Mrisho Gambo acha Unafiki

Inaweza kuwa jamaa naye anashida zake,lakini alichokisema ni sahihi kabisa.

Rejea kwa Makonda hata PM alikuwa hatii mguu..achilia mbali hawa mawaziri na wengine.
Uyu jamaa nafikiri we humjui ni mnafiki Sana kwani yeye alikua anagombana na lema Mara ngapi ametumia nafasi yake Kama mkuu wa mkoa kuminya haki za wapinzani Leo anakuja kujisafisha kipumbavu namna hii Bora akae kimya tu
 
Hiki ndicho alichokiongea Mrisho Gambo kweli? Mzaramo aliyesoma kwa kubahatisha hapo Kibaha, kisha kupewa ukuu wa mkoa Arusha na kutetewa pamoja na kushambuliwa na aliyekuwa mbunge G Lema leo hii anadaia alikuwakuwa anapewa maagizo kutoka juu kutekeleza halafu anasema hadharani siri aliyoapa kutoitoa popote ila kwa utekelezaji wa majukumu yake, huku watu tayari walishaumia kwanini hakujiuzulu kuonesha kutoridhika na mwenendo wa kiuongozi uliopita kama sio unafiki na uzandiki, majungu , chuki na dharau zinazohitaji.

Huyu ni msaliti, mwenye tamaa na ndumila kuwili anayetaka uteuzi wa cheo cha uwaziri tu kwa kutweza na kumdhalilisha aliyekuwa kiongozi wake na mamlaka ya uteuzi.

Je alijaribu kuzuia utaratibu wa nguvu kazi (Task-force) wa TRA wa ukusanyaji mapato kisha akatishwa na mtu yeyote?

Amtaje hadharani kama ilivyoandikwa kwenye mtandao wa kijamii, redio au TV ili kila mmoja amfahamu moja ya watu waliokuwa wanafiki kwa JPM ni nani?
 
Ivi mnadhani kwenye utawala wa yule dhalimu Kuna mtu ambae angethubutu kwenda kinyume chake?? Au mmesahau yaliyomkuta Nape Nnauye na wengineo wengi
 
Amalizie tu ubunge wake atorudi tena bungeni.
Teknologia inatunza kumbukumbu,ukishaiharibu cv yako Katu huwezi iunga
 
Unasahau kuwa Makonda alikuwa na nguvu kupita Samia na Majaliwa?
Mfano mzuri ni huu...hapa bosi ni nani? Mtazame Majaliwa na hiyo body language, kapoa kama maji kwenye mtungi akipokea maagizo kutoka kwa bosi wake Bashite!

Pamoja na hilo, Gambo hawezi kukwepa lawama...analalamika nini hivi sasa? Kwa nini hakujiuzulu? Tatizo ni unafiki na tamaa ya madaraka na hata huo Ubunge wake kabebwa tu!


 
Naona hamtaki watu wazungumze udhalimu ambao alikuwa anaufanye yule kiongozi wa Malaika, Bado yatafichuliwa mabaya yake mengi sana, iko siku atajulikana hadi aliyetumwa akamteke Ben saanane na kwenda kumuua
 
Pamoja na hyo haimnyimi kuongea ukweli, ni mjinga pekee anaweza asimuelewe

Sent from my SM-G973U using JamiiForums mobile app
 

Hayo maneno kwenye tweet ni ya Gambo kweli?
 
Gambo anaomba radhi indirectly kwa kuonesha uovu uliofanywa na mwendazake ktk mkoa amabao yeye alikuwa RC.

Yeye alipokea maagizo toka juu na hakuwa na namna ya kuyakwepa.

Tunataka na HAPI, Chalamila, Mnyeti na Makonda watoke hadharani watubu.
 
Anaogopa kwenda kusemewa kwa Bwana mkubwa
 
Umesema vyema kabisa
 
Wahenga wana msemo, you can't eat your cake and have it! Gambo angefanya la maana kama la kwanza angejiuzulu ubunge...hawezi kulaumu utaratibu uliomwezesha kuwa mbunge wakati akiendelea na ubunge

La pili, angeomba radhi kwa ushiriki wake katika kuwadhulumu wananchi haki zao za msingi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…