Msaada: Hivi vidonge sio ARV?

Msaada: Hivi vidonge sio ARV?

Hazipaswi kua hivyo HIV isikie kwa jirani, fikiria ikupate na dawa zikukatae? Tusiwanyanyapae tu waathirika.
Aaaahh ni kweli kabisa.. Mimi kuna moja ilinitokea nikiwa hospital niliona huruma sana..

Nilimsindikiza rafiki yangu wa kike kupima malaria.. Sasa tumepita kwa doctor akatudirect maabara.. kufika mahabara tukawakuta vijana wawili walionekana kama wapenzi wakiwa wanalazimishana kuingia maabara. Yule wa kiume ndio alikuwa akimlazimisha sana yule binti mwishowe wakaingia. Akili ya fasta nikajua hawa watakuwa wanachuo alafu wapenzi wamekuja kupima UKIMWI.. Basi wakatoka wakaambiwa wasubiri nje, na mie mgonjwa wangu akaingia akatoka akaambiwa turudi kwa doctor. Tukawaacha wale vijana kule.. Basi tuko kwa doctor yule kijana aliyekuwa anapima kule maabara akaja mbio mbio akiwa anahema na sura ilikuwa inaonekana kama kachanganyikiwa.. Nadhani hata sie hakutuona kama tupo mule ndani.. Kwa hamaki na uwoga akamwambia yule doctor.. "Doctor kuna mmoja pale kaumia aisee" Doctor akamuuliza yupi? Yule kijana akajibu "Yule demu kaumia aisee"

Aisee niliumia sana maana anaonekana ni binti mdogo with a promising future.. Lakini na mimi the same week nikafanya mistake ya kufanya ngono zembe na mwanamke ambaye simwamini vizuri.. Ingawa asubuhi yake nilimwambia we made a mistake na mimi siamini afya yako kama vipi twende tukapime.. Yule msichana hakuonyesha wasiwasi alisema yupo tayari lakini bado nina kauoga fulani bado.. Asikudanganye mtu, kupima baada ya kujua umefanya ngono zembe ni mtihani mkubwa sana..
 
Wengi ni wale wavivu wa kunywa dawa wanakunywa leo kesho wanasahau au wanakumbuka baada ya siku tatu, wengine ni kutokana na matatizo ya kisaikolojia, wengine ulevi na utumiaji wa madawa ya kulevya. Watu hawa wanafanya dawa ziwe sugu. Nilikutana na dada mmoja yeye tangu anaanza kutumia dawa zimemkataa, kwahiyo inabidi apewe cocktail na kuchekiwa kila mwezi. Tumaini lake ni hizi dawa mpya zilizogunduliwa sasa.
Mkuu ina maana ukiwa unakunywa hizo dawa pombe huruhusiwi kunywa?

Naomba nilijue hili kwanza kabla sijaenda kupima kwa mara nyingine..
 
Mkuu ina maana ukiwa unakunywa hizo dawa pombe huruhusiwi kunywa?

Naomba nilijue hili kwanza kabla sijaenda kupima kwa mara nyingine..
Unaruhusiwa kunywa lakini ulevi unawafanya wengine kusahau dose. Kunywa kwenyewe pia unywe kwa tahadhari, WHO recommendation ni siku tatu za kupumzika katika siku saba za wiki na ukumbuke units zinazoruhusiwa ni units 14 kwa wiki hii ni sawa na chupa moja ya wine kwa wiki.
 
Anauliza kuhusu hyo PEP?hata mm ningependa kupata shule kidogo

PEP -post exposure prophylaxis
Ni dawa hizo hizo za ARV (TLE-tenofovir,lamivudine na efavirenz)
Anapewa mtu aliyepata exposure ya maambukizi,lakini iwe ndani ya masaa 72 baada ya exposure.
Wanapewa watu waliobakwa,wafanya kazi wa hosp,hata katika discordant couples.
Dawa hizo anatakiwa apewe mapema kabla ya saa 72 kupita tangu amepata exposure ikiwa mapema kabla ya 36 inafanya kazi effectively kwa asilimia >89% lakini ikipita saa 36-72 inaweza saidia kuliko kuacha kutumia.
 
Vinatumika baada ya maambukizi, kwa mfano ikigundulika ulisex na demu mwenye ngoma au kupasukiwa na condom halafu ukawahi hospital wanakuanzishia dozi ya mwezi mzima.
wafanyakazi hospitali ukijidunga sindano au kiwembe kwa bahati mbaya ukimtibu mgonjwa kama mgonjwa akikutwa na maambukizi unatumia. Ila nawewe unapimwa pia kwanza.
 
Huu uzi kwakweli unastahili pongezi maana kwa mara yakwanza humu kuna watu wamekiri madhaifu yao .
1. Wazinzi wameahidi wataacha au kupunguza.
2. Wazee wa CHAPUTA wao wamesema ni vyema kurudi ktk chama chao kuliko kuja kupatwa kama ya mtoa uzi.
3. Wazee wa kuchepuka nao wameonekana kupatwa na hofu kubwa.
4.Wazee wa vibamia,kwa mara ya kwanza wapo waliosema vimkia vyao vimegoma kufunction,hii ikimaanisha wana vimkia yaani vibamia.
 
Huu uzi kwakweli unastahili pongezi maana kwa mara yakwanza humu kuna watu wamekiri madhaifu yao .
1. Wazinzi wameahidi wataacha au kupunguza.
2. Wazee wa CHAPUTA wao wamesema ni vyema kurudi ktk chama chao kuliko kuja kupatwa kama ya mtoa uzi.
3. Wazee wa kuchepuka nao wameonekana kupatwa na hofu kubwa.
4.Wazee wa vibamia,kwa mara ya kwanza wapo waliosema vimkia vyao vimegoma kufunction,hii ikimaanisha wana vimkia yaani vibamia.
Hahahahaha mkuu pongezi zikufikie kwa haya mawazo maana umeifanya wkend yangu Kuwa murua kbs.
 
Back
Top Bottom