Mrejesho wangu katika jitihada na mchakato wa kufungua biashara, kutafuta vibali katika Mamlaka mbalimbali

Mrejesho wangu katika jitihada na mchakato wa kufungua biashara, kutafuta vibali katika Mamlaka mbalimbali

Ndugu kwa uelewa wangu kupitia huu mchakato nnaoendelea nao, kupata Leseni ya aina ya biashara yangu (Uwakala) hawahitaji kufahamu mtaji (hamna mahali kwenye form panapokutaka ujaze ukubwa wa mtaji wako).
Labda katika TIN, huko watasaidia wataalamu na wazoefu wengine hapa
nasikia ili upate driving licence ni lazima uwe na TIN, nayo inakuaje pia
 
Aisee kuna kipindi nilienda kufatilia license ya guest house ya braza dah sitasahau

kwnz kabisa nilipoenda TRA kufatilia tax clearance skuwa na clue yyte kwmb maelezo unayotoa ndio wa natumia kukadiria kodi yako (nikaeleza viwango vikubwa sana maana bro hakunipa way forward kabisa kinachoulizwa huko[emoji22][emoji22]. .. sijui nae alikuwa hakuwahi kufik huko?)

Jamaa wakanikadiria bana, dah ilikuwa balaaa[emoji3]

Ilibidi tu kufunga biashara yenyewe baadae maana kodi tu ilikuwa ni millions kadhaa kwa mwaka so ilikuwa ni faida mzima tunawapa TRA
 
nje kidogo ya maada,je? ni kiwango kipi cha mtaji mtu anatakiwa awe na TIN na lesini ya biashara.kuna mtu anauza vitu vidogo sana eneo la shule hata mtaji haufiki laki tano ,tuseme anatengeneza vitu wanafunzi wanakula.huyu anayo frame.
lakini kuna mtu anamwaga vitu chini kkoo mzigo wa 2m,huyu analipia kitambulisho cha ujasiliamali
hii inakaaje
Machinga, mamantilie, boda boda nk wote wamesamehewa mkuu. Only wawe na kitambulisho cha mlipa kodi = 20,000/- tu
 
nasikia ili upate driving licence ni lazima uwe na TIN, nayo inakuaje pia

Kwa uelewa wangu Ili umiliki chombo cha moto (Magari na Pikipiki) ndiyo unapaswa kuwa na TIN toka TRA ambayo inaitwa Non-Business TIN. Wamiliki wa driving licence pekee (bila kumiliki chombo cha moto) sidhani kama wanahitaji TIN dada angu.
 
Aisee kuna kipindi nilienda kufatilia license ya guest house ya braza dah sitasahau

kwnz kabisa nilipoenda TRA kufatilia tax clearance skuwa na clue yyte kwmb maelezo unayotoa ndio wa natumia kukadiria kodi yako (nikaeleza viwango vikubwa sana maana bro hakunipa way forward kabisa kinachoulizwa huko[emoji22][emoji22]. .. sijui nae alikuwa hakuwahi kufik huko?)

Jamaa wakanikadiria bana, dah ilikuwa balaaa[emoji3]

Ilibidi tu kufunga biashara yenyewe baadae maana kodi tu ilikuwa ni millions kadhaa kwa mwaka so ilikuwa ni faida mzima tunawapa TRA
Pole sana, ni muhimu kupata mawili matatu toka kwa wazoefu au hata huku mitandaoni esp hapa JF kabla ya kuanza hizi process.... mimi imenisaidia sana kupitia threads zilizopita pamoja na hii, vilinipa mwongozo safi kabisa katka huu mchakato na bado naendelea kujifunza.
 
Mkuu hata sisi tumepita tumepita huko, lengo lako unataka kuwaaminisha wanaJF kuwa TRA tanzania nzima wako hivyo, jaribu na ofisi nyingine ya TRA ili uthibitishe research yako
We jamaa hajasema ofisi zote za TRA Tanzania wako hivyo bali ni ofisi aliyoenda yeye yakamtokea hayo, Mimi pia ilishawahi kunikuta ofisi za TRA Songea mwaka 2017.
 
Update 6. I just posted my last update on the original post.
 
Mifumo ya Taifa bado michanga sana. It will take years kabla ya kuwa sawa na tena ikiwa tunafuatilia na kujumuisha katika mitaala ya elimu katika ngazi mbali mbali. Hii shule haipo popote utafikiri hili taifa ni la wachawi pekee. Shule za msingi wangejumuisha mtaala wa jinsi ya kufungua biashara na hatua zote. Kisha ingesaidia kuwaelemisha hata watoa huduma wasipate nafasi ya kuwazungusha na kuwaogopesha wafanyabiashara wapya. Kwanza kwa nchi yetu inaonekana kama wafanyabiashara wapya wanaogopeshwa kuingia katika biashara ndiyo maana magumashi mengi na umaskini na ukosefu wa weledi katika biashara. Nchi nyingine kufungua biashara ni from dakika 10 hadi 20 you are set to go. Kweli mpaka kutegemea na biashara unaweza hata miaka miwili hujafanikiwa kupata legality yote ya biashara.
 
Back
Top Bottom