Msaada: Gari kuwa na miss na RPM kushuka

Msaada: Gari kuwa na miss na RPM kushuka

Petrol filter umewahi kubadili? Ulibadili genuine? Check kwanza hilo... Kumbuka ni petrol filter sio oil filter
Habarini wakuu, nina gari Toyota Vits RS Manual Transmission. Hii gari ina matatizo yafuatayo:

1.Ina miss ambayo haiishi. Nimesafisha nozzel na plug zote ziko poa.

2. Ukiwasha gari asubuhi RPM inashuka mpaka inazima. Nimeshafanya adjustment ya silencer lakini ikikaa muda inashuka mpaka gari inazima na check engine inawaka baada ya kutembea umbali fulani shida inaweza kuwa nini maana

Jr[emoji769]
 
NIMEFANYA DIAGNOSIS LAKIN HALIJAONESHA KAMA KUNA TATIZO ILA CHECK ENGINE INAWAKA FUNDI AKACHEK FUEL PUMP KUNA KIRABA KIMELIKA HAKIZUII MAFUTA VZURI NDO CHA KUBADILISHA

K vant
Haiwezekani mzee lazima isome ..anatumia mashine gani??.usisumbuke sana nitafute mm nitakupimia bureeee kabisa lkn ukihitaji nikutengenezee hapo ndio utagaramikia kiJF JF usihangaike sana mkuu..
 
Poa mkuu nakutafuta kesho
Haiwezekani mzee lazima isome ..anatumia mashine gani??.usisumbuke sana nitafute mm nitakupimia bureeee kabisa lkn ukihitaji nikutengenezee hapo ndio utagaramikia kiJF JF usihangaike sana mkuu..

K vant
 
Mkuu kwa maelezo yako hayo hapo unashida kama mbili au tatu.

Ishu ya silensa na ukiwasha asubuhi inazima hapo kuna switch inaitwa IDLE SWITCH ndio shida na shida yenyewe lazima itakuwa chafu ingekuwa imekufa ingekuwashia taa ya check engine..hiyo switch inapatikana kwenye throttle body/batter fly..
Hiyo ndio kazi yake kubalans silensa na kuongeza silensa asubuhi au gari ikiwa ya baridi au ukiwasha AC au ukiipa mzigo engine kama ukiweka gear yenyewe inaongeza silens ili kubalans..

Ishu ya hard start umesafisha nozel lkn umesahau petrol filter.. kwanza hapo kuna mawili yaweza kuwa petrol filter chafu sana au mfumo wa mafuta ushachokonolewa hivyo mafuta yanakuwa yana return kwenye tank.hivyo unavyo park gari mda mrefu mafuta yanaludi kwenye tank yote na unavyowasha yanakuwa yanaanza safari na moya yajae kwenye filter kisha yafanye safari mpaka kufika kwenye nozeli lazima gari iwe na hard start mkuu..

Anza na hivyoo kwanza
Jibu zuri sana hili...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habarini wakuu, nina gari Toyota Vits RS Manual Transmission. Hii gari ina matatizo yafuatayo:

1.Ina miss ambayo haiishi. Nimesafisha nozzel na plug zote ziko poa.

2. Ukiwasha gari asubuhi RPM inashuka mpaka inazima. Nimeshafanya adjustment ya silencer lakini ikikaa muda inashuka mpaka gari inazima na check engine inawaka baada ya kutembea umbali fulani shida inaweza kuwa nini maana
Hilo tatzo nlikutana nalo mwaka huu ilipimwa bila shida kuonekana, nilinunua plugs nkajaza mfuko maana kila ukienda kwa mafundi wanadai plugs unanunua tu, engine ilibomolewa mara mbili bila tatzo kuisha, mwisho wasiku nikagundua tatzo mimi mwenyewe kuwa waya wa crankshaft sensor ulikuwa umekatika nikaweka sawa, naenjoy mpaka sasa gari ni namba B lakini mwenye namba D jipange.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom