Msaada: Ananihudumia, nimeenda kuoa sijui nimwambiaje!

Msaada: Ananihudumia, nimeenda kuoa sijui nimwambiaje!

Nipo kwenye mahusiano na huyu Dada kwa mwaka mmoja na nusu sasa. Hatuishi pamoja lakini muda mwingi nipo kwake, ananihudumia kwa kila kitu. Mimi nafanya kazi lakini kipato changu ni kidogo sana siwezi kuhudumia mwanamke nayeye anajua. Amenilipia kodi kwenye nyumba nzuri, kaninunulia Pikipiki na kila mahitaji yangu yote.

Namshukuru Mungu kwa hilo, wakati naanzisha naye mahusiano nilimuambia kuwa nina mwanamke wangu ambaye yuko mkoa mwingine na anajua tunawasiliana naye. Hakuonekana kuwa na shida na hilo lakini kadri siku zinavyoenda niliona anazidisha wivu hataki niwasiliane na huyo mwanamke, alikua ananibana sana kuna kipindi akamblock mwanamke wangu kwenye simu yangu.

Nilitafuta namba nyingine na kumuambia Mpenzi wangu kuwa ile namba yangu nilipoteza na Voda wakaigawa hivyo asiipige na kweli nikawa nawasiliana naye kimyakimya mpaka sasa. Sababu ya kuja kwako ni hivi, huyu dada alikua analazimishia sana nimbebeshe mimba, mimi nilikua nakwepa sana lakini kama unavyojua haya mambo ukitengewa chakula unakula, ana mimba yangu.

Amelazimisha sana niende kujitambulisha kwao na kutoa mahari lakini nilikua nakataa, alinipa milioni mbili ili kwenda kutoa mahari kwao, nilienda hivyo hivyo nikajitambulisha kwao lakini sikutoa mahari nilimuambia bado mpaka kwetu wajipange kwani Baba alikua anaumwa.

Baada ya kuona kuwa ananisumbua Nilijiona kama mimi ndiyo mwanamke kwake, nilichukua ile milioni mbili, nikaenda kwa mpenzi wangu, nikatoa mahari nusu na kuwaambia kuwa nataka kufunga ndoa ya harakaharaka nimefunga ndoa ya kanisani ilke ya suabuhi tun a watu wachache. Sababu ya kuja kwako ni hivi, namuachaje huyu dada bila kumuumiza kwani pamoja na kwamba ana wivu sana na ni king’ang’anizi sana lakini hajawahi kunifanyia kitu kibaya.
"WEMA NA UBAYA, VYOTE NI MADENI"

Utalipwa tu, MUNGU HAJAWAHI KUSHINDWA.
 
Mkuu angalia usije ukauliwa . USA hata hapo Kwa madiba ukimfanyia hivyo mwanamke anakutafutia hit men for hire unamalizwa faster
 
Umeonesha ulivyo kijana sio mwanaume. Pia bado mshamba wa wanawake. Unatumia pesa ya mwanamke mwingine kuoa mwanamke mwingine utavuna ulichopanda

Kosa ambalo baadhi ya wanaume tunafanya ni kuoa wanawake tunawapenda sana sisi. Mwanaume oa mwanamke anayekupenda zaidi yeye.

Huyo uliyemuoa utarud hapa na unalia. Malipo ni hapa hapa Duniani. Ni suala la muda tu
 
Kwenye miti hakuna wajenzi ndugu ila sikulaumu maana umekosa ushauri,nina hakika utakuja kujitia baadae... Kwa dunia ya sasa kwa wanaume wote oa mtu anayekupenda na kuhofia kukupoteza itakusaidia sana kukutuliza akili yako kuliko kujitafutia matatizo ya kuoa ambao wewe ndo unaonekana unaihitaji sana hiyo ndoa.
 
Back
Top Bottom