Msaada: Kuhusu ugonjwa wa pumu

Mimekuelewa vyema kabisa mkuu ubarikiwe sana....
 

Asante sana Daktari kwa majibu haya mazuri.
 
Na imani hiyo mzee [emoji120] [emoji120] [emoji120]
AMENI , LABDA NIKUELEWESHE KITU !!

[emoji117] [emoji117] KWANN BAMIA ......???
Bamia ni mbogamajani ambayo ina utajiri mwingi wa Vitamin C na Antioxidants nyingi ,, sasa ivi kwa pamoja huzuia kutokea kwa Pumu +kuzuia mashambulizi ya Pumu.
 
AMENI , LABDA NIKUELEWESHE KITU !!

[emoji117] [emoji117] KWANN BAMIA ......???
Bamia ni mbogamajani ambayo ina utajiri mwingi wa Vitamin C na Antioxidants nyingi ,, sasa ivi kwa pamoja huzuia kutokea kwa Pumu +kuzuia mashambulizi ya Pumu.
Kwani zikipikwa zinapoteza hizo vit C
 
Mi nimekunywa hayo madawa ya miti shamba mengi yanakupa nafuu ya muda kama ya hospitali.

Nenda kwa madaktari bingwa wa mapafu watakusaidia.
Nenda upimwe uwezo wako wa kupumua kawaida. Na baadaye watakushauri utumie dawa zipi kwa utaratibu mzuri.
 
Kwani zikipikwa zinapoteza hizo vit C
Aaahhh moja ya sababu kubwa inayofanya deformation ya structure ni Joto. Kutumia bamia zilizopikwa utendaji wake nihafifu .

Ndo maana hata vitunguu vinakua tiba ikiwa utakitafuna kibichi.
 
Mi nimekunywa hayo madawa ya miti shamba mengi yanakupa nafuu ya muda kama ya hospitali.

Nenda kwa madaktari bingwa wa mapafu watakusaidia.
Nenda upimwe uwezo wako wa kupumua kawaida. Na baadaye watakushauri utumie dawa zipi kwa utaratibu mzuri.
Binafsi huko hospitali nimeshazunguka pia, kunakipindi nilipimwa vipimo kadhaa na kupewa dozi ya kipindi kirefu ila dozi ilipoisha baada ya muda flan mashambulizi yakawa yanarudi taratibu.
 
Binafsi huko hospitali nimeshazunguka pia, kunakipindi nilipimwa vipimo kadhaa na kupewa dozi ya kipindi kirefu ila dozi ilipoisha baada ya muda flan mashambulizi yakawa yanarudi taratibu.
Hizo dozi walizokupa ndo zinakusaidia na hutakiwi kuacha.
 
I

Inamaana ni dozi ya maisha sasa haina mwisho
Pumu haina tiba ya kudumu ukapona kabisa. Labda kwa mitishamba ambayo bado kuna watu hata baada ya kutumia hawaponi.

Ulivyosema unatumia aminophyline na salbutamol na uliacha inhaler nikajua hauna watu sahihi wanaokutaarifu.

Ndio maana nikakueleza fanya utaratibu uwaone madaktari bingwa wa mapafu ufanyiwe vipimo sahihi na upewe dawa kutokana na hali yako.

Kwa mfano mimi niko kwenye mazingira ambayo naweza kupata attack mara nyingi lakini nimepewa dawa ambazo zimepunguza sana hizo attack ingawaje nikiwa kwenye mazingira mengine naweza kuwa sawa bila hata dawa.
 
Nadhani utumiaji wa dawa flani hasa za hospitali inategemea na condition au stage ya Pumu iko kwa kiasi gani, mf. sindano na hizo inhaler zinatumika mara nyingi na watu walio na critical conditions sasa nadhani nilivyoambiwa kuacha kutumia hivyo kwa namna moja au nyingine ilionekana kwa condition yangu ntakuwa natumia dozi kubwa sana kuliko ukubwa wa tatizo. Hiyo ni kwa vile ninavyojua
 
Sawasawa.

Kuna inhaler za attack na inhaler za matumizi ya kila siku.

Aminophyline haishauriwi kutumika mara kwa mara.

Viko na vidonge vingi ambavyo pengine huvawahi hata kusikia.

Wakikupima lung test na wakisikia maelezo ya unapata attack mara ngapi kwa wiki/mwezi/mwaka ndo wanakupangia dawa za kutumia kawaida na za kutumia unapopata attack.
 
Hapo nimekupata mkuu, pia itabidi nirudi kwa wataalam kufanya vipimo zaidi ili nijue kwa sasa niko stage gani
 
Hapo nimekupata mkuu, pia itabidi nirudi kwa wataalam kufanya vipimo zaidi ili nijue kwa sasa niko stage gani
Kila la heri. Kumbuka hivyo vipimo vipo hospitali chache za binafsi kubwa kubwa na za serikali najua Muhimbili zipo. Gharama kuanzia laki
 
Loweka karafuu punje kama 12 kwenye glas asubui kunywa fanya hivyo kwa 2weeks
 
Pumu ni mzio....unapaswa ujue ni aalergens gani zina trigger attack...na mara nyingi huanza polepole na sio ghafla. Ukiona umebanwa ujue ilshaanza taratibu. DALILI zake mara kwa mara ni mafua,kupaliwa paliwa na irritating coughs.

Nenda THE PHARMACY pale karibu na hindu mandal hospital au ile branch yao Mkapa towers opozit posta mpya...kanunue nebulizing compressor(Handy Neb) then ununue dawa zake za kufukizia kama wanazotoa hospital kwenye mashine ya gas ukutani...itakusaidia sana
Hizo dozi walizokupa ndo zinakusaidia na hutakiwi kuacha.
 
Mimi nilipoambiwa vituu swaumu vinasaidia kumaliza tatizo hili niliamua kuvigeuza siyo dawa Bali chakula,nakula vitunguu vya kukatakata kila usiku ktk maisha yangu maana niliona wakati Fulani nilianza kuona dalili hasa baada ya stress kunizidi,
Trust me tatizo limepotea kabisa japo bado naendelea kutumia na nimezoea kabisa,kiiiila siku kabla ya kulala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…