Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 57,951
- 32,619
Mrembo albino ajiondoa katika mashindano ya Miss Mwanza
Na Paulina David, Mwanza
MREMBO Grace Wabani (23) amejiondoa kwenye mashindano ya kumsaka mrembo wa Mkoa wa Mwanza yanayotarajia kufanyika Juni 5 mwaka huu katika Uwanja wa CCM, Kirumba jijini hapa.
Grace ambaye ni mlemavu wa ngozi (albino) amejiondoa katika mashindano hayo kutokana na kile alichokieleza kuwa amejikuta akitumia muda mwingi katika maandalizi ya mashindano hayo na hivyo kukosa muda wa masomo.
Alisema kutokana na hali hiyo ameogopa kurudia mwaka kutokana na kushindwa kufanya vizuri katika mitihani yake.
Mie sikujua kama mashindano ya U-Miss mtu anatumia muda mwingi sana katika maandalizi, lakini nilipogundua kuwa muda mwingi unatumika na masomo nimesimama nimeona niache tu kushiriki ili niendelee na masomo,î alisema
ìUnaju mie nilikuwa sijafanya baadhi ya mazoezi na hivi sasa tunajiandaa kwa ajili ya mitihani ya mwisho wa mwaka sasa kama nitashindwa kufanya vizuri kwenye mitihani yangu ni wazi kuwa nitarudia mwaka, jambo ambalo litanipotezea muda,î alisema Grace
Alisema kuwa yeye ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT), akisomea masomo ya ugavi na kwamba kuacha kwake kushiriki mashindano ya urembo hakuhusiani na shinikizo la mtu yoyote, bali ni maamuzi yake binafsi baada ya kupima uzito wa masomo na urembo.
ìMie najua watu watasema mengi , lakini ukweli nimeangalia faida ya kushiriki mashindano ya urembo halafu nirudie mwaka ama kuacha kushiriki halafu niendelee na masomo, nikaamua kuchagua,î alisema.
Kwa upande wa mratibu wa mashindano hayo, Flora Lauwo amethibitisha mrembo huyo kujiondoa kwenye mashindano hayo ya urembo tangu Mei 31 mwaka huu.
Na Paulina David, Mwanza
MREMBO Grace Wabani (23) amejiondoa kwenye mashindano ya kumsaka mrembo wa Mkoa wa Mwanza yanayotarajia kufanyika Juni 5 mwaka huu katika Uwanja wa CCM, Kirumba jijini hapa.
Grace ambaye ni mlemavu wa ngozi (albino) amejiondoa katika mashindano hayo kutokana na kile alichokieleza kuwa amejikuta akitumia muda mwingi katika maandalizi ya mashindano hayo na hivyo kukosa muda wa masomo.
Alisema kutokana na hali hiyo ameogopa kurudia mwaka kutokana na kushindwa kufanya vizuri katika mitihani yake.
Mie sikujua kama mashindano ya U-Miss mtu anatumia muda mwingi sana katika maandalizi, lakini nilipogundua kuwa muda mwingi unatumika na masomo nimesimama nimeona niache tu kushiriki ili niendelee na masomo,î alisema
ìUnaju mie nilikuwa sijafanya baadhi ya mazoezi na hivi sasa tunajiandaa kwa ajili ya mitihani ya mwisho wa mwaka sasa kama nitashindwa kufanya vizuri kwenye mitihani yangu ni wazi kuwa nitarudia mwaka, jambo ambalo litanipotezea muda,î alisema Grace
Alisema kuwa yeye ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT), akisomea masomo ya ugavi na kwamba kuacha kwake kushiriki mashindano ya urembo hakuhusiani na shinikizo la mtu yoyote, bali ni maamuzi yake binafsi baada ya kupima uzito wa masomo na urembo.
ìMie najua watu watasema mengi , lakini ukweli nimeangalia faida ya kushiriki mashindano ya urembo halafu nirudie mwaka ama kuacha kushiriki halafu niendelee na masomo, nikaamua kuchagua,î alisema.
Kwa upande wa mratibu wa mashindano hayo, Flora Lauwo amethibitisha mrembo huyo kujiondoa kwenye mashindano hayo ya urembo tangu Mei 31 mwaka huu.