Mrembo hajui kumuandaa kuku

Mrembo hajui kumuandaa kuku

Mimi kuna mmoja alitumia Unga wa ngano kupika ugali akidhani kuwa ni unga wa sembe.

Na kitu ambacho nilishindwa kuamini alipika kabisa. Haya mambo haya aisee

alikupkia ugali wa kwetu makete mtam sana huo ugali
 
Hello wana Chit - Chat

Nilikuwa napiga story ofisini na mates wenzangu tulikuwa na story za namna ya kuimaliza weekend ya mwisho wa mwezi bila vishawishi vya kutumia pesa ovyo ndio ikaja topic ya jinsi hali ngumu ya uchumi ilivyofanya watu wabadili utaratibu wa kula makange, pizza na burger huko kwenye food corners na maeneo mbalimbali ya kula bata batani hapa mjini.

Sasa kuna mate wangu akatupa story hii yeye ana mpenzi wake kweli mzuri sana wa sura na umbo ila tabia me sijui nadhani anaijua mpenziwe akatusimulia jinsi alivyochoka na umbumbu wa mrembo wake kwenye masuala ya kuandaa vyakula jikoni. Akasema alimshtukia mrembo siku myingi kuwa kwenye mapishi yuko ovyo hivyo akaamua kukaza a hapo hapo ili ajiridhishe kama ni kweli au hisia zake tu.

Huyu jamaa alipata kijisafari cha mkoani week zilizopita wakati anarudi akabeba kuku wa kienyeji huko njiani. Weekend iliyofuata akamkaribisha mrembo waje wamshughulikie. Jamaa anasema alimtafuta hamisi chinjachinja wa mtaani akampiga kisu ili awe "halal" kazi ikaangukia kwa mrembo sasa. Mrembo hajui manyoya kama hutolewa na maji moto jamaa akatoa maelekezo maana aliona mrembo haelewi namna ya kumnyonyoa kuku manyoya
Mrembo akafanikiwa kuweka maji moto na kuanza shughuli ya kumtoa manyoya kuku huku amenuna hamna mfano ☹️☹️☹️
Baada ya kumnyonyoa kilichofuata hapo ni kumkata vipande maana kama mjuavyo kuku ana vipande vyake kadhaa vinajulikana kwa macho na majina kama vile paja, kipapatio, shingo, firigisi na kadhalika jamaa anasema aliondoka jikoni akamuacha mrembo aendelee na phase (hatua) ya pili
Anasema baada ya muda mfupi aliamua kumchungulia mrembo wake ili kujua anaendeleaje na mambo ya butcher akakuta mrembo yuko busy anakataka nyama kwa mtindo wa ajabu kabisa alikuwa anakatakata vipande vidogo vidogo kama vya mishkaki . Jamaa akaona hii kali lakini alijipa moyo kuwa labda mrembo ana mikato yake ila jamaa anasema alikosa raha hakuamini alichokiona akaamua amuache aendelee kuandaa yule ndege kwa style ile mpya machoni pake.

Baadae akaendela na mapishi kule jikoni akapika na wali jamaa anasema alishindwa kula hata kipande kidogo maana kuku alikuwa haeleweki shingo imechanganyika na kipande cha kipapatio badala yake nyama ikawa inatisha sio kidogohalafu anasema ilikuwa na harufu ya mavi ya kuku anahisi utumbo ulikatwa katwa na hivyo kinyesi kikatapakaa kwenye minofu

Jamaa amepanga mkakati kwa sasa anafanya utaratibu wa kumtafutia kisa kidogo tu mrembo yule ili amuache mara moja ameona hana vigezo vinavyoendana na mambo ya jikoni. Mrembo ana miaka 24 hajui kuandaa kuku mbichi amezoea kutoa order vibandani " chips kuku paja funga na pilipili pembeni" na akiletewa kuku mwenye manyoya anashindwa kuonyesha hilo paja na kidari viko wapi

Weekend njema wana Chit-chat
Jamaa yuko right amtafutie tu kisa wanalizane
 
Wanaume wengine hata kuku mwenyewe kumuandaa na kumgawa vipande hawajui. Mifano ipo. Hatupendagi ujinga siye. Ngoma drooo. Yaani hata boxer kufua ni matata hapo mnasemaje? Yaani it plays both ways kama Mzazi hujasimama imara kulea Watoto kujitegemea. Endekezeni Kuwatumikisha ma house boy and girls na mtavuna. Mtu zima hata shoe shine kiatu chake na kupasi mzigo. Eti anasubiria akioa mke awe punda, ngamia, kihongo na tractor la kumfanyia Kazi. Khaaaaaa bora ubaki kwenu uendelee kulelewa na mamako tu.
 
Jamaa yuko right amtafutie tu kisa wanalizane
Aiseee na wanaume wanaosoma magazeti na kukodolea macho vituo vyite vya tv vya mioira na muereka nyumbani wakitumia wake zao kama tractor la Kubota, ngamia na punda itabidi kumalizana haraka zaidi.
 
Hii imenifundisha story moja wakati tunakuwa, baba mmoja jirani yetu alikwenda Egypt kusomea medicine, kula alikutana na binti wa Kiegypt na walioana na kupata watoto, ile family tuliishi nayo mtaani lakini familia ya baba na mama wote madaktari, watoto walikuwa ni kusoma tu, hata kuwe na birthday mtaani hatukuwaona.

Basi yule binti alipata mchumba kijana wa kiarabu, kwao walikuwa na mali, lakini familia yote waliishi nyumba moja. Baada ya harusi na honeymoon ndiyo maisha ya ndoa yalianza pale, walipewa chumba chao self contained. Kupika wanawake ndiyo wapishi, kuanzia mke wa kaka mkubwa mpaka wa mdogo. Chai yao ilinywewa saa nne asubuhi, maandazi ya chai yanaanza kukandwa saa moja na jogoo anataarishwa kila asubuhi.

Ilipofika zamu ya jirani yangu sasa, amewekewa unga akande maandazi na kuku amechinjwa, wakwe, mawifi, mashemeji, wake wenza wanasuburi chai, walipoona vinachelewa walikwenda jikoni, kukuta jogoo ameshaiva kwenye maji yaliyochemshwa kwa kukunyonyolea kuku.
 
Umenikumbusha my best friend
Yeye aliwahi kunambia hawezi kumuandaa kuku kwenye kumnyonyoa kuku anaweza ila kwenye suala la kumtoa utumbo na kumkatakata hawezi.Ikifikaga hatua hiyo mamake au mdogo wake wa kiume anashughulika mana yeye hawezi.
Hajui kabisa kupika chapati wala maandazi na yupo comfortable kabisa wala hajishughulishi ajue.
Sasa hivi ni mke wa mtu nadhani atajifunza.
Malezi ndo yanachangia mtu kuwa hivo.
Kuna vitu unapofanya ndo unajifunza hivo kama hufanyi au hata kutaka kujaribu hutokaa ujue.
 
Mwanamke ambaye hajui kupika apite kuleee! Yani kupika hajui na hela anaomba,, shwainn!!
"the way to a man's heart is through his stomach", endeleeni na undezi tu!
 
AHAHAAA HAJUI KUMFANYIA KUKU OPERESHENI KAKATIA HUMO HADI UTUMBO NA MAVI YAKE
 
Back
Top Bottom