Mrejesho wangu nikiwa kama mtumiaji wa tigo post paid Internet, The juice i get is worth the squeeze from my wallet

Mrejesho wangu nikiwa kama mtumiaji wa tigo post paid Internet, The juice i get is worth the squeeze from my wallet

Nataka lipa ya tigo Pesa inawezekana kupata?
UKIWA NA TIGO UNAWEZA USIZIME DATA KWA HIZI BANDO ZENYE UNAFUU MNOO‼️
15G=15000/=, 35GB=30000/=, 48GB=40000/= 72GB=60000/= NA 120GB=100000/=
Bando hizi utakua unazipata kwa miaka miwili mfululizo kila tarehe moja unaingiziwa, KUJIUNGA HUMTUMII MTU YEYOTE HELA,

nakupa maelekezo buree unalipia moja kwa moja tigo kama unavyojiunga vifurush vingine. Huduma hii ni uhakika nikikupa maelekezo unaweza hata kupiga 100 ukaulizia na ukalinganisha maelekezo yangu na ya customer care.
( Airtel pia naunga Huduma ya SME itakayokupa GB kibao kwa gharama kidogo)

Soma maelekezo hapo chini au nicheki 0717700921

JINSI YA KUJIUNGA
Piga *150*01#
➡️Kisha chagua no4
➡️Kisha chagua no 2 (kupata majina)
➡️Kisha chagua no 6 (tigo business)
➡️Kisha chagua no 2 (security deposit)
➡️Kisha chagua no1
➡️Kisha kumbukumbu no weka no yako ya tigo
➡️Kisha weka kiasi kulingana na kifurushi unachotaka kama ilivyo kwenye chat( angalia chat kwenye dp yangu )
➡️Kisha weka no ya siri kudhibitisha!

Ukikamilisha nifahamishe !
 
Wakati kwa 115,000 unapata unlimited ya voda
Nikuulize inakuwa unlimited kweli bila kupunguza kasi, au kuishia njiani kutokana na matumizi yako kwa maana niliona hawa Voda wanaujanja,unpodownload spidi hupunguza ukilinganisha na kuupload na sisi huku tunadownload zaidi kuliko kuupload
 
Nipo natumia huduma hii tangu mwaka jana na msukumo wa kuja huku ilikuwa ni baada ya mitandao kupandisha bei za mabando, nadhani wote mnakumbuka mabando yalikuwa bei chee ila kuna wabongo hawakutosheka wakaanza kuyabipu makampuni ya simu kwamba vifurushi visiwe vina expire, Mb ni chache, n.k. ishu ikafika hadi wizarani ikawa ajenda kubwa, mitandao ikapiga na ndio ukawa mwanzo wa vifurushi kuuzwa bei kali, hakika huwezi jua thamani ya ulichonacho hadi kipotee!!

Ok back to the topic, Nipo na hawa tigo since last year na huu ndio mrejesho wangu.

Kupunguza gharama za internet - Kila mwez naungwa GB 80 kwa shilingi elf 60, hii ni sawa na shilingi 750 kwa kila GB, kwangu ni deal safi kabisa sijui kabisa mambo ya kuzima data,

kumekuwa na mabadiliko ya bei kwa wateja wapya lakini sisi wateja wa zamani hatuguswi na mabadiliko, kwa sasa wateja wapya bei zao hizi hapa.

View attachment 2642869

Upigaji / Wizi - Kuna ule upigaji unakuta umejiunga gb 1 ila ukitumia MB 300 tu unaambiwa bando limeisha au unatumiwa sms kwamba umetumia 75%, Huku sijaona hicho kitu, Natumia router inayohesabu nimetumia gb ngapi, na nikiangalia salio kwenye mtandao kweli naona kuna uwiano. Mfano kwa hapa Kwenye router umetumija GB 2 na MB 207, kwenye salio la tigo inaonyesha zimebaki GB 77 na MB 793, kwa kifurushi changu cha GB 80 pana uwiano.

View attachment 2642874

View attachment 2642890



Speed - Mwanzoni speed nilikuwa napata changamoto nikitumia internet nyumbani nje kidogo ya mji tofauti na nikiwa ofisni sehemu za centre, yani nikifika home nlikuwa napata speed ndogo sana tena ikifika usiku ndio naweza kuzima kabisa, kipindi hiki nilikuwa natumia line yao kwenye simu yangu ya Samsung iliyokuwa na laini 2, Ndipo nilipokutana na kijana wetu wa IT ninapofanyia kazi akanishauri ninunue pocket router sababu ni kifaa maalum kwajili ya kukusanya mawimbi ya Net, Hio router ni 75,000 lakini niliingia group la facebook la mkoa nilipo nikapata iliyotumika kwa 20,000, niliongezea elf 10 ya mwanasheria kutuandalia mkataba wa kuuziana (mkataba unilinde endapo router ni ya wizi).

niliambiwa niiweke dirishani ila kwa eneo nilipo speed ilipanda kidogo, kijana wa IT alikuja nyumbani kwangu akakonnect wifi anadownload muvi kwenye simu yake huku anatembea na router anaipitisha maeneo kadhaa ya mle ndani anacheki sehem yenye speed kubwa, alipoiweka juu ya mlango speed ikafika MB 2 kwa sekunde, ndio sehemu nayotegesha router kila niwapo nyumbani.

View attachment 2642928

Malipo - Kila Tarehe 1 inapofika bando linaingia , Napewa siku 9 za kukamilisha malipo kuanzia tarehe 1 hadi tarehe 9.

View attachment 2642865

Mobility - Niliwahi fikiria kufunga nyumbani fibre ya ttcl elf 50 kwa mwezi unlimited, tatizo likawa ni mobility (utumiaji wa sehemu zaidi ya moja) ndipo paliponishinda, pia umeme ukikatika haitumiki, nguzo zikidondoka hakuna huduma, n.k. ni tofauti na post paid nabeba ki router changu sehemu yoyote napoenda hata nikiwa na drive.
Mkuu nashukuru sana kwa kunionesha hili chimbo maana hawa wezi Halotel wananiumiza kichwa!
 
Upigaji / Wizi - Kuna ule upigaji unakuta umejiunga gb 1 ila ukitumia MB 300 tu unaambiwa bando limeisha au unatumiwa sms kwamba umetumia 75%, Huku sijaona hicho kitu, Natumia router inayohesabu nimetumia gb ngapi, na nikiangalia salio kwenye mtandao kweli naona kuna uwiano. Mfano kwa hapa Kwenye router umetumija GB 2 na MB 207, kwenye salio la tigo inaonyesha zimebaki GB 77 na MB 793, kwa kifurushi changu cha GB 80 pana uwiano.




Mnadanganya mpaka mnapitiliza unaposema kifurushi chako cha gb 80 ilhali kwenye chat hakuna kifurushi hicho unakuwa mnajisikiaje.....tangazo la kibiashara haihitaji uongo wa wazi wa kiwango hicho
 
Back
Top Bottom