kama alivyosema mwenzangu hapo juu ni kweli kuna usanii unafanywa na hawa dealers wa gesi,ukiwa unapimiwa kwanza hakikisha unaona reading za mizani na hakikisha iko zero,kisha utoe uzito wa mtungi wako ambao unakuwa steel-printed kwenye mtungi wako,hapo ndipo uakapojua,,,pia ujaribu kununua kwa dealers wengine,kama tatizo litaendelea nakushauri ukague pipe inayoenda kwenye plates na plates zenyewe ili kuhakikisha kwamba hazivujishi gesi,ikibidi badilisha kabisa...(ili kujua kama ni pipe inavujisha gesi,chukua maji yenye sabuni uparaze kwenye pipe kama kuna mahali imetoboka basi itatoa mapovu,fanya hivyo hivyo kwenye sehemu inapoingia kwenye mdomo wa plates.
cha msingi zaidi pia ukague Gas control valves,hizi hazitengenezeki kirahisi,so itabidi uingie mfukoni....pia kumbuka wakati unatumia sabuni ili kugundua leakage HAKIKISHA JIKO LAKO LIMEZIMWA.
nakutakia kila la kheri