonesha alizoenda kununua yeye dem town kimya kimya) na pia nikamnunulia na mtoto ili iwe rahisi kwa yeye kunikubali mimi kupitia njia ile ya nguo. Kumbuka huyo ni rafiki yangu, hivyo hiyo taarifa ilimuumiza sana kugundua kuwa mimi namtaka mke wake na nimemuhonga hadi nguo. Mwamba akaja nyumbani, bila kuniuliza na kuanza kunishambulia mbele ya mkewe kuwa kitambo namtongoza mkewe, na kama hiyo haitoshi na nguo nimemuhonga. Hii habari ki ukweli ilinishangaza maana mimi sikuwahi kumtongoza huyo mmama, pili hizo nguo alizomuonesha huyo mmama sikuzinunua mimi na wala sizijui, na tatu zile nguo za mtoto ni kweli nilizipeleka kwa ajili tu ya huruma wangu kwa mtoto maana hata nguo alizokuwa anavaa ki ukweli hazikuwa za kuridhisha.
Sasa kama hakutaka nimpe nguo angezikataa ila sio kunisingizia mbele ya mumewe ambae ni best friend wangu kuwa namtaka. Sasa wewe unaona alichofanya yeye kujaribu kuvunja ndoa yangu na mke wangu ni sawa? Mbona mimi sikuwa na mpango wa kuvunja ndoa yake ndomaana sikuwahi kumwambia mumewe anachokifanya kwa mtoto wake wa kambo?
Kama mke wangu asingekuwa anajua kwamba nilifanya vile kwa ajili tu ya mtoto saa hizi si angekuwa ameshaondoka au ndani kungekuwa hakukali? Kifupi kama asingefanya upumbavu wa kumwambia mumewe kuwa namtaka kwa lengo la kunidhalilisha, akaamua tu kuchukua nguo kumvisha mtoto au kuacha kumvisha, au kukataa kupokea nguo nilizipeleka basi mpaka leo angekuwa bado yupo ndani ya ndoa yake na hakuna ambae angekuwa na wazo la kumwambia mumewe maana toka Zamani tulikuwa hatuna mawazo ya kumwambia mchizi mpaka siku aje agundua mwenyewe. Lakini mmama umeharibu kwa kujua kuwa ananikomoa na kunidhalilisha mimi matokeo yake ubaya umemrudia yeye.
2pac anakwambia "The bad seed turn good in this world of G's".